PostGE2025 Hivi internet ikizimwa tena siku za usoni, umejipangaje?

PostGE2025 Hivi internet ikizimwa tena siku za usoni, umejipangaje?

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections
Starlink ndio kila kitu, Lakini kwa jinsi inavyo fanya kazi sidhani kama wanaweza kukubaliana na kufika muafaka na serekali.
Starlink hawana kona na wala haihitajiki ofisi yao iwepo Tz ili ifanye kazi.
Kwa hili sidhani kama wana weza pewa ithibati.
Tunamsemaga mzungu vibaya ila hawa jamaa wapo mbali saana. Ile starlink ikija hapa mambo ni moto wa kuotea mbali.

Mateso ya voda, airtel n.k tutayasahau.
 
Ntaandika uzi mwingine kuhusu packages zao na cost zote. Napanga kuinstall kufikia January, so ntatoa uzoefu wangu mwenyewe. Ila internet ikifungwa bado wanakuwa hewani (kama ambavyo TV ziliendelea kufanya kazi wakati ambapo internet ilizimwa. Na media za kimataifa kama al-jazeera waliendelea kustream. Na pia kuna wabongo waliendelea kupata internet hata kupitia hizo zilizozimwa, maajabu).
Njoo ututoe tongotongo mkuu
 
Kwa

Kwa ufupi ukishalipia hiyo 70k, unaweza kutembea kwa mbps hadi 50. Ila kuna kadata limit, kwa sababu mitandao yote inaoperate kwenye falsafa ya FUP (Fair Usage Policy). Ukitumia beyond a given limit unaweza kupata degraded performance, pamoja na kwamba internet itaendelea kuwepo.
Mkuu kukuwekea hiyo net inacost kiasi gani?
 
Back
Top Bottom