Niliyoyagundua baada ya kuwatembelea wagonjwa Muhimbili

Mtetezi.com

JF-Expert Member
Oct 6, 2016
3,134
3,568
1. Kwa wagonjwa wasio na rufaa ni ghali zaidi ya mara 3 ya private hospital
2. Sio hospitali ya wanyonge tena bali ya wenye fedha
3. Wagonjwa huzuiwa kutoka hospitalini hapo kama wanadaiwa na kushikiliwa hata kwa zaidi ya miezi.
4. Bima za NHIF husaidia dawa na vipimo vidogo tu vikubwa havipo
5. Huduma za uzazi (mama na mtoto) ni ghali mno

Habari kamili
1. Kama utapata ajali ya ghafla au tatizo lolote la haraka eti hupaswi kwenda direct muhimbili unapaswa uanzie Temeke, Mwananyamala na Amana ili upewe rufaa!.

Swali ni je mmeziwezesha hizo hospitali kuwaokoa wagonjwa walio ktk hatari kubwa za kupoteza maisha?

Eti kwakuwa tu huna rufaa ulipie gharama za matibabu mara kumi ya mwenye rufaa?

Is this fair

2. Sio hospitali ya wanyonge tena bali matajiri!
Nimemkuta dada mmoja kajifungua pre mature (7month) gharama alizoletewa(bill) ni zaidi ya milioni 8 na wamezuia asitoke hadi alipe na hana uwezo huu ni mwezi wa pili wakemshikilia.

Sio mmoja tu wapo wengi mno juzi kuna mmoja kataka kujirusha ghorofani kwakuwa kashikiliwa na hospitali kwa kyshindwa kulipa milioni tano huku hana mume kazaa na mume wa tu tu ambaye naye hana uwezo
Kuna marehemu kibao maiti zao zimezuiwa kupewa wasizikwe kwakuwa zinadaiwa gharama za matibabu.

3. Bima za Afya esp NHIF haina msaada wowote kwa mtanzania wa hali ya chini kwakuwa kifurushi chao hain vipimo vikubwa wala dawa za gharama.

Kuna kijana kaenda kupima ulcers kwa kushushwa mpira tumboni pale OGD_Ostra Genology Department, kile kipimo gharama yake ni sh 150,000/= pekee but hakipo kwenye bima.

Wanapatiwa dawa na vipimo ambavyo wanaweza kuvimudu wasivyoweza hawapatiwi na bima sasa umuhimu wake uko wapi

4. Ilani ya chama cha mapinduzi ya mwaka 2020/2025 inaeleza wazi kuwa huduma za mama mjamzito na mtoto bi bure kabisa but ukienda pale martenity block utawakuta zaidi ya wanawake zaidi ya 50 ambao wamezuiwa kutoka hospitalini kwakuwa hawajalipa bill za huduma hiyo ambayo utashangaa kusikia mtu kajifungua anadaiwa zaidi ya milioni kumi jamani tanzania hii hii ya watanzania wengi wanaoishi chini ya dola moja?

Mwisho kabisa kama una sadaka yako unatamani iwafikie walengwa nenda hospitali watu wana shida aisee

Wagonjwa wameshikiliwa zaidi ya miezi miwili kisa wanadaiwa

Serikali itoe tamko wagonjwa wote walioshikiliwa Muhimbili kisa wanadaiwa waachiwe huru mana wanavyozidi kukaa pale gharama zinaongezeka na serikali inazidi kuwahudumia na kuzidi kuzidi kuongeza gharama ambao hawawezi kulipa sasa mtu kakaa mwezi kisa anadaiwa bado mnamwandika accomadation fee kila siku mna akili kweli?

Hayo ni baadhi ya mengi niliyoyashuhudia Muhimbili sio siri yamenitoa machozi but wote hao hawana sauti wala connection nani awasemee kama sio mtetezi wao?
 
Yaani hospitali ya serikali inakuwa kama gereza kwa kushikilia watu!

Hapo kwenye bima nimekuelewa sana. Tulishakuwa na mgonjwa ambaye chuma kilikuwa kinamsumbua, baada ya kumpima wakasema hakina shida.

Cha kushangaza wakamwandikia dawa ambazo hata hapo hospitali eti hazipo, so tukaenda kununua.
 
Jamaa alimpeleka mtoto wa miezi 6 hospital baada ya matibabu bilo kuletwa jama hana uwezo wa kulipa itabidi wamzuiye , jamaa akawa anampelekea chakula mke wake ambae ndio yupo na mtoto, jamaa akawazaaa itabidi amwite nesi akamwambia ss tunaondoka tunawaachia mtoto ambae ndie alikuwa anaumwa na ndio anaedaiwa, nesi akaona hii kali itabidi aitwe daktari jamaa akatoa tena maelezo hayo hawakuwa na cha kufanya itabidi wamwache aende na mwanae,

Lakini kabla ya hapo ashaenda mpka ocf ya mkuu wa wilaya kueleza changamoto yake lkn akaambiwa mkuu ametoka amehangaika sanaaaa kupata suruhu alipoona imeshindikana akaamua afanye hivyo na akafanikiwa kutoka
 
Kwenye Bima nakubaliana na weww hasa bima NHIF haifai kabisa nimekata bima hiyo mwezi wa 4 kwa sh 987000/ mpaka leo hii nahangaika ukienda CCBRT wanakwambia nenda kapate rufaa nimeenda saifee hospital wamesema hawataki kuona.

Kuhusu muhimbili madaktari na wakurugenzi baada ya kuondoka jpm wao wanajiona mungu mtu hata ukienda hospitali ya Jakaya Kikwete ya moyo nayo shida utafikiri hospitali milki yao ajira zenyewe za kiundugu sana wakina moleli
 
kwenye Bima nakubaliana na weww hasa bima NHIF haifai kabisa nimekata bima hiyo mwezi wa 4 kwa sh 987000/ mpaka leo hii nahangaika ukienda ccbrt wanakwambia nenda kapate rufaa nimeenda saifee hospital wamesema hawataki kuona, kuhusu muhimbili madaktari na wakurugenzi baada ya kuondoka jpm wao wanajiona mungu mtu hata ukienda hospitali ya jakaya kikwete ya moyo nayo shida utafikiri hospitali milki yao ajira zenyewe za kiundugu sana wakina moleli
Mna dharau ajira mkadhani mna pesa sana.

Kaulize Mfagiaji wa ofsi analipwa Mshahara wa Laki Mbili lakini Ana Bima kupitia Ajira yake anatibiwa hospitali yoyote bila vikwazo.
 
4,Ilani ya chama cha mapinduzi ya mwaka 2020/2025 inaeleza wazi kuwa huduma za mama mjamzito na mtoto bi bure kabisa but ukienda pale martenity block utawakuta zaidi ya wanawake zaidi ya 50 ambao wamezuiwa kutoka hospitalini kwakuwa hawajalipa bill za huduma hiyo ambayo utashangaa kusikia mtu kajifungua anadaiwa zaidi ya milioni kumi jamani tanzania hii hii ya watanzania wengi wanaoishi chini ya dola moja?
CCM ni waongo na Walaghai wanawadanganya.

Sera ya Huduma kwa Mama na Watoto walivamia bila kujua mikakati yake.

Waliiba Sera ya Chadema. Hawakujua itatekelezwa vipi wao wakaingia kichwa kichwa
 
1,Kwa wagonjwa wasio na rufaa ni ghali zaidi ya mara 3 ya private hospital
2,Sio hospitali ya wanyonge tena bali ya wenye fedha
3,Wagonjwa huzuiwa kutoka hospitalini hapo kama wanadaiwa na kushikiliwa hata kwa zaidi ya miezi.
4,Bim
Nchi hii ina wapuuzi wengi sanaa, haswa humu jamiiforum 'na chadema,

Serikali Ilitaka kuleta bima ya afya kwa wote, wakajitia kukosoa
 
Jamaa alimpeleka mtoto wa miezi 6 hospital baada ya matibabu bilo kuletwa jama hana uwezo wa kulipa itabidi wamzuiye , jamaa akawa anampelekea chakula mke wake ambae ndio yupo na mtoto , jamaa akawazaaa itabidi amwite nesi akamwambia ss tunaondoka tunawaachia mtoto ambae ndie alikuwa anaumwa na ndio anaedaiwa, nesi akaona hii kali itabidi aitwe daktari jamaa akatoa tena maelezo hayo hawakuwa na cha kufanya itabidi wamwache aende na mwanae,


Lkn kabla ya hapo ashaenda mpka ocf ya mkuu wa wilaya kueleza changamoto yake lkn akaambiwa mkuu ametoka amehangaika sanaaaa kupata suruhu alipoona imeshindikana akaamua afanye hivyo na akafanikiwa kutoka
Tumelaaniwa,Mungu alifute hili taifa
 
Kwenye Bima nakubaliana na weww hasa bima NHIF haifai kabisa nimekata bima hiyo mwezi wa 4 kwa sh 987000/ mpaka leo hii nahangaika ukienda CCBRT wanakwambia nenda kapate rufaa nimeenda saifee hospital wamesema hawataki kuona.

Kuhusu muhimbili madaktari na wakurugenzi baada ya kuondoka jpm wao wanajiona mungu mtu hata ukienda hospitali ya jakaya kikwete ya moyo nayo shida utafikiri hospitali milki yao ajira zenyewe za kiundugu sana wakina moleli
Eh nikajifanya nataka kukata hii ya najali afya ya laki mbili sijui. So ya laki 9 tu kuna vitu hupati?

Hapana aisee
 
Back
Top Bottom