Kuna dhana iliyojengeka miongoni mwa viongozi wengi wa serikali na taasisi zake kwamba yeyote anayetofautiana na CCM au kuikosoa kwenye public basi ni MCHOCHEZI. Mifano ni mingi, lakini tishio la kuyafungia magazeti ya Mwananchi na Mwanahalisi ni mfano mzuri zaidi wa hali hiii iliyojengeka kwenye jamii yetu. Viongozi wa MAELEZO (bila shaka kwa umbumbumbu wao) wanaamini kwamba ukienda tofauti na CCM kimtazamo basi wewe ni mchochezi. Bado wana mawazo mgando na hawajui kwamba tulikwishaondoka siku nyingi kwenye enzi za 'chama kushika hatamu'. Ujinga huu unatoka wapi na tutauondoaje?