Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Leo katika mtanange wa ligi kuu Tanzania bara VPL, ulikuwa ni mtifuano katika ya Azam FC na Yanga SC kwenye uwanja wa Chamazi, ambapo kwenye mchezo huu Yanga imeibuka na ushindi wa goli mbili kwa moja dhidi ya Azam FC.
Huku mchezaji wa Azam FC Abubakar Salum ' Sure Boy' akitolewa nje ya uwanja kwa kadi nyekundu baada ya kumsukuma beki wa Yanga Hassan Ramadhan.
Nakumbusha Azam FC na kuwauliza hivi Abubakar Salum huwa anawapa nini zaidi kugharimu timu?
Yaani viongozi mmeziba pamba kwenye masikio? Na macho mnayo lakini hamuoni? Sasa mnataka awaonyeshe namna gani kuwa huyo mchezaji ni Yanga wakutupwa, kwahivyo kuendelea kumtumia kwenye mechi dhidi ya Yanga ni ujinga.
Kwasababu tayari mnakuwa 10 uwanjani badala ya 11. Mchezaji anahujumu timu wazi wazi kiasi hicho halafu mnajifanya hamuoni?
Na wachezaji kama hawa ndo chanzo cha soka la Tanzania kupiga hatua. Poleni sana Azam FC.
Huku mchezaji wa Azam FC Abubakar Salum ' Sure Boy' akitolewa nje ya uwanja kwa kadi nyekundu baada ya kumsukuma beki wa Yanga Hassan Ramadhan.
Nakumbusha Azam FC na kuwauliza hivi Abubakar Salum huwa anawapa nini zaidi kugharimu timu?
Yaani viongozi mmeziba pamba kwenye masikio? Na macho mnayo lakini hamuoni? Sasa mnataka awaonyeshe namna gani kuwa huyo mchezaji ni Yanga wakutupwa, kwahivyo kuendelea kumtumia kwenye mechi dhidi ya Yanga ni ujinga.
Kwasababu tayari mnakuwa 10 uwanjani badala ya 11. Mchezaji anahujumu timu wazi wazi kiasi hicho halafu mnajifanya hamuoni?
Na wachezaji kama hawa ndo chanzo cha soka la Tanzania kupiga hatua. Poleni sana Azam FC.