Tulimumu
JF-Expert Member
- Mar 11, 2013
- 14,325
- 13,038
Mimi sijawahi kufika Dubai na wala sijui kukoje. Lakini nimewasikia viongozi wakubwa wanasiasa katika ngazi ya urais mara kwa mara wakiahidi kuzijenga sehemu fulani za Tanzania kuwa kDubai. JK wakati wa kampeni zake wakati huo akigombea mara ya pili alisema ataibadili Tanga kuwa Dubai na pia nilimsikia akisema hata Kigoma ataifanya kuwa Dubai. Sijafika Tanga na Kigoma kuona jinsi zilivyokuwa sasa ni Dubai. Wenyeji wa huko wanaofurahi maisha ya Dubai sasa watatujuza raha wanazozipata.
Hivi karibuni nimemsikia pia rais wa jeecha naye akiahidi kuvifanya visiwa vile kuwa Dubai. Ninacho jiuliza ni kuwa hivi wanasiasa wa Tanzania wanaifahamu Dubai tu au na sehemu nyingine za Dunia? Hivi Dubai ni sehemu iliyoendelea sana kuliko sehemu nyingine duniani au ni rahisi sana kuijenga? Mbona sijawasikia wakisema wataifanya sehemu fulani ya Tanzania kuwa New Yorik, Woshngton, London, Paris, Tokyo au hata Pretoria Afrika ya Kusini au hata pengine Nairobi?! Mimi nawaomba watembelee na miji hiyo niliyoitaja ili angalau wasifanye nchi yote kuwa Dubai wajaribu kutofautisha ili sehemu nyingine ziwe Tokyo, Paris, London, nk
Hivi karibuni nimemsikia pia rais wa jeecha naye akiahidi kuvifanya visiwa vile kuwa Dubai. Ninacho jiuliza ni kuwa hivi wanasiasa wa Tanzania wanaifahamu Dubai tu au na sehemu nyingine za Dunia? Hivi Dubai ni sehemu iliyoendelea sana kuliko sehemu nyingine duniani au ni rahisi sana kuijenga? Mbona sijawasikia wakisema wataifanya sehemu fulani ya Tanzania kuwa New Yorik, Woshngton, London, Paris, Tokyo au hata Pretoria Afrika ya Kusini au hata pengine Nairobi?! Mimi nawaomba watembelee na miji hiyo niliyoitaja ili angalau wasifanye nchi yote kuwa Dubai wajaribu kutofautisha ili sehemu nyingine ziwe Tokyo, Paris, London, nk