Hivi kuna kitu kinaitwa Maadili ya Mtanzania??

SnowBall

JF-Expert Member
Sep 13, 2011
3,054
2,840
Ukilitazama neno MAADILI kwa kiingereza linatafsirika kama 'ethics' au 'morals'...kwa wenye kujua kiingereza vizuri mnaweza kunisaidia kueleza kinagaubaga nini maana ya morals or ethics.. na wale wajuzi wa kiswahili mtaniambia..Ila kwa tafsiri yangu yangu ya kichina..nadhani inamaanisha mambo ambayo kimsingi jamii imekubaliana kwa pamoja kwamba yakifanyika yanaleta mwonekano mwema kwenye jamii..na hii inaweza kuhusisha namna ya kuvaa, kusalimiana..kufarijiana misibani nakadhalika.................

Mada iliyoko mezani ni hii..Katika pita pita zangu za kimaisha hapa juzi kati nilibahatika kupanda daladala na ndani ya daladala kulikuwa na watu wa marika tofauti kuanzia wanafunzi na watu wazima wenye umri wa karibu miaka hamsini. Sasa basi mule ndani ya gari nilipaa na siti but kwa mbele yangu kulikuwa na watoto wa shule wawili wakike nadhani ni wa sekondari umri wa kati 15 na 16.walikuwa wamesimama huku wamebanwa na watu wazima...Sasa kwa kuwahurumia wale wadogo nikawaita na kuwaomba wakae kwenye siti yangu kwa kubebana..Of course kama nilivyosema kulikuwa na watu wazima wamesimama but my sense of humour fell on those poor small girls...

Sasa wakati mie nimesimama nikasikia siti za nyuma watu wakilalamika kuwa 'Maadili ya Mtanzania yameshuka kwamba nawezaje kuwaachia wanafunzi wakae ilhali kulikuwa na watu wazima wamesimama'..Niliupenda mjadala lakini kwa kuwa nilishukia jirani sikujua uliishaje..Baadaye nikiwa zangu njiani nikaanza kujiuliza maswali..Hivi ni kweli kuna kitu kama maadili ya Mtanzania?..na kama yapo hivi yanafundishwa wapi??..Binafsi kwa kuishi kwangu..mara nyingi katika kufanya maamuzi ya mambo yanayonikabili natumiaga busara ya dini yangu na ikizidi kabisa basi nitaconsult wazee wa kabila letu au zaidi nayatafakari tu kwa upeo wangu mwenyewe na kufanya maamuzi..lakini ever sijawahi kujua yapi ni maadili ya Mtanzania..kiasi kwamba naweza kusimama na kujitambulisha nayo...

Probably kama kuna mtu anayajua haya yanayoitwa..'Maadili ya Mtanzania'..hebu ajaribu kunielewesha basi!!..Manake kila kukicha tunalalamika watoto wa siku hizi hawana maadili..hivi ni kweli zamani yalikuwepo?? na ni kweli kwamba hayo ya zamani ndiyo yanamtambulisha Mtanzania??....lol!
 
mh pacha leo umetoka kivingine leo!hii outing yako ya leo toka asubuhi mimi penda sana
:focus:maadili ya kitanzania yapo
kuna kitu kinaitwa mila na desturi,mila zinaweza kuwa ni za kikabila
lakini desturi tunaweza kuwa nazo kwa kushare yani kama taifa
kwa desturi zetu tukiwa ni watanzania desturi mojawapo ni wadogo kuanza kuamkia wakubwa,kusimama ili wakubwa wakae
kunyamaza wakubwa wanapoongea
kutokujibizana na waliokuzidi umri
kunyamaza wakati wa kula
na mengine meengi
lakini hili la maadili kuwa yapo au hayapo na kilichofanya maadili hayo yasiwepo kwa kweli ni mada pana sana!
ukimbuka malezi tuliyokulia zamani yalikuwa ni malezi funge yaani malezi ya jamii moja ndo mana kulikuwa na theory za wanawake wa mkoa huu wako hiiv ana wa kabila hili wako vile
siku hizi watoto wetu tunawalea malezi huria,yaani ni mchanganyiko kwisha kazi!mtoto anazaliwa na mzazi mchaga na mngoni analelewa na housegirl mhehea u mmakonde!
matokeo yake hata yale tulikuwa tunaamini ndiyo maadili ya kitanzania hayapo
wakati sisi tulikuwa hatuwezi kuhoji amri za wazazi wetu na walimu au wakubwa zetu watoto wetu wanajiona wana hiyo mandate kuna kamsemo wanakatumia wenyewe mum/dad but its not fair
jamii imeanza kulizoea hili tukiamini haya ndo maendeleo
zamani mama anajifungua mtoto wa kiume na mtoto anakuwa treated kama mwanaume since then siku hizi unakuta mtoto wa kiume kasukwa nywele na kavalishwa bangili ,bado tunaweza kutembea kifua mbele kudai tuna maadili ya kitanzania?
zamani tulikuwa tunaamini watoto wanauzwa hospitali au baharini siku hizi wanetu wameenda mbali zaidi muulize gfsonwin akiwa anafundisha biology anakuatana na maswali gani kwenye topic ya reproduction.
wazazi siku hizi tumerelax sana kuhusu malezi,sana tumebaki kuwalaumu walimu na kina dada!
tumewaachia uhuru hawa watoto kiasi cha kutisha kabisa!matokeo yake ndo hayo ya kutokujijua hata kama tuna maadili ya kitanzania au la!
 
Last edited by a moderator:
The difference between ethics and morals can seem somewhat arbitrary to many, but there is a basic, albeit subtle, difference. Morals define personal character, while ethics stress a social system in which those morals are applied. In other words, ethics point to standards or codes of behavior expected by the group to which the individual belongs. This could be national ethics, social ethics, company ethics, professional ethics, or even family ethics. So while a person's moral code is usually unchanging, the ethics he or she practices can be other-dependent.


When considering the difference between ethics and morals, it may be helpful to consider a criminal defense lawyer. Though the lawyer's personal moral code likely finds murder immoral and reprehensible, ethics demand the accused client be defended as vigorously as possible, even when the lawyer knows the party is guilty and that a freed defendant would potentially lead to more crime. Legal ethics must override personal morals for the greater good of upholding a justice system in which the accused are given a fair trial and the prosecution must prove guilt beyond a reasonable doubt.
 
Hizi mila na desturi ni universal??..mtu wa Kigoma anaweza kuziobserve kama alivyo wa Nachingwea?
kuna mila na desturi za kitanzania hamna maadili ya kitanzania.
maadili ni ya Mungu tuu ambeye ndio muanzilishi wa maadili.
 
Kwa hiyo my pacha wa kuachina ziwa snowhite unaamini zamani kulikuwa na maadili ya Mtanzania?...ryte?...sasa yameenda wapi?....Na mlifundishwa wapi hayo maadili?...
lakini hili la maadili kuwa yapo au hayapo na kilichofanya maadili hayo yasiwepo kwa kweli ni mada pana sana! matokeo yake hata yale tulikuwa tunaamini ndiyo maadili ya kitanzania hayapo
 
Last edited by a moderator:
I got your point buddy...but i still ask the same thing..do we have morals and ethics that qualify to be branded as Tanzanian morals in its generality???...
The difference between ethics and morals can seem somewhat arbitrary to many, but there is a basic, albeit subtle, difference. Morals define personal character, while ethics stress a social system in which those morals are applied. In other words, ethics point to standards or codes of behavior expected by the group to which the individual belongs. This could be national ethics, social ethics, company ethics, professional ethics, or even family ethics. So while a person's moral code is usually unchanging, the ethics he or she practices can be other-dependent.


When considering the difference between ethics and morals, it may be helpful to consider a criminal defense lawyer. Though the lawyer's personal moral code likely finds murder immoral and reprehensible, ethics demand the accused client be defended as vigorously as possible, even when the lawyer knows the party is guilty and that a freed defendant would potentially lead to more crime. Legal ethics must override personal morals for the greater good of upholding a justice system in which the accused are given a fair trial and the prosecution must prove guilt beyond a reasonable doubt.
 
Ukilitazama neno MAADILI kwa kiingereza linatafsirika kama 'ethics' au 'morals'...kwa wenye kujua kiingereza vizuri mnaweza kunisaidia kueleza kinagaubaga nini maana ya morals or ethics.. na wale wajuzi wa kiswahili mtaniambia..Ila kwa tafsiri yangu yangu ya kichina..nadhani inamaanisha mambo ambayo kimsingi jamii imekubaliana kwa pamoja kwamba yakifanyika yanaleta mwonekano mwema kwenye jamii..na hii inaweza kuhusisha namna ya kuvaa, kusalimiana..kufarijiana misibani nakadhalika.................

Mada iliyoko mezani ni hii..Katika pita pita zangu za kimaisha hapa juzi kati nilibahatika kupanda daladala na ndani ya daladala kulikuwa na watu wa marika tofauti kuanzia wanafunzi na watu wazima wenye umri wa karibu miaka hamsini. Sasa basi mule ndani ya gari nilipaa na siti but kwa mbele yangu kulikuwa na watoto wa shule wawili wakike nadhani ni wa sekondari umri wa kati 15 na 16.walikuwa wamesimama huku wamebanwa na watu wazima...Sasa kwa kuwahurumia wale wadogo nikawaita na kuwaomba wakae kwenye siti yangu kwa kubebana..Of course kama nilivyosema kulikuwa na watu wazima wamesimama but my sense of humour fell on those poor small girls...

Sasa wakati mie nimesimama nikasikia siti za nyuma watu wakilalamika kuwa 'Maadili ya Mtanzania yameshuka kwamba nawezaje kuwaachia wanafunzi wakae ilhali kulikuwa na watu wazima wamesimama'..Niliupenda mjadala lakini kwa kuwa nilishukia jirani sikujua uliishaje..Baadaye nikiwa zangu njiani nikaanza kujiuliza maswali..Hivi ni kweli kuna kitu kama maadili ya Mtanzania?..na kama yapo hivi yanafundishwa wapi??..Binafsi kwa kuishi kwangu..mara nyingi katika kufanya maamuzi ya mambo yanayonikabili natumiaga busara ya dini yangu na ikizidi kabisa basi nitaconsult wazee wa kabila letu au zaidi nayatafakari tu kwa upeo wangu mwenyewe na kufanya maamuzi..lakini ever sijawahi kujua yapi ni maadili ya Mtanzania..kiasi kwamba naweza kusimama na kujitambulisha nayo...

Probably kama kuna mtu anayajua haya yanayoitwa..'Maadili ya Mtanzania'..hebu ajaribu kunielewesha basi!!..Manake kila kukicha tunalalamika watoto wa siku hizi hawana maadili..hivi ni kweli zamani yalikuwepo?? na ni kweli kwamba hayo ya zamani ndiyo yanamtambulisha Mtanzania??....lol!

Maadili ya Mtz ni Ufisadi.Tunapenda madili haoo.... hebu jifanye unataka kununua kitu alafu ndenda popote alafu anzakuuliza mtu yeyote utakayekutana nae wapi utanunua hicho kitu...nakwambia hamna mtu atakwambia hajui....hata kama unataka kununua ndege atakwambia anajua......
 
Back
Top Bottom