Hivi hii Biblia kuna manyang'au hawajabadilisha baadhi ya vipengele vya maandiko kwa faida yao kweli?

Jana Ulirudi Usiku

JF-Expert Member
Sep 9, 2021
2,362
2,261
Ninatafakari sana.
Pombe ni dhambi na kulewa ni dhambi, leo makanisa ya kiroho yanapiga vita unywaji wa pombe wakisema ni dhambi, wakitoa maandiko ya kukazia(bold) hili jambo. Ila wakati huo huo Yesu alikiri na kusema,

"Yohana hakula wala hakunywa, ila alikula nzige na asali, wakasema ana pepo huyu, ila mimi nakunywa nao wananiita mlevi, nakula, nao wananiita mlafi".

Maandiko hayo yanadhihirisha Yesu alikuwa akinywa mvinyo/divai/kilevi, sasa hii ya kusema kunywa pombe ni dhambi imetoka wapi? Nani muasisi wa hili? Tuwekeni wazi raia tupo njia panda.

Pia, agano la kale ni agano na Mungu na Waisrael pekee, bali agano jipya ni la Mungu na wanadamu wote watakaoliitia jina la Yesu na kuliamini. Sasa, hii inamaanisha walioamini agano jipya(jina la Yesu) hawafungwi tena na sheria za agano la kale ambalo limeipa nguvu torati(torah) na sheria zake.

Kama ndivyo, kwa nini basi bado makanisa yanadai zaka(fungu la 10) kwa waumini na kusema ni lazima? Je, ni wizi au hawajatambua kuwa agano la kale na sheria zake halitumiki tena baada ya ujio wa Yesu na kufufuka kwake katika wafu?

Kitabu cha Malachi ambacho ni cha mwisho kama sikosei kwenye agano la kale, kinawaambia WANA WA ISRA'IL kuwa wanamuibia BWANA kwa kutotoa fungu la kumi. Kimsingi walioamini agano jipya hawana nafasi katika agano kati ya Mungu na Wayahudi na vitabu vyake vyote ikiwemo sheria zake zote za torati. Je, watu waachwe au waendelee kulazimishwa na kutishiwa kutoa zaka kinguvu?

Naomba nieleweshwe kwenye haya tafadhalini.

Sent from my A50s using JamiiForums mobile app[/I]
 
Usitumie maandiko vibaya mpendwa!! Divai inatengenezwa na mizabibu!!huwezi kusema pombe ndo divai,ukisoma biblia nzima huwezi kukuta neno pombe ila divai utaipata!! Kabla haujapinga kuwa pombe ni dhambi unapaswa kujiuliza kwa Nini pombe ya leo isiitwe Basi divai? Unapaswa kujiuliza pia kwa Nini Kuna aina nyingi za pombe mpaka za kienyeji kila kabila? Kwa Nini nazo wasiziite divai pia? Umewahi kujiuliza kwa nini hizo pombe wanaruhusu watu wenye umri kuanzia miaka 18? Mbona soda na vinywaji hazina hayo masharti? Umewahi kujiuliza kwa nini pombe hazinyweki kanisani hata huko Romani,zina sehemu zao maalumu? Umewahi kujiuliza kwanini sehemu zote ambazo hizo pombe zinanyweka lazima utakutana na mambo yafuafayo, wavuta sigara, wanawake waliovaa nusu uchi nk!! Umewahi kujiuliza hivyi leo Yesu akija duniani mkatembea naye unafikiri anaweza kwenda bar kunywa hizo pombe? Mbona Mambo mengine hayahitaji elimu kubwa kuelewa sijui nyie huwa mnafeli wapi!!! Sasa haya ni maandiko yanayothibitisha kuwa ulevi ni dhambi na wote wanywa pombe wataenda motoni

1 Wakorintho 6:9
Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,

1 Wakorintho 6:10
wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi.

Luka 21:34
Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo;
 
Ahsante, nikutoe hofu tu kwamba sijayatumia vibaya maandiko ila nimeuliza maswali yangu kwa ku refer hayo maandiko.

Nikusahihishe kidogo;

"Umewahi kujiuliza kwa nini pombe hazinyweki kanisani hata huko Romani,zina sehemu zao maalumu????" hainyweki makanisani kwa sababu si sehemu yake, kanisani ni sehemu ya kumuabudu Mungu si kunywa pombe.

Shida ni kwamba hata kunywa nyumbani hiyo pombe au sehemu zake kama bar, pub nk, wanapinga kwa nguvu na kusema ni dhambi, si kweli kwa mujibu wa maandiko.
mlevi ni nani?.

Pia, suala ni kulewa pombe, mvinyo unalewesha, divai inalewesha, hizi zote tunaziweka kwa kundi moja na kuziita jina moja la 'pombe', pombe ni kitu kinacholewesha, yaani alcohol kwa kimombo.

Sasa je, kwa nini Yesu walimuita mlevi ingali alikuwa akinywa mvinyo/divai?

Pia, huna uhakika na umetumia hisia zaidi kusema kuwa, Yesu akirudi hatokwenda bar kunywa pombe, kwa sababu hajarudi bado.! Umejuaje kuwa hatokwenda bar, club nk?

Pia, kuonekana malaya, wavaa nusu uchi na waovu wengine mahali ambapo pombe inauzwa au inapatikana ni hoja muflisi. Kwa sababu huwezi kuiharamisha pombe kwa hoja hiyo na nyingine kama hizo. Vipi kama mtu akinunua huko na kwenda kunywea nyumbani kwake?!
 
Nikikazia hoja yako ni kwamba Muujiza wa kwanza kabisa wa Bwana Yesu ulikuwa ni kutengeneza pombe.--- hii ni kuonyesha umuhimu wa kunywa pombe kwa wafuasi wake.

Na ndio maana Wafuasi wake leo ndio wanaongoza duniani kunywa pombe.
 
Ahsante, nikutoe hofu tu kwamba sijayatumia vibaya maandiko ila nimeuliza maswali yangu kwa ku refer hayo maandiko.

Nikusahihishe kidogo;

"Umewahi kujiuliza kwa nini pombe hazinyweki kanisani hata huko Romani,zina sehemu zao maalumu????" hainyweki makanisani kwa sababu si sehemu yake, kanisani ni sehemu ya kumuabudu Mungu si kunywa pombe.

Shida ni kwamba hata kunywa nyumbani hiyo pombe au sehemu zake kama bar, pub nk, wanapinga kwa nguvu na kusema ni dhambi, si kweli kwa mujibu wa maandiko.
mlevi ni nani?.

Pia, suala ni kulewa pombe, mvinyo unalewesha, divai inalewesha, hizi zote tunaziweka kwa kundi moja na kuziita jina moja la 'pombe', pombe ni kitu kinacholewesha, yaani alcohol kwa kimombo.

Sasa je, kwa nini Yesu walimuita mlevi ingali alikuwa akinywa mvinyo/divai?

Pia, huna uhakika na umetumia hisia zaidi kusema kuwa, Yesu akirudi hatokwenda bar kunywa pombe, kwa sababu hajarudi bado.! Umejuaje kuwa hatokwenda bar, club nk?

Pia, kuonekana malaya, wavaa nusu uchi na waovu wengine mahali ambapo pombe inauzwa au inapatikana ni hoja muflisi. Kwa sababu huwezi kuiharamisha pombe kwa hoja hiyo na nyingine kama hizo. Vipi kama mtu akinunua huko na kwenda kunywea nyumbani kwake?!
Kama kanisani ni sehemu ya kumwabudu Mungu, kwa Nini vinywaji vingine Kama maji na juice vinatumika lakini sio pombe??? Nafikri unatumia maandiko vibaya, angalia impact ya unywaji pombe ndo maana haitakiwi mpendwa! Kusema kuwa Yesu walimwita Mlevi haimanishi kuwa alikuwa mlevi unatakiwa kuelewa, hata hananh mamake samwel, Eli kuhani alimwita mlevi lakini hakuwa mlevi, mitume wakati wa pentecoste waliiitwa walevi lakini kumbe hawakuwa walevi na hayo maandiko ndiyo haya

1 Samweli 1:13
Basi Hana alikuwa akinena moyoni mwake; midomo yake tu ilionekana kama anena, sauti yake isisikiwe; kwa hiyo huyo Eli alimdhania kuwa amelewa.

1 Samweli 1:14
Ndipo Eli akamwambia, Je! Utakuwa mlevi hata lini? Achilia mbali divai yako.

1 Samweli 1:15
Hana akajibu, akasema, Hasha! Bwana wangu, mimi ni mwanamke mwenye roho ya huzuni, mimi sikunywa divai wala kileo, ila nimeimimina roho yangu mbele za BWANA.
Matendo ya Mitume 2:12
Wakashangaa wote wakaingiwa na shaka, wakiambiana, Maana yake nini mambo haya?

Matendo ya Mitume 2:13
Wengine walidhihaki, wakisema, wamelewa kwa mvinyo mpya.

Matendo ya Mitume 2:14
Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu.

Matendo ya Mitume 2:15
Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana;

Kuitwa kuwa wewe ni mzinzi haimanishi kuwa wewe ni mzinzi mpendwa! Watu wanaweza kukutungia uongo pia! Hamna sehemu yoyote ambayo Yesu alikunywa divai!!

Usiendelee kutumia maandiko vibaya, kwa sababu ya tamaa za watu wamejihalalishia uovu lakini mwisho wake unapaswa kujua kuwa walevi hawataingia mbinguni, msidanganyike na makanisa hayo ya kichwara yanayohalalisha pombe, hayana mbingu ya kuwapeleka mpendwa, wanafundisha maagizo ya wanadamu yasiyo na uzima wowote wa Kimungu

Mathayo 15:8
Watu hawa huniheshimu kwa midomo; <br>Ila mioyo yao iko mbali nami.

Mathayo 15:9
Nao waniabudu bure, <br>Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu. Hata kama usiponiamini ndugu wewe endelea kuamini uongo!
2 Petro 2:13
Wakipatikana na madhara, ambayo ni ujira wa udhalimu wao, wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa; wamekuwa ni mawaa na aibu wakifuata anasa zisizo kiasi katika karamu zao za upendo, wafanyapo karamu pamoja nanyi;

2 Petro 2:14
wenye macho yajaayo uzinzi, watu wasiokoma kutenda dhambi, wenye kuhadaa roho zisizo imara, wenye mioyo iliyozoezwa kutamani, wana wa laana;

2 Petro 2:15
wakiiacha njia iliyonyoka, wakapotea, wakiifuata njia ya Balaamu, mwana wa Beori, aliyependa ujira wa udhalimu;

2 Petro 2:16
lakini alikaripiwa kwa uhalifu wake mwenyewe; punda, asiyeweza kusema, akinena kwa sauti ya kibinadamu, aliuzuia wazimu wa nabii yule.

2 Petro 2:17
Hawa ni visima visivyo na maji, na mawingu yachukuliwayo na tufani, ambao weusi wa giza ni akiba waliyowekewa.

2 Petro 2:18
Maana wakinena maneno makuu mno ya kiburi, kwa tamaa za mwili na kwa ufisadi huwahadaa watu walioanza kuwakimbia wale wanaoenenda katika udanganyifu;

2 Petro 2:19
wakiwaahidia uhuru, nao wenyewe ni watumwa wa uharibifu, maana mtu akishindwa na mtu huwa mtumwa wa mtu yule.

Pombe ni kitu kichafu haijalishi unakunywa ukiwa nyumbani au njiani, au nk ni machukizo kwa Mungu na unajipeleka mwenyewe motoni
 
Kama kanisani ni sehemu ya kumwabudu Mungu, kwa Nini vinywaji vingine Kama maji na juice vinatumika lakini sio pombe??? Nafikri unatumia maandiko vibaya, angalia impact ya unywaji pombe ndo maana haitakiwi mpendwa! Kusema kuwa Yesu walimwita Mlevi haimanishi kuwa alikuwa mlevi unatakiwa kuelewa, hata hananh mamake samwel, Eli kuhani alimwita mlevi lakini hakuwa mlevi, mitume wakati wa pentecoste waliiitwa walevi lakini kumbe hawakuwa walevi na hayo maandiko ndiyo haya

1 Samweli 1:13
Basi Hana alikuwa akinena moyoni mwake; midomo yake tu ilionekana kama anena, sauti yake isisikiwe; kwa hiyo huyo Eli alimdhania kuwa amelewa.

1 Samweli 1:14
Ndipo Eli akamwambia, Je! Utakuwa mlevi hata lini? Achilia mbali divai yako.

1 Samweli 1:15
Hana akajibu, akasema, Hasha! Bwana wangu, mimi ni mwanamke mwenye roho ya huzuni, mimi sikunywa divai wala kileo, ila nimeimimina roho yangu mbele za BWANA.
Matendo ya Mitume 2:12
Wakashangaa wote wakaingiwa na shaka, wakiambiana, Maana yake nini mambo haya?

Matendo ya Mitume 2:13
Wengine walidhihaki, wakisema, wamelewa kwa mvinyo mpya.

Matendo ya Mitume 2:14
Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu.

Matendo ya Mitume 2:15
Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana;

Kuitwa kuwa wewe ni mzinzi haimanishi kuwa wewe ni mzinzi mpendwa! Watu wanaweza kukutungia uongo pia! Hamna sehemu yoyote ambayo Yesu alikunywa divai!!

Usiendelee kutumia maandiko vibaya, kwa sababu ya tamaa za watu wamejihalalishia uovu lakini mwisho wake unapaswa kujua kuwa walevi hawataingia mbinguni, msidanganyike na makanisa hayo ya kichwara yanayohalalisha pombe, hayana mbingu ya kuwapeleka mpendwa, wanafundisha maagizo ya wanadamu yasiyo na uzima wowote wa Kimungu

Mathayo 15:8
Watu hawa huniheshimu kwa midomo;
Ila mioyo yao iko mbali nami.

Mathayo 15:9
Nao waniabudu bure,
Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu. Hata kama usiponiamini ndugu wewe endelea kuamini uongo!
2 Petro 2:13
Wakipatikana na madhara, ambayo ni ujira wa udhalimu wao, wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa; wamekuwa ni mawaa na aibu wakifuata anasa zisizo kiasi katika karamu zao za upendo, wafanyapo karamu pamoja nanyi;

2 Petro 2:14
wenye macho yajaayo uzinzi, watu wasiokoma kutenda dhambi, wenye kuhadaa roho zisizo imara, wenye mioyo iliyozoezwa kutamani, wana wa laana;

2 Petro 2:15
wakiiacha njia iliyonyoka, wakapotea, wakiifuata njia ya Balaamu, mwana wa Beori, aliyependa ujira wa udhalimu;

2 Petro 2:16
lakini alikaripiwa kwa uhalifu wake mwenyewe; punda, asiyeweza kusema, akinena kwa sauti ya kibinadamu, aliuzuia wazimu wa nabii yule.

2 Petro 2:17
Hawa ni visima visivyo na maji, na mawingu yachukuliwayo na tufani, ambao weusi wa giza ni akiba waliyowekewa.

2 Petro 2:18
Maana wakinena maneno makuu mno ya kiburi, kwa tamaa za mwili na kwa ufisadi huwahadaa watu walioanza kuwakimbia wale wanaoenenda katika udanganyifu;

2 Petro 2:19
wakiwaahidia uhuru, nao wenyewe ni watumwa wa uharibifu, maana mtu akishindwa na mtu huwa mtumwa wa mtu yule.

Pombe ni kitu kichafu haijalishi unakunywa ukiwa nyumbani au njiani, au nk ni machukizo kwa Mungu na unajipeleka mwenyewe motoni
Ahsante, japo vifungu ulivyoandika ni vingi vingine ni irrelevant na mada husika. Siyo mbaya!

"Kama kanisani ni sehemu ya kumwabudu Mungu, kwa Nini vinywaji vingine Kama maji na juice vinatumika lakini sio pombe??? Nafikri unatumia maandiko vibaya, angalia impact ya unywaji pombe ndo maana haitakiwi mpendwa!" kanisa gani unaongelea? Ni RC au Pentecoste? Nani kakudanganya hakuna pombe?
Pombe ni nini kwa tafsiri yako wewe? RC mapadri(baadhi) pombe tena zile chupa kubwa za mizinga wanatumia, bia wanatumia, nakumbuka nikiwa high school Ndanda, kwenye shule ya Mapadri pale kanisani zilikuwa zikitumika. Siyo kwa kificho na haikuwa haramu.

Ile divai itumikayo kanisani ni pombe/kilevi! Na ndiyo maana huwekwa maji kidogo na 'father' ili kupunguza ukali wake.

Hivyo basi, nakupinga unaposema pombe haiwekwi makanisani isipokuwa maji, juice n.k kwa mfano huo hapo juu kutoka RC.


Kwa upande wa makanisa ya kipentecoste, suala la kutokuwepo kwa pombe makanisani ila juice na maji, hili hata mwenyewe nataka kufahamu na ndiyo maana nikauliza kwa kuleta uzi huu.
Kwa sababu ikiwa Yesu anakiri kunywa na kula na kuitwa mlevi, iweje pombe izuiliwe makanisani? Hivi mnywaji wa juice anaweza kuitwa mlevi? Yesu alisema wazi wazi kuwa alikuwa akinywa ila hakuwa mlevi.

Kumbuka siyo wote wanywaji wa pombe ni walevi. "Luke 7 indicates that Jesus drank alcohol at times. While John the Baptist did not drink wine". Na ukumbuke wine/mvinyo ni pombe(alcoholic).

NB; nakusahihisha tena, sijatumia maandiko vibaya bali nimenukuu maandikoni, elewa tafadhali!
 
Back
Top Bottom