Binafsi nimekuwa nikishangazwa sana na baadhi ya watu wanaopiga kelele na kupinga pinga tu kwa kile kinachofanywa na Serikali hii ya sasa chini ya rais wetu amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama mh. Dk. JPM,
Hivi tulikuwa tunahitaji kiongozi wa aina gani tofauti na huyu rais tuliyenaye? Sipati jibu hasa kwa hawa watanzania wenzangu ninaowaona wakitokwa misuli ya shingo kubishia na kupinga kile kinachofanywa na rais wetu.
Zimekuwa zikitafutwa sababu za kipuuzi na zisizo na mashiko zenye mlengo wa kuchochea wananchi wapinge juhudi zinazofanywa na serikali lakini kwa umadhubuti wa Serikali na kutowajali wapiga kelele hao wamejikuta wako wenyewe na wananchi wamewapuuza na kuwaona ni wapiga domo tu, kama wanapinga kinachofanywa sasa hivi je walitaka kifanyweje na kwa ubora upi.
Juhudi za rais ziungwe mkono na kila raia wa Tanzania pasipo kujali chama, dini, ukanda ukabila, n.k . Tuungane kuijenga nchi kwa manufaa yetu na vizazi vijavyo. Tutaumia kwa sasa ila maumivu yakizidi ndivyo neema inakaribia.
.............. Wako katika kazi...........
Kalenga kidamali