Mtetezi.com
JF-Expert Member
- Oct 6, 2016
- 3,134
- 3,568
1. Kwa wagonjwa wasio na rufaa ni ghali zaidi ya mara 3 ya private hospital
2. Sio hospitali ya wanyonge tena bali ya wenye fedha
3. Wagonjwa huzuiwa kutoka hospitalini hapo kama wanadaiwa na kushikiliwa hata kwa zaidi ya miezi.
4. Bima za NHIF husaidia dawa na vipimo vidogo tu vikubwa havipo
5. Huduma za uzazi (mama na mtoto) ni ghali mno
Habari kamili
1. Kama utapata ajali ya ghafla au tatizo lolote la haraka eti hupaswi kwenda direct muhimbili unapaswa uanzie Temeke, Mwananyamala na Amana ili upewe rufaa!.
Swali ni je mmeziwezesha hizo hospitali kuwaokoa wagonjwa walio ktk hatari kubwa za kupoteza maisha?
Eti kwakuwa tu huna rufaa ulipie gharama za matibabu mara kumi ya mwenye rufaa?
Is this fair
2. Sio hospitali ya wanyonge tena bali matajiri!
Nimemkuta dada mmoja kajifungua pre mature (7month) gharama alizoletewa(bill) ni zaidi ya milioni 8 na wamezuia asitoke hadi alipe na hana uwezo huu ni mwezi wa pili wakemshikilia.
Sio mmoja tu wapo wengi mno juzi kuna mmoja kataka kujirusha ghorofani kwakuwa kashikiliwa na hospitali kwa kyshindwa kulipa milioni tano huku hana mume kazaa na mume wa tu tu ambaye naye hana uwezo
Kuna marehemu kibao maiti zao zimezuiwa kupewa wasizikwe kwakuwa zinadaiwa gharama za matibabu.
3. Bima za Afya esp NHIF haina msaada wowote kwa mtanzania wa hali ya chini kwakuwa kifurushi chao hain vipimo vikubwa wala dawa za gharama.
Kuna kijana kaenda kupima ulcers kwa kushushwa mpira tumboni pale OGD_Ostra Genology Department, kile kipimo gharama yake ni sh 150,000/= pekee but hakipo kwenye bima.
Wanapatiwa dawa na vipimo ambavyo wanaweza kuvimudu wasivyoweza hawapatiwi na bima sasa umuhimu wake uko wapi
4. Ilani ya chama cha mapinduzi ya mwaka 2020/2025 inaeleza wazi kuwa huduma za mama mjamzito na mtoto bi bure kabisa but ukienda pale martenity block utawakuta zaidi ya wanawake zaidi ya 50 ambao wamezuiwa kutoka hospitalini kwakuwa hawajalipa bill za huduma hiyo ambayo utashangaa kusikia mtu kajifungua anadaiwa zaidi ya milioni kumi jamani tanzania hii hii ya watanzania wengi wanaoishi chini ya dola moja?
Mwisho kabisa kama una sadaka yako unatamani iwafikie walengwa nenda hospitali watu wana shida aisee
Wagonjwa wameshikiliwa zaidi ya miezi miwili kisa wanadaiwa
Serikali itoe tamko wagonjwa wote walioshikiliwa Muhimbili kisa wanadaiwa waachiwe huru mana wanavyozidi kukaa pale gharama zinaongezeka na serikali inazidi kuwahudumia na kuzidi kuzidi kuongeza gharama ambao hawawezi kulipa sasa mtu kakaa mwezi kisa anadaiwa bado mnamwandika accomadation fee kila siku mna akili kweli?
Hayo ni baadhi ya mengi niliyoyashuhudia Muhimbili sio siri yamenitoa machozi but wote hao hawana sauti wala connection nani awasemee kama sio mtetezi wao?
2. Sio hospitali ya wanyonge tena bali ya wenye fedha
3. Wagonjwa huzuiwa kutoka hospitalini hapo kama wanadaiwa na kushikiliwa hata kwa zaidi ya miezi.
4. Bima za NHIF husaidia dawa na vipimo vidogo tu vikubwa havipo
5. Huduma za uzazi (mama na mtoto) ni ghali mno
Habari kamili
1. Kama utapata ajali ya ghafla au tatizo lolote la haraka eti hupaswi kwenda direct muhimbili unapaswa uanzie Temeke, Mwananyamala na Amana ili upewe rufaa!.
Swali ni je mmeziwezesha hizo hospitali kuwaokoa wagonjwa walio ktk hatari kubwa za kupoteza maisha?
Eti kwakuwa tu huna rufaa ulipie gharama za matibabu mara kumi ya mwenye rufaa?
Is this fair
2. Sio hospitali ya wanyonge tena bali matajiri!
Nimemkuta dada mmoja kajifungua pre mature (7month) gharama alizoletewa(bill) ni zaidi ya milioni 8 na wamezuia asitoke hadi alipe na hana uwezo huu ni mwezi wa pili wakemshikilia.
Sio mmoja tu wapo wengi mno juzi kuna mmoja kataka kujirusha ghorofani kwakuwa kashikiliwa na hospitali kwa kyshindwa kulipa milioni tano huku hana mume kazaa na mume wa tu tu ambaye naye hana uwezo
Kuna marehemu kibao maiti zao zimezuiwa kupewa wasizikwe kwakuwa zinadaiwa gharama za matibabu.
3. Bima za Afya esp NHIF haina msaada wowote kwa mtanzania wa hali ya chini kwakuwa kifurushi chao hain vipimo vikubwa wala dawa za gharama.
Kuna kijana kaenda kupima ulcers kwa kushushwa mpira tumboni pale OGD_Ostra Genology Department, kile kipimo gharama yake ni sh 150,000/= pekee but hakipo kwenye bima.
Wanapatiwa dawa na vipimo ambavyo wanaweza kuvimudu wasivyoweza hawapatiwi na bima sasa umuhimu wake uko wapi
4. Ilani ya chama cha mapinduzi ya mwaka 2020/2025 inaeleza wazi kuwa huduma za mama mjamzito na mtoto bi bure kabisa but ukienda pale martenity block utawakuta zaidi ya wanawake zaidi ya 50 ambao wamezuiwa kutoka hospitalini kwakuwa hawajalipa bill za huduma hiyo ambayo utashangaa kusikia mtu kajifungua anadaiwa zaidi ya milioni kumi jamani tanzania hii hii ya watanzania wengi wanaoishi chini ya dola moja?
Mwisho kabisa kama una sadaka yako unatamani iwafikie walengwa nenda hospitali watu wana shida aisee
Wagonjwa wameshikiliwa zaidi ya miezi miwili kisa wanadaiwa
Serikali itoe tamko wagonjwa wote walioshikiliwa Muhimbili kisa wanadaiwa waachiwe huru mana wanavyozidi kukaa pale gharama zinaongezeka na serikali inazidi kuwahudumia na kuzidi kuzidi kuongeza gharama ambao hawawezi kulipa sasa mtu kakaa mwezi kisa anadaiwa bado mnamwandika accomadation fee kila siku mna akili kweli?
Hayo ni baadhi ya mengi niliyoyashuhudia Muhimbili sio siri yamenitoa machozi but wote hao hawana sauti wala connection nani awasemee kama sio mtetezi wao?