Hivi kuna aliyekutana na hii kitu shuleni au ni mimi tu?

Daaaaah darasa la nne nilipangwa dawati moja na binti nimpendaye suzana, kwenye mitihani nikawa nampiga tuff sana, nikaja kustukiwa na mwalimu moja kwasababu alinishinda marks 4, mwalimu massawe akaniambia wewe umeshindwa na mwenzako kwa sababu wewe unamsaidia lakini kuna hili swali moja wewe hulijui na yeye analijua na wala hukumuuliza.
Na huo ndio ukweli, Mimi sijawahi kumwomba yeye kunisaidia kwenye masomo.
Suzana popote ulipo arusha nakupa hi chalii yangu, wish tuonane tena siku moja.
 
Kuna kajamaa kalikuwa kanajifanya kamekufa kameoza kwa binti mmoja, basi siku moja akamwandikia barua ya mambo hayo hayo ya mahaba na kuiweka kwenye daftari kipindi hicho mm monitor wa standard vi. Hivyo wakati wa kukusanya nikaifuma ile Barua nikaenda kumuonesha madam Josephine...
Kama unavyojua walimu wa kike ambao hawajaolewa wanavyokuwa na kisirani.
Akaichukua na kusubiri muda wa assembly ya kwenda nyumbani akaniita niisome kwa sauti! Basi na mm bila ajizi nikaifanya kazi nzuri kama nilivyoagizwa na madam.

Nyie ndo mlikua mnapigwa siku tukiwa tunafunga shule sababu ya Unoko tu..Nauhakika utakua TISS Sasa hivi au sio?
 
Mimi nlikua shule ya msingi darasa la nne, dem naemuelewa yuko shule nyingine sekondari kidato cha kwanza.
Bas ilikua naamka asubuhi mapemaaa nawahi naenda kujismamisha jirani karibu na kwao ntasubili mpaka mwisho najua atatoka tu aende shule, akitoka tu macho yangu yote kwake ntamfuata kwa nyuma mpaka stand apande gari maana shule yake ni mbali gari likiondoka ndo narudi kwenda shule kila Siku nachelewa napigwa namba, lakini sikomi kila Siku ni vilevile.
nlikua siwezi hata kumuambia kitu maana mi katoto yeye mkubwa, sikumoja nmewahi kama kawaida nkaenda jirani na kwao nasubili atoke nimsindikize kwa miguu na kwa macho akanikuta nmesimama tu akaniambia "unashangaa nini wahi shule"
Siku iyo nlienda shule na furaha sana kumsikia akiniongelesha.
 
Kuna kajamaa kalikuwa kanajifanya kamekufa kameoza kwa binti mmoja, basi siku moja akamwandikia barua ya mambo hayo hayo ya mahaba na kuiweka kwenye daftari kipindi hicho mm monitor wa standard vi. Hivyo wakati wa kukusanya nikaifuma ile Barua nikaenda kumuonesha madam Josephine...
Kama unavyojua walimu wa kike ambao hawajaolewa wanavyokuwa na kisirani.
Akaichukua na kusubiri muda wa assembly ya kwenda nyumbani akaniita niisome kwa sauti! Basi na mm bila ajizi nikaifanya kazi nzuri kama nilivyoagizwa na madam.
Aisee ulichomesha kinoma
 
Dah

Nimekuja kuanza kupenda secondary

Shule ya msingi nisipo kuwa kwenye kamali,za penseli,stika(vikosi vya Nigeria na brazili) au kucheza mpira one touch basi tupo tumetoroka tunaiba migagi au tupo kwenye mianza tunatengeneza viposho na kutafuta risasi..mpk namaliza while msing sijawai Jua wanao penda wanapendea mini kwakweli..


Mimi shule nilikuwa naona rahaa kushinda trench huko tunaiba migagi nk

Aisee mkuu bilashaka utakuwa unatokea Mbeya maana iyo migagi ijawai kumuacha mwanafunzi salama
 
Kuna kajamaa kalikuwa kanajifanya kamekufa kameoza kwa binti mmoja, basi siku moja akamwandikia barua ya mambo hayo hayo ya mahaba na kuiweka kwenye daftari kipindi hicho mm monitor wa standard vi. Hivyo wakati wa kukusanya nikaifuma ile Barua nikaenda kumuonesha madam Josephine...
Kama unavyojua walimu wa kike ambao hawajaolewa wanavyokuwa na kisirani.
Akaichukua na kusubiri muda wa assembly ya kwenda nyumbani akaniita niisome kwa sauti! Basi na mm bila ajizi nikaifanya kazi nzuri kama nilivyoagizwa na madam.
Watu wa pigo ka zako darasan walikua vilaza sana
 
Kama hutaki na huamini basi Mkuu sikulazimishi ila Mimi ndiyo najijua kuwa ni Kapuku / Masikini na kama kuna ' Kitu ' ambacho nakiweza kama siyo Kukimudu ipasavyo ni kusema ukweli, kutokuwa mnafiki na kuona aibu kwa kusema ukweli wangu wa Kimaisha.

Pole sana ndugu yangu GENTA Mungu yupo nawe,mtegemee na ipo siku maisha yatakunyookea mpaka utasahau yote yanyuma,, Sio wewe tu, tuko wengi mno wenye mitihani kama yako.
 
Kama hutaki na huamini basi Mkuu sikulazimishi ila Mimi ndiyo najijua kuwa ni Kapuku / Masikini na kama kuna ' Kitu ' ambacho nakiweza kama siyo Kukimudu ipasavyo ni kusema ukweli, kutokuwa mnafiki na kuona aibu kwa kusema ukweli wangu wa Kimaisha.
Ni kweli mkuu inawezekana umekuwa mkweli kwamba huko vizuri kivile. Lakini kumbuka mara nyingi hizi "self ranging" huwa ni kutokana na matarajio ya mtu kutofikia pale alipotarajia kufika. Lakini wakati huo huo kuna watu wanaotamani wafike hapo ulipofika wewe. Hali hii huwa haina mwisho, ni hadi mtu anaondoka hapa duniani. Ni kama mashindano ya riadha, kila mmoja yuko kwenye position ambayo hapendi kuwa, hata yule anayeongoza mbio, haamini kama atamaliza akiwa wa kwanza. Kwa hiyo mkuu, tuendelee tu na haya maisha.
 
Mdada pekee ambae alikua Mpendwa wangu hata kumsogelea ni shida kutokana na majukumu ya Kitaifa na Protokali anayoambatana nayo. Last time tulikutana Dom akaishia kunitazama muda wooote wa Kikao. Mungu akusaidie Madam ktk majukum yako met
 
nikiwa primary, aliitwa Helena,mweupe na alivaa miwani..macho yake yalikuwa mekundu ya ruby Fulani..

wa secondary yeye aliitwa Farida,alikuwa mzuri natural; dizaini msomali.. Yeye Hakumaliza shule

Chuoni...aliitwa Saada,alikuwa na mnyonyo hataree mweupe pee..na alikuwa haubanii kuuonyesha kimtindo..

Hao wasipofika..masaa yalikuwa yanaongezeka.!
 
Back
Top Bottom