Hivi Chato iko Geita au Kagera?

Hivi Chato iko Geita au Kagera?

amewakosea heshima wananchi wa kagera kwa kuwasimanga kwa maneno ya shombo
 
Mpango wako wa kukumbukwa kwenye teuzi vipi bado unao au ushakata tamaa?
 
Swali la msingi ni kuwa ;

kwa nini Chato ilihamishwa kutoka Kagera kuja Geita(mkoa mpya)?

Swali la nyongeza...ilikuwaje Baada ya Chato kupewa hadhi ya wilaya makao makuu hayakuwekwa Mganza na badala yake yakawa Chato?

swali dogo la nyongeza. kwa nini barabara ya Bwanga kwenda BIharamulo ilipindishwa badala ya kuweka lami kuelekea nyakanazi, ikapindishwa kupitia chato hadi Muganza?..je, biharamulo hawakustahili kupata barabara ya lami?

ntashukuru nikipata majibu ya maswali hayo.
Chato ndiyo nyumbani kwa mkuu wa kaya.
 
ameukimbiza kule kwa kua kuna ngono na katelelo lo!!!
 
Kumbe ndo maana kila siku anaenda kwao tu.
Hivi amerudi?
Chato hapo awali ilikuwa katika mkoa wa Kagera Wilaya ya Biharamulo na Magufuli alikuwa mbunge toka mkoa wa Kagera. Ikaenda Wilaya ya Biharamulo ikawa na majimbo mawili ya uchaguzi Biharamulo Magharibi na Chato baadae chato ikawa wilaya kamili (Busubi na Bugufi wana lugha na desturi sawa na Watusi, Wahutu na Waha). Wasukuma katika Wilaya ya Chato) Wakati huo. Wazinza and Warongo pia wanapatikana Biharamulo ya wakati huo

Kifupi soma link hii itakupanua macho:
http://www.tanzania.go.tz/egov_uploads/documents/MKOA_WA_KAGERA_sw.pdf
 
Unaumwa wivu kavae dela mkuu, wilaya kadhaa zimebadilika hujaongea ebu hoji kwanini busega ilikuwa magu mwanza na sasa ni simiyu? Kwanini hujahoji kulikoni bariadi ikawa makao makuu ya simiyu na isiendelee kuwa shiyanga? Bila shaka wewe ni mpiga majungu maarufu mtaani kwako.
 
Baada ya Geita kuwa mkoa ilihitaji wilaya za kujaziliza ili ukamilike kuwa mkoa, hivyo maeneo yaliyokuwa karibu yakasogezwa kuunda mkoa na Chato ikiwa mojawapo
 
Geita ilipokuwa mkoa wilaya ya chato ilijumuishwa kwenye huo mkoa wakati huo huo ili kurahisisha upatikanaji wa huduma mbali mbali mfano kijiografia ni rahisi sana mtu kusafiri kutoka chato kwenda mkoani (Geita ) kuliko kwenda Bukoba.
Mbona hujahoji ni kwanini wilaya ya Geita ilijitenga kutoka Mkoa wa Mwanza?
Haijitengi Geita ila ilihamishiwa tuu na mamlaka zilizopo
 
Chato iko geita baada ya geita kutengwa kutaka mwanza kuna mikoa ilipunguzwa ikiwa ni pamoja na kagera wakatoa chato Shinyanga wakatoa MBOGWE
 
Swali la msingi ni kuwa ;

kwa nini Chato ilihamishwa kutoka Kagera kuja Geita(mkoa mpya)?

Swali la nyongeza...ilikuwaje Baada ya Chato kupewa hadhi ya wilaya makao makuu hayakuwekwa Mganza na badala yake yakawa Chato?

swali dogo la nyongeza. kwa nini barabara ya Bwanga kwenda BIharamulo ilipindishwa badala ya kuweka lami kuelekea nyakanazi, ikapindishwa kupitia chato hadi Muganza?..je, biharamulo hawakustahili kupata barabara ya lami?

ntashukuru nikipata majibu ya maswali hayo.

Speculations. La muhumu tu ni kuwa je maamuzi hayo yalifanyika kwa mujibu wa sheria? Wakati mwingine sheria huwapendelea watu fulani kuliko wengine.
 
Ushamba huu, naomba kuuliza jamani:-

Hivi Rais anatokea MKOA WA Kagera au MKOA WA Geita? Kulingana na hotuba yake kagera majuzi.

Je, wilaya ya Chato iko MKOA WA Geita au MKOA WA Kagera? Wanajiografia nisaidieni?

Kwanini kuelekea Uchaguzi Mkuu WA 2015 wilaya ya Chato ilihamishwa kutoka Kagera na kupelekwa Geita? Je, ililenga kufata kabila au ni mpango mji?

Nchi hii sio ya ukabila lakini ilikuwaje hapa? Yaani Mimi ni mjinga kweli, hebu nifahamisheni.

Ni Mimi Mwana CCM mtapeliwa:

# Deogratius Kisandu.
Mkuu bado ile ndoto yako ya urais unayo ?
 
Back
Top Bottom