Hivi hii hali ni ya kawaida?

Hivi hii hali ni ya kawaida?

Wakuu, kuna hali inanitokea sana mpaka najikuta najishangaa 2,labda mimi mtu wa ajabu au vp.. Yani naweza fanya jambo alafu nastuka kwamba nilishafanya hivyo ila sikumbuki mda gani ila nakuwa na uhakika kabisa kwamba nilishafanya tena vile vile bila kukosea step..
Mfano naweza pita njia flani na kukutana na watu alafu hapo hapo picha inajirudia kichwani kwamba nilishapita hapo na kukutana na watu hao hao.. Hivi hii hali wakuu ni ya kawaida au kuna namna?
jitahidi kuwa unafuatlia ndoto zako, inawezekana kile unachoota usiku unakutana nacho baada ta siku 1 au mbili, ni hali ya kawaida wala usiogope, kuna watu wanaweza kuota kitu na kikatokea kweli.
 
Ipo mkuu,hata Mimi hivo hivo.
Yani unapokuwa unaendelea na jambo hilo inakuja hali inayokuonesha na kukupa taarifa kuwa umewahi kufanya kama lilivyo.


Hiyo ni kweli Mkuu,inanitokeaga sana..yaani kama photocopy vile..hasa nikiwa nimetulia,sina stress na yeyote

Mawazo yale ya kina
 
Wakuu, kuna hali inanitokea sana mpaka najikuta najishangaa 2,labda mimi mtu wa ajabu au vp.. Yani naweza fanya jambo alafu nastuka kwamba nilishafanya hivyo ila sikumbuki mda gani ila nakuwa na uhakika kabisa kwamba nilishafanya tena vile vile bila kukosea step..
Mfano naweza pita njia flani na kukutana na watu alafu hapo hapo picha inajirudia kichwani kwamba nilishapita hapo na kukutana na watu hao hao.. Hivi hii hali wakuu ni ya kawaida au kuna namna?
Very true hiyo hali ipo
 
cc: The Bold

Njoo huku ile kitu unatudadavuliaga kule chit chat kuna mkubwa fella anakuita uje kudadavua tena
 
ipo ila hutokea mara chache sanaaaaa, sasa km ww inajirudia rudia pengne Una uamsho
 
Wakuu, kuna hali inanitokea sana mpaka najikuta najishangaa 2,labda mimi mtu wa ajabu au vp.. Yani naweza fanya jambo alafu nastuka kwamba nilishafanya hivyo ila sikumbuki mda gani ila nakuwa na uhakika kabisa kwamba nilishafanya tena vile vile bila kukosea step..
Mfano naweza pita njia flani na kukutana na watu alafu hapo hapo picha inajirudia kichwani kwamba nilishapita hapo na kukutana na watu hao hao.. Hivi hii hali wakuu ni ya kawaida au kuna namna?
sasa si inajirudia wakati umekifanya kitu hicho,
hiyo hali inaitwa kumbukumbu.

Ingekuwa hiyo hali inatokea kabla hujafanya kitu ingekuwa sawa kujishangaa,
sasa wewe inakutokea baada ya kitendo,
hiyo ni kumbukumbu
 
Wakuu, kuna hali inanitokea sana mpaka najikuta najishangaa 2,labda mimi mtu wa ajabu au vp.. Yani naweza fanya jambo alafu nastuka kwamba nilishafanya hivyo ila sikumbuki mda gani ila nakuwa na uhakika kabisa kwamba nilishafanya tena vile vile bila kukosea step..
Mfano naweza pita njia flani na kukutana na watu alafu hapo hapo picha inajirudia kichwani kwamba nilishapita hapo na kukutana na watu hao hao.. Hivi hii hali wakuu ni ya kawaida au kuna namna?
sasa si inajirudia wakati umekifanya kitu hicho,
hiyo hali inaitwa kumbukumbu.

Ingekuwa hiyo hali inatokea kabla hujafanya kitu ingekuwa sawa kujishangaa,
sasa wewe inakutokea baada ya kitendo,
hiyo ni kumbukumbu
 
Hiyo hali inayokutokea inaelezeka

Inakuwa kama hivi

Umesafiri umeenda Arusha kwa mara ya kwanza unaingia kwenye chumba cha hoteli ukiangalia mazingira inaonekana kama unayafahamu ulishawahi kuwepo kwenye chumba hiki

Au wewe ni mwalimu umehamia kwenye shule mpya. Unaingia darasani unaandika somo utakalokuwa unafundisha halafu unageuka kuangalia wanafunzi wako. Lakini angali unaangalia unamwona mwanafunzi ambaye unahisi umeshawahi kumuona sehemu lakini hukumbuki ni wapi

Hapa kinachotokea ni kwamba brain yako ilikuwa na picha ya tukio hili punde tu ulipoingia darasani lakini kwasababu mwanzoni uliangalia kwa haraka na sasa unangalia kwa umakini zaidi basi brain yako inajaribu kukukumbusha ulichokiona mwanzo ulipokuwa huangalii wanafunzi kwa umakini hivyo huleta confusion unadhani ulishawahi kumwona huyo mwanafunzi

Wafaransa wanaita deja vu
 
Inaitwa "Déjà vu"
Inamaanisha kua kumbukumbu yako ipo nzima... Yaani kwa mda huo inafanya kazi fasta mpaka jambo lililotokea linaonekana kama ni kumbukumbu...
 
Inaitwa "Déjà vu"
Inamaanisha kua kumbukumbu yako ipo nzima... Yaani kwa mda huo inafanya kazi fasta mpaka jambo lililotokea linaonekana kama ni kumbukumbu...
Kama mimi yaani muda wote nakumbuka niko na Paprika kumbe wakati huo utakuta niko na Anah..![emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125]
 
Duuuh..., you just described me brother.., nilikuwa naogopa kuuliza watu wasije wakafikiri naanza kuchanhanyikiwa. Kuna mtu aliwahi kuniambia kwamba information inayoenda kuwa proceesed kwenye ubongo kuna wakati huwa inajigawa as a replica, moja inaruka circuit na kupita shortcut na hivyo kufika kabla ya replica nyingie (photocopy), hivyo ile ya pili ikifika ubongo unakumbuka kwamba ulishwahi kufanya kile kitu vile vile..! Na huwezi kumbuka ni mda gani, maana zinatofautiana mda mdogo sana, kama a trillionth of a second!
 
Kama mimi yaani muda wote nakumbuka niko na Paprika kumbe wakati huo utakuta niko na Anah..![emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125]
images-17.jpg
 
Kumbe tupo wengi!! Kiukweli hili jambo huwa nashindwa hata kuwahadithia watu kwani ni ngumu kueleweka!!

Huwa nahisi labda nilifanya/kuona tukio kwa roho kabla ya kutenda/kuona tena!!
 
Ukiangalia mental disorders kuna tatizo linalojuliana kama schizophrenia ambapo huwa tunagawanya symptoms zake katika makundi matatu;
1.Positive symptoms
-Delusions
-Hallucinations
-combativeness
-Insomnia
2.Negative symtoms
-Asocial behaviour
-Apathy
-Alogia
Anhedonia
-Affective flattening
3.Disorganised symptoms
-disoganised speech
-disorganised behaviour
-poor attention

Hallucinations ambayo ni moja kati ya positive symptoms za schizophrenia is a sensory experience of something that does not exist outside the mind....unaweza ukaona taswira, au ukasikia sauti au ukahisi harufu au hata ukahisi kuguswa na kitu lakini kiuhalisia hakuna taswira wala sauti wala harufu au wala hakuna kitu kilichokugusa.
Sisemi una schizophrenia mkuu ila nimeanzia mbali kidogo ili nifike hapo kwenye hallucinations ambapo naona kidogo kama panarelate na unachokiuliza, sio kila anaepata hallucinations ana schizophrenia,kupata kama mtu ana schizophrenia hutegemea kuangalia na symptoms nyingine na pia zinadumu kwa muda gani na zinamuathiri vipi mhusika katika social life na kikazi.
-
 
Back
Top Bottom