Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,175
- 48,459
Chama cha Mapinduzi kwa nyakati toauti kimekuwa kikivishambulia vyama vingine kwa hoja kwamba vyama hivyo vimejaa ukanda, udini na ukabila. Lakini huwa najiuliza maana ya ukanda na udini ni nini kwa Tafsiri ya CCM na wana CCM wenyewe. Mimi nakubaliana na tafsiri aliyowahi kuitoa Mwandishi nguli hapa nchini, Jenerali Ulimwengu kuhusu udini na ukabila.
Ulimwengu anasema kuwa udini ni ile hali ya kuwapima watu kwa kutazama dini zao na wala si wao kwanza kama binadamu. Kwa mfano kuna kazi inatolewa mahala fulani na wewe ndiye mtoa kazi, kuna watu wawili wana sifa zinazotofautiana. Wa dini yako ana sifa hafifu na wa dini nyingine ana zinazojitosheleza, lakini wewe unamuajiri wa dini yako kwa kuwa tu ni wa dini yako ingawa sifa zake hazitoshelezi, huo ndiyo udini na ukabila pia nao huko hivyo hivyo.
Lakini ukienda Pemba na Unguja ambako CUF ina wanachama wengi, asilimia kubwa ni waislam, hivyo haitarajiwi viongozi wengi wa CUF wawe wakristo, huo si udini bali ni matokeo ya Historia na ndiyo uhalisia. Kwa vyovyote vile hawa watu wa kutoka Zanzibar watakapokuwa Tanganyika wataahamiana sana na watu wanaokutuna nao kwenye misikiti kuliko wale wanaokwenda Kanisani, ushawishi wa CUF misikitini hautokani na udini bali unatokana na Historia ya chama chenyewe na uhalisia. Kuwa Mwanachama wa CUF si lazima uwe Muislamu wala Mpemba.
Tunayoifahamu kwa karibu Historia ya CHADEMA tunajua wakati wa kuanzishwa kwake na kabla hakijawa hivi kilivyo, wenye nguvu ndani ya CHADEMA walikuwa ni watu wa Kigoma wakiongozwa kina Alhaj Jaffary Kasisiko, Walid Kaborou na wengine wengi toka Shinyanga kama kina Mzee Philip Magadula Shelembi na Bob Nyanga Makani. Leo CHADEMA inapoitwa chama cha Wachaga eti kwa sababu tu mwenyekiti wake ni Mchaga huwa nashangaa sana!
Hivi CCM haina wanachama huko "Kaskazini"? Kati ya mawaziri Wakuu tisa tuliowahi kuwa nao kama taifa tena wakiwa wakati huo ni wana CCM wanne hawakutoka Kaskazini? Edward Sokoine, Edward Lowassa,Cleopa Msuya na Frederick Sumaye hawakuwa watu wa Kaskazini wakati wanapewa wadhifa huo. Huo ubaya wa watu wa Kaskazini huwa unaonekana wakati tu mtu anapokuwa nje ya CCM peke yake? Kinana ni mtu wa wapi kama siyo Kaskazini?
Kama watu wa dini moja kuwepo kwenye chama ndiyo chama hicho kuwa cha kidini, hivi wajumbe wengi Halmashauri Kuu na kamati Kuu ya CCM si waislam, hiyo peke yake inakifanya chama chao kuwa cha Kiislam? Uteuzi wa Magufuli umejaa watu wengi wa Kanda ya ziwa, hadi mbunge wa kutoka kwenye Jimbo analotoka la Chato, Jee Magufuli kachagua mawaziri na watu wengine kwa kufuata mambo ya Ukanda?
Kwa kufuata vigezo vya watu wa CCM wao kama chama hawana UKANDA na UKABILA na UDINI katka kuendesha siasa zao? Hivi yule mjinga aliyesema tena hata bila ya kukemewa na chama chake kwamba "Rais wa Tanzania hawezi toka Kaskazini" hakuwa anapalilia mambo ya ukanda?
Ulimwengu anasema kuwa udini ni ile hali ya kuwapima watu kwa kutazama dini zao na wala si wao kwanza kama binadamu. Kwa mfano kuna kazi inatolewa mahala fulani na wewe ndiye mtoa kazi, kuna watu wawili wana sifa zinazotofautiana. Wa dini yako ana sifa hafifu na wa dini nyingine ana zinazojitosheleza, lakini wewe unamuajiri wa dini yako kwa kuwa tu ni wa dini yako ingawa sifa zake hazitoshelezi, huo ndiyo udini na ukabila pia nao huko hivyo hivyo.
Lakini ukienda Pemba na Unguja ambako CUF ina wanachama wengi, asilimia kubwa ni waislam, hivyo haitarajiwi viongozi wengi wa CUF wawe wakristo, huo si udini bali ni matokeo ya Historia na ndiyo uhalisia. Kwa vyovyote vile hawa watu wa kutoka Zanzibar watakapokuwa Tanganyika wataahamiana sana na watu wanaokutuna nao kwenye misikiti kuliko wale wanaokwenda Kanisani, ushawishi wa CUF misikitini hautokani na udini bali unatokana na Historia ya chama chenyewe na uhalisia. Kuwa Mwanachama wa CUF si lazima uwe Muislamu wala Mpemba.
Tunayoifahamu kwa karibu Historia ya CHADEMA tunajua wakati wa kuanzishwa kwake na kabla hakijawa hivi kilivyo, wenye nguvu ndani ya CHADEMA walikuwa ni watu wa Kigoma wakiongozwa kina Alhaj Jaffary Kasisiko, Walid Kaborou na wengine wengi toka Shinyanga kama kina Mzee Philip Magadula Shelembi na Bob Nyanga Makani. Leo CHADEMA inapoitwa chama cha Wachaga eti kwa sababu tu mwenyekiti wake ni Mchaga huwa nashangaa sana!
Hivi CCM haina wanachama huko "Kaskazini"? Kati ya mawaziri Wakuu tisa tuliowahi kuwa nao kama taifa tena wakiwa wakati huo ni wana CCM wanne hawakutoka Kaskazini? Edward Sokoine, Edward Lowassa,Cleopa Msuya na Frederick Sumaye hawakuwa watu wa Kaskazini wakati wanapewa wadhifa huo. Huo ubaya wa watu wa Kaskazini huwa unaonekana wakati tu mtu anapokuwa nje ya CCM peke yake? Kinana ni mtu wa wapi kama siyo Kaskazini?
Kama watu wa dini moja kuwepo kwenye chama ndiyo chama hicho kuwa cha kidini, hivi wajumbe wengi Halmashauri Kuu na kamati Kuu ya CCM si waislam, hiyo peke yake inakifanya chama chao kuwa cha Kiislam? Uteuzi wa Magufuli umejaa watu wengi wa Kanda ya ziwa, hadi mbunge wa kutoka kwenye Jimbo analotoka la Chato, Jee Magufuli kachagua mawaziri na watu wengine kwa kufuata mambo ya Ukanda?
Kwa kufuata vigezo vya watu wa CCM wao kama chama hawana UKANDA na UKABILA na UDINI katka kuendesha siasa zao? Hivi yule mjinga aliyesema tena hata bila ya kukemewa na chama chake kwamba "Rais wa Tanzania hawezi toka Kaskazini" hakuwa anapalilia mambo ya ukanda?