commonmwananchi
JF-Expert Member
- Mar 12, 2011
- 3,377
- 1,952
kuna tatizo la mfumko wa bei sasa hivi nchini kote,tena kwa kiwango cha juu sana.kwa mwananchi wa kawaida kila kukicha ni aheri ya jana.tunalo bunge kubwa kuliko nchi za kenya,uganda,na hata rwanda na zambia ambao kitakwimu wanafanya vizuri kuliko sisi.
Humo ndani ya bunge tukisomewa majina tuna kila aina ya wasomi,ma-DK,PROF,ENG nk.sasa basi tultegemea kipindi hiki cha anguko la uchumi nchini.mbali na wao kukaa pale kugawana posho na kufukuzana uwaziri ili na wengine wakalie unono, lakini pia wale ambao ni wasomi wazuri na wachache. Nawashauri kama ifuatavyo ili watusaidie kupitia bunge letu ambalo linamermeta pale dodoma,wakati raia tumepauka huku site wafanye hili.
*Kuna fedha nyingi sana kwa sasa ambayo iko nje ya mzunguko wa mabenki yetu nchini kwa sasa,jambo ambalo linaifanya hata benki kuu ishindwe kudhibiti mzunguko wa fedha nchini.na hili ni jambo ambalo halihitaji ubishi kuliona na kulielewa
Sasa wakati hali ikiwa hivyo hawa wabunge wetu hakuna anayekuna kichwa ili walau kuja na hoja binafsi bungeni ili serikali ichukuwe hatua ya kudhibiti huu mzunguko usio rasmi kupitia kampuni za simu ambazo kwa sasa zimegeuka kufanya kazi za kibenki bila mfumo rasmi wa udhibiti ili kuhakikisha wanailipa serikali kodi stahiki na kuliongezea taifa kipato kwa faida ya wananchi pia.
Ni ukweli usiopingika kuwa huduma hizi zimetusaidia sana wananchi wa tanzania ukizingatia kwamba mabenki yetu yamejaa ukiritimba uliokithiri katika utoaji huduma zake na kugeuka kuwa kero kwa wananchi hasa pale unapokuwa na shida muhimu na za haraka kwa watu wa vijijini hii imekuwa kama mkombozi wetu namba moja.
Lakini nikiwa nimezingatia hilo basi ni vema sasa serikali ingeanza rasmi kama si kufungua kitengo rasmi pale TRA ambacho kitashughulika na hizi kampuni za simu nchini ili kuhakikisha kila promoshheni ambayo inahusika na ukusanyaji pesa kama bahati nasibu za kushindania magari,internet packages na zinginezo zinalipiwa kodi husika ili kuongeza wigo wa kodi nchini na tusikae kulilia nadini tu wakati na hii nayo inazidi madini kwa sababu ni mzunguko wa ndani na ni rahisi kuudhibiti,
Nina uhakika kuna matokeo chanya yatakayotokea na tusikae tu bungeni kusema michakato inaendelea.....nk,
Humo ndani ya bunge tukisomewa majina tuna kila aina ya wasomi,ma-DK,PROF,ENG nk.sasa basi tultegemea kipindi hiki cha anguko la uchumi nchini.mbali na wao kukaa pale kugawana posho na kufukuzana uwaziri ili na wengine wakalie unono, lakini pia wale ambao ni wasomi wazuri na wachache. Nawashauri kama ifuatavyo ili watusaidie kupitia bunge letu ambalo linamermeta pale dodoma,wakati raia tumepauka huku site wafanye hili.
*Kuna fedha nyingi sana kwa sasa ambayo iko nje ya mzunguko wa mabenki yetu nchini kwa sasa,jambo ambalo linaifanya hata benki kuu ishindwe kudhibiti mzunguko wa fedha nchini.na hili ni jambo ambalo halihitaji ubishi kuliona na kulielewa
Sasa wakati hali ikiwa hivyo hawa wabunge wetu hakuna anayekuna kichwa ili walau kuja na hoja binafsi bungeni ili serikali ichukuwe hatua ya kudhibiti huu mzunguko usio rasmi kupitia kampuni za simu ambazo kwa sasa zimegeuka kufanya kazi za kibenki bila mfumo rasmi wa udhibiti ili kuhakikisha wanailipa serikali kodi stahiki na kuliongezea taifa kipato kwa faida ya wananchi pia.
Ni ukweli usiopingika kuwa huduma hizi zimetusaidia sana wananchi wa tanzania ukizingatia kwamba mabenki yetu yamejaa ukiritimba uliokithiri katika utoaji huduma zake na kugeuka kuwa kero kwa wananchi hasa pale unapokuwa na shida muhimu na za haraka kwa watu wa vijijini hii imekuwa kama mkombozi wetu namba moja.
Lakini nikiwa nimezingatia hilo basi ni vema sasa serikali ingeanza rasmi kama si kufungua kitengo rasmi pale TRA ambacho kitashughulika na hizi kampuni za simu nchini ili kuhakikisha kila promoshheni ambayo inahusika na ukusanyaji pesa kama bahati nasibu za kushindania magari,internet packages na zinginezo zinalipiwa kodi husika ili kuongeza wigo wa kodi nchini na tusikae kulilia nadini tu wakati na hii nayo inazidi madini kwa sababu ni mzunguko wa ndani na ni rahisi kuudhibiti,
Nina uhakika kuna matokeo chanya yatakayotokea na tusikae tu bungeni kusema michakato inaendelea.....nk,