Hivi kweli kesho ni siku ya mapumziko?

Hivi kweli kesho ni siku ya mapumziko?

kweli watanzania mmenishinda kweli mkulu kachoka ,serikali yake na raia wote, kazi kwelikweli,
 
Mbona sisi tuko hapa Mnadani tunakula nyama choma na larger bila kuwa na taarifa kama hiyo. Tukio liliochukua muda mrefu kuandaliwa linaweza kubadilishwa kwa kurudishwa nyuma au kupelekwa mbele kirahisi hivyo, tena siku moja kabla !! Huyo Mgeni Rasmi atatoka wapi ? hakuna kitu kama hicho.
Tunakula nyama na tunakunywa Ulevi
 
Huku Mwanza sherehe za 8/8 zinafungwa kesho. Ila sijui ni kwanini??
 
Kwani nimebisha n dugu yangu mie nimeuliza hapa nani mwenye hizo data basi maana watu bado hawajaamini hili kua linawezekana

mimi niko kaskazini, mtoto wangu shuleni kwake walikua waende tr 8 nanenane Arusha wameambiwa wanakwenda kesho kwasababu tr 8 ni Idd nikajua ni uamuzi wa walimu wao ili wawe huru siku ya Idd 8/8, ngoja tusubiri tutapata taarifa.
 
Wabongo kwa kupenda kulala! Kuna jamaa hapa Ofisini kwetu kila mwanzo wa mwaka zikitoka kalenda kitu cha kwanza ni kuangalia sikukuu zimekaaje, furaha yake ni kuona sikukuu ikiangukia Ijumaa au Jumatatu.

Inanikumbusha enzi za Mzee ruksa ilikuwa sikukuu ikiangukia J'pili basi J'tatu hamuendi kazini kulipia ile siku ya sikukuu!
 
Ni kwamba JK anatoa hotuba ya Nane Nane jumatano tarehe 7. Na kufunga rasmi maonesho ya kilimo. Hii ni ili asiamke kabisa siku ya tarehe 8. Ambayo inadaiwa kuwa ni Eid.

Kwa kuwa siku kuu ya Eid, inategemea kuandama kwa mwezi, kama mwezi hautaandama itakuwaje.
 
Back
Top Bottom