Hivi kuunda serikali bila vyama vya siasa haiwezekani?

Jumakidogo

R I P
Jul 16, 2009
1,851
417
Kwanza napenda kutoa pole kwa familia ya marehemu Regia Mtema na watanzia wote kwa ujumla kwa kifo cha mpendwa wetu dada Regia. Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi. AMINA........Nimeanza kuumiza kichwa na kupata kizunguzungu. Kila kukicha kupitia vyombo vya habari utasikia; mara, 'CCM wakabana koo' mara 'CDM yawagaragaza CCM' mara kamati kuu CCM sijui nini....? Hivi demokrasia bila vyama vya siasa katika nchi haiwezekani? Mi naona serikali kavu kavu itapunguza hizi kelele na uhasama kila kukicha. Naona kama mambo ya vyama haya kwa kiasi fulani yanapoteza muda wa watu kufanya kazi, manake tunapoteza sana muda kufuatilia mbwembwe za wanasiasa na kuacha mambo mengine. Kila chama kinapigania kuingia madarakani ili kuongoza serikali. Nauliza tena, je serikana bila chama cha siasa haiwezekani?
 
Utawala/Serikali inaweza ikawepo bila vyama lakini Demokrasia sidhani kama inaweza ikawepo bila vyama vya siasa!
 
Kwa mfumo wa dunia ulivyo sasa tunaweza sema haiwezekani,unless otherwise unabadilisha mfumo wa uongozi kwamba nchi inakuwa na mfalme tu hakuna vyama ama unaanzisha udikteta
 
Nauliza tena, je serikana bila chama cha siasa haiwezekani?

Inawezekana kabisa.Uingereza pamoja na kuwa ina vyama vya siasa ni nchi isiyokuwa na katiba ya nchi.Wao wanaamini sheria zilizopitishwa zinatosha kulinda demokrasia na haki za raia.Hivyo nchi bila katiba ya nchi inawezekana.Na bila vyama vya siasa inawezekana pia.

Ili uwe na nchi bila vyama vya siasa ruhusu wagombea binafsi kuanzia chini udiwani ,ubunge hadi uraisi,Ukuu wa wilaya na mikoa kote chagua watu binafsi kwenye kura.Yawezekana kabisa kufuta hata vyama vyote vya siasa ukabaki na wagombea binafsi.YAWEZEKANA KABISA.Kinachotakiwa ni kuamua kuanza kuzoea wagombea binafsi.Vyama vinaogopa ukiruhusu wagombea binafsi ruzuku zitakufa,wachangiaji watatimka sababu mtu akiwa na pesa yake aweza gombea mwenyewe au akapeleka kwa rafiki yake badala ya chama.
 
Back
Top Bottom