barafuyamoto
JF-Expert Member
- Jul 26, 2014
- 32,323
- 29,584
Ilikuwa kama RIFARO. Wamekusanya chao na kusepa, hamna nguvu wala kupona magonjwa.Hii biashara ilivuma sana hasa ikihusisha na nguvu za kiume na watu walipiga hela sana kwa kuanzisha ufugaji wa kware na kuuza mayai yake lakini sasa naona kimyaa. Watu wakianza kuvumisha kitu hasa kukihusisha na nguvu za kiume kinapata soko sana. Akiibuka mtu leo na kusema mayai ya nyoka yanaongeza nguvu za kiume msako mkali utaanza kutafuta mayai ya nyoka popote mashimoni na mapangoni na ukitaka watu waanze kufuga nyoka tangaza kuwa mayai yake yanaleta nguvu za kiume