Hivi hiki wanachotufanyia Muhimbili Hospital ni haki kweli?

ELIAS MICHAEL MORRIS

JF-Expert Member
Sep 26, 2016
385
298
Habari zenu wanajamvi,

Kuna ndg yangu mmoja (RIP) alipata ajali ya pikipiki mwezi June mwaka jana, aliumia sana kichwani, akapelekwa muhimbil akatibiwa na akaruhusiwa (mwaka jana huo huo) na akashauriwa asitumie vilevi na hata kukaa kwenye vurugu vurugu.

Alikua anafanya shughuli zake kama kawaida ila wiki iliyopita tarehe 5 akazidiwa na tukampeleka Muhimbili tena. Alipofika kule hali ikazid kuwa mbaya tukaambiwa inatakiwa afanyiwe scan. Tukalipia na akafanyiwa, majibu yakaonyesha kuwa ubongo wake umevimba sababu ya ile ajali hivyo mwili hauna mawasiliano kabisa na ubongo na hakuna njia ya kutatua hilo (na kipind hiko alkuwa haongei wala hajitikisi).

Akapelekwa ICU na akawekewa mashine ya kumsaidia kupumua hadi siku Mungu atakayoamua kumchukua. Majuzi tarehe 11 akafariki, sasa tatizo limekuja baada ya kufariki.

Juzi tumeenda muhimbili kufatilia taratibu ya maiti wanatuambia maiti inadaiwa tsh mil 1.5. Sasa sisi tunajiuliza iyo milioni 1 na laki 5 inatoka wapi wakati scan na vipimo vingine vyote tulilipia. Kuna vidawa kidogo navyo tulilipia. Je kulala ICU pekee na ile mashine ya Oxygen pekee kwa siku 5 ndo mil 1.5? Maana huko ICU hakuwekewa hata dripu au dawa yeyote zaid ya hiyo oxygen pekee.

Hadi sasa maiti bado haijachukuliwa sababu ya ukubwa wa hizo gharama. Je wanajamvi wenzangu hii ni sawa? Je muhimbili imebinafsiswa?,

Asanteni na nawasilisha.
 
Ni shida sasa hvi bora uende private hospital kuliko hizo za serikali kwenye issue ya gharama.
 
Pole sana kaka, yaani hata mimi hospitali za serikali sina hamu nazo kabisa wanapenda pesa na hata ukiwapa pesa hawana matibabu mazuri
 
Pole mkuuu, uone uongozi wajuu au kama vipi ofisi ya waziri anayehusika maaana siku hizi hawa watu walishazoea yaaani mpaka hapo atumbuliwe mtu
 
Pole mkuuu, uone uongozi wajuu au kama vipi ofisi ya waziri anayehusika maaana siku hizi hawa watu walishazoea yaaani mpaka hapo atumbuliwe mtu
asante, nahisi hata huo uongozi wa juu w hospital wanayajua haya maan naskia hii si mala y kwanza ndomana nahisi labda hosptal ishabnafsishwa ila wanatumia tu jina la hospital y taifa wakat y watu bnafsi maana mbon hawafany mambo yao kiutaifa?
 
Alilala Wodini kwa muda gani ?

- Alitunzwa Mortuary kwa muda gani ?

- Na kama alipokuwa mzima alipewa chakula hapo MNH ?

- Alikuwa na referral au mli - mrefer ninyi wenyewe from home to MNH ( Kumbuka MNH ni referral hospital, kama huna huna barua au forms za referral basi unakuwa treated kama Private Mgonjwa !

N.B Ndugu zangu bima ya afya ni muhimu sana kuliko watanzania wengi wanavyodhani.
 
Pole sana kaka, yaani hata mimi hospitali za serikali sina hamu nazo kabisa wanapenda pesa na hata ukiwapa pesa hawana matibabu mazuri
si kweli Serikal imeboresha sana matibabu na hospital zake saizi matibabu yapo vizuri sana sana
 
Alilala Wodini kwa muda gani ?

- Alitunzwa Mortuary kwa muda gani ?

- Na kama alipokuwa mzima alipewa chakula hapo MNH ?

- Alikuwa na referral au mli - mrefer ninyi wenyewe from home to MNH ( Kumbuka MNH ni referral hospital, kama huna huna barua au forms za referral basi unakuwa treated kama Private Mgonjwa !

N.B Ndugu zangu bima ya afya ni muhimu sana kuliko watanzania wengi wanavyodhani.
Tunashukuru kwa ufafanuzi mzuri kiongozi,, PIA Serikali IMELETA MADAWA PALE MUHIMBILI, na Kuna MADAKTARI wengine wameongezwa
 
Personally sijui ila naomba tu nikupe pole kwa msiba wa ndugu yako.Mungu amrehemu.
 
asante, nahisi hata huo uongozi wa juu w hospital wanayajua haya maan naskia hii si mala y kwanza ndomana nahisi labda hosptal ishabnafsishwa ila wanatumia tu jina la hospital y taifa wakat y watu bnafsi maana mbon hawafany mambo yao kiutaifa?
Huo ni UZUSHI MNH HAIJABINAFSISHWA watu waacha uzushi wao
 
Tunashukuru kwa ufafanuzi mzuri kiongozi,, PIA Serikali IMELETA MADAWA PALE MUHIMBILI, na Kuna MADAKTARI wengine wameongezwa
Ni kweli Muhimbili wako vizuri tu siku hizi, tatizo ni kwamba watu hawajajua ni kwa jinsi gani wanaweza kupunguza gharama za matibabu hapo MNH, Mtu anakuwa na mgonjwa wake nyumbani anamchukua moja kwa moja tu MNH ( Lazima gharama ziwe kubwa ) tofauti na mtu ambaye labda kaanzia Tumbi akashindikana akawa referred to MNH
 
asante, nahisi hata huo uongozi wa juu w hospital wanayajua haya maan naskia hii si mala y kwanza ndomana nahisi labda hosptal ishabnafsishwa ila wanatumia tu jina la hospital y taifa wakat y watu bnafsi maana mbon hawafany mambo yao kiutaifa?
Kaka pole kwa msiba.
Kwa siku alizokaa ICU hiyo gharama ni reasonable.
Kumbuka nchini kwetu matibabu tunagharamia wananchi angalau kwenye elimu ya msingi gharama ni free lakini sio kwenye sekta ya afya.

Pia kuna tofauti kama angepatiwa referral kutoka kituo cha afya au hospital ya wilaya gharama zingekuwa chini.

But tembeleeni kituo cha ustawi wa jamii pale Muhimbili ipo ofisi watawasaidia kuwaombea msahama kama hamna uwezo wa kuilipa.

poleni kwa msiba. Mwenyezi mungu awape subira.
 
Huo ni UZUSHI MNH HAIJABINAFSISHWA watu waacha uzushi wao
Kama haijabinafsishwa mbona wanagonga bei kiasi hiko,yaani watu wanahuzuni ndugu yao kufariki kabla hata hawajajipanga watamsitiri vipi ndugu yao wanaenda kuuliza taratibu za kuupata mwili wanapewa bill ya 1.5mill,sio kila mtu mwenye pesa wengine ni maskini ukiwaletea vitu kama hivi unazidi kuwavuruga bora hata angekuwa amepona lakini kafa.hii sio haki
 
Alilala Wodini kwa muda gani ?

- Alitunzwa Mortuary kwa muda gani ?

- Na kama alipokuwa mzima alipewa chakula hapo MNH ?

- Alikuwa na referral au mli - mrefer ninyi wenyewe from home to MNH ( Kumbuka MNH ni referral hospital, kama huna huna barua au forms za referral basi unakuwa treated kama Private Mgonjwa !

N.B Ndugu zangu bima ya afya ni muhimu sana kuliko watanzania wengi wanavyodhani.
kama nilivyoeleza hapo juu, alidondoka ghafla tar 5 (j pili) akakimbizwa hospital ya kata wakasema hawaiwezi kesi yake ikabidi akimbizwe amana hospital, nao wakaona kesi nzito wakamkimbiza haraka MUHIMBIL hospital na kipindi hiko chote hakua na faham wala hakuwa anajitingisha ila moyo ulikua bado unadunda, muhimbili wakamfanyia scan (ambayo tulilipia) na baada y majibu ndo wakatuambia hatoweza kupona ila inabidi awekewe oxygen machine ili kumsaidia kupumua adi siku atakayofariki, kuhusu chakula (kwanz alkua hatikisiki hata kdogo kwa cku zote hizo), kwakwel mi cjaona akipewa chakula ktk cku zote 6 tulizoenda kumtembelea labda cjui wakat tusipokuwepo, na amekaa hapo kw cku 6 (toka tar 5 mpk 11 alpofaliki) tar 12 ndo tulifata maiti tukaambiwa gharama hizo za ml 1.5 sasa ndo tnajiuliza kulazwa kw hzo cku 7 n cku 1 monchwar ndo mil 1.5??
 
Icu ni gharama..hapo mnh ni cheap kdg..ukienda agha khn icu si chini ya milion kwa siku..
 
Kaka pole kwa msiba.
Kwa siku alizokaa ICU hiyo gharama ni reasonable.
Kumbuka nchini kwetu matibabu tunagharamia wananchi angalau kwenye elimu ya msingi gharama ni free lakini sio kwenye sekta ya afya.

Pia kuna tofauti kama angepatiwa referral kutoka kituo cha afya au hospital ya wilaya gharama zingekuwa chini.

But tembeleeni kituo cha ustawi wa jamii pale Muhimbili ipo ofisi watawasaidia kuwaombea msahama kama hamna uwezo wa kuilipa.

poleni kwa msiba. Mwenyezi mungu awape subira.
sisi tulimpeleka amana hospital wao baada ya kushindwa wakampakia ktk ambulance mpska muhimbili so he referraled from Amana to Muhimbili
 
penda kuwa MZALENDO WA NCHI YAKO
inaelekea unatoka familia moja na Makondakta wewe sio bure. Wapi nilipoonesha ishara ya kuichukia nchi yangu.

Nikitibiwa private kodi serikalini haifiki?

Think out of the box.

Uzalendo sio kuwa masikini wa fikra.
 
Back
Top Bottom