Washawasha
JF-Expert Member
- Aug 7, 2006
- 16,652
- 13,077
Ahsante sana kwa historia
Nalog off
Nalog off
Watanzania bana. Akili ndogo sana. Kwa hiyo Mbeya ilitakiwa iwe wapi Zambia au Malawi? Ruvuma ilitakiwa iwe wapi? Bukoba,Kigoma, Mtwara, Mara,Tanga, Moshi na mikoa/wilaya nyingine zilizo mipakani? Kwa vile Wahangaza wanaongea lugha moja na utamaduni sawa na Warundi na Wanyarwanda sio sababu ya kuwa na fikira mbovu kama hizo. Afrika iligawanywa na Wakoloni kwa hiyo hapakuwa na sayansi iliyotumika kufanya mji Fulani uwe katika nchi Fulani au mto Fulani uwe katika nchi yako au ya jirani yako. Kumbuka Tanganyika,Rwanda na Burundi zilikuwa himaya ya Mjerumani kabla ya vita ya kwanza ya dunia kwa hiyo Wajerumani wasingeshindwa katika vita hatujui mipaka ya nchi 3 hizi ingekuwaje. Yamkini mkoa unapotoka wewe ungekuwa ndani ya nchi nyingine kama wakoloni wangeimega Tanganyika/TZ Bara tena. Muwe mnafikiria kwa kina kabla hamjaongea utumbo.all in all ngara ilitakiwa kuwa burundi au rwanda hata waangaza hawafananii na watanzania
Swali mujarabu majibu plzOk, asante kwa taarifa. Swali jingine rafiki yangu. Hivi Wahangaza, Warundi, Waha na Wanya Rwanda mbona Lugha ZAO zinafanana? Sasa mbona ni Makabila tofauti? Zamani walikuwa wa moja?
mkiowana mnafanana lugha?Mkuu kwa ufahamu wangu ni kwamba waha na warundi wameoana na kufanya mwingiliano wao uwe rahisi hata lugha zao kufanana.kwa mfano ukienda kakonko hasa kijiji kinaitwa Malenga unaweza kuvuka kwa mguu kwenda Burundi .hata soko huwa wanaingiliana.Kwa upande wa waha kufanana na wahangaza katika lugha zao ukweli ni kwamba kugha zao zinafanana sana na utofauti upo kwenye utamkaji kwani wahangaza hutamka neno kwa kuvuta lkn neno hilohilo waha hulitamka kwa kawaida ila maana huwa ileile.Pia wanafanana lugha kwasababu ya mwingiliano.
Punguza hasira hao watoto wa miaka ya 2000 hawazomi vitabuWatanzania bana. Akili ndogo sana. Kwa hiyo Mbeya ilitakiwa iwe wapi Zambia au Malawi? Ruvuma ilitakiwa iwe wapi? Bukoba,Kigoma, Mtwara, Mara,Tanga, Moshi na mikoa/wilaya nyingine zilizo mipakani? Kwa vile Wahangaza wanaongea lugha moja na utamaduni sawa na Warundi na Wanyarwanda sio sababu ya kuwa na fikira mbovu kama hizo. Afrika iligawanywa na Wakoloni kwa hiyo hapakuwa na sayansi iliyotumika kufanya mji Fulani uwe katika nchi Fulani au mto Fulani uwe katika nchi yako au ya jirani yako. Kumbuka Tanganyika,Rwanda na Burundi zilikuwa himaya ya Mjerumani kabla ya vita ya kwanza ya dunia kwa hiyo Wajerumani wasingeshindwa katika vita hatujui mipaka ya nchi 3 hizi ingekuwaje. Yamkini mkoa unapotoka wewe ungekuwa ndani ya nchi nyingine kama wakoloni wangeimega Tanganyika/TZ Bara tena. Muwe mnafikiria kwa kina kabla hamjaongea utumbo.
all in all ngara ilitakiwa kuwa burundi au rwanda hata waangaza hawafananii na watanzania
Kwa kuongezea tu ni kwamba Wafaransa hawajawahi kutawala Rwanda na Burundi. Baada ya vita kuu ya pili ya dunia Rwanda Urundi ilitwaliwa na wabeligiji ambao wanaongea kifaransa.Rudi kasome tena historia dogo, Rwanda, burundi na tanganyika ilikua nchi moja ikiitwa German Ostafrica...hao wabelgiji na wafaransa wamekuja kupewa tu baada ya mjerumani kushindwa ww1..Na waingereza wakapewa Tanganyika.
Duuh mkuu unanikumbusha enzi za rulenge secondary ( saint Alfred) R.I.P. OPOBOrwanda na burundi hazikuwa chini ya mjermani bali mbelgiji na mfaransa kwa nyakati tofauti,nimekaa ngara nimesomea rulenge secondary najua ninachomaanisha
Mkuu inasemekana wengi ya wanaojiita wahangaza ni warundi kuna ukweli wwote?
Daraja la R$usumo Mpakani mwa Tanzania na Rwanda
MAPOROMOKO ya Rusumo ni moja ya maporomoko yanayomvutia mgeni yeyote anayefika katika eneo la maporomoko hayo yaliyopo katika eneo la Rusumo wilaya ya Ngara mkoani Kagera.
Uwepo wa maporomoko hayo unatokana na mto Kagera au Ruvubu uliopo katika mpaka wa Tanzania na Rwanda na ni moja ya eneo ambalo ni kivutio kikubwa kwa wageni mbalimbali wanaofika katika ene hilo lililopo nje kidogo ya mji wa Ngara.
Maporomoko hayo huonekana kwa chini ukiwa juu ya daraja linalotengaisha nchi ya Tanzania na Rwanda na yamekuwa kivutio kikubwa kutokana na maji yake kuporomoka kwa kasi sana.
Ukiwa katika eneo hilo si rahisi sana kuona mpaka chini kutokana na mvuke wa maji wenye muonekano wa ukungu unaotokana na kasi ya maji yanayoporomoka kutoka mto Kagera upande wa Ngara.
Wageni wanaovuka mpaka huo wa Rusumo ni kawaida kukuta wakishangaa maporomoko hayo ya aina yake ambayo ni kivutio kikubwa cha kitalii.
Mbali ya maporomoko hayo kuwa maonyesho ya kuvuti ya kitalii,Kwa mjibu wa watafiti ni kuwa maporomoko hayo ambayo chanzo chake ni mto Kagera au Ruvubu yana uwezo wa kuzalisha megawati 90 za umeme.
Tangu mwaka 2013 serikali za Tanzania, Burundi na Rwanda zitiliana saini mkataba wa maridhiano ya pamoja katika kusimamia mradi mpya na mkubwa wa kuzalisha umeme kwenye maporomoko hayo ya maji katika Mto Kagera uliopo wilaya ya Ngara.
Mradi huo uliopo chini ya Uratibu wa Jumuiya ya nchi za Afrika Mashariki (EAC), umefadhiliwa na Benki ya Dunia (WB) kwa kiasi cha dora Milioni 340, na nchi hizo wananchama zinatarajia kunufaika na nishati hiyo ya umeme na kila nchi itapata mgao sawa wa nishati hiyo.
Ikumbukwe kuwa kabla ya malidhiano hayo, mradi huo uliwahi kuwa katika mipango ya kuendeleza umeme katika miaka ya 1980 hadi 1990, mipango hiyo iliingiliwa na kile kilichotajwa kuwa ni matumizi ya maji ya Mto Nile hivyo kukosa ufadhili na kisha baadae vita vya wenye kwa wenyewe katika nchi za Burundi na Rwanda zikadhorojesha jitihada hizo.
Imeandaliwa na Ng’oko Innocent
Umeelewa Viziri. Mto Ruvubu unatoka Burundi, Ukifika sehemu inaitwa Rusumo(Sasa hivi wanatengeneza Umeme wa Maji) unakutana na Mto Akagera unaotoka Rwanda. Kuanzia hapo Maji ya Ruvubu na Akagera vinapokutana hadi Ziwa Victoria, unaitwa Mto Kagera.
weweWatanzania bana. Akili ndogo sana. Kwa hiyo Mbeya ilitakiwa iwe wapi Zambia au Malawi? Ruvuma ilitakiwa iwe wapi? Bukoba,Kigoma, Mtwara, Mara,Tanga, Moshi na mikoa/wilaya nyingine zilizo mipakani? Kwa vile Wahangaza wanaongea lugha moja na utamaduni sawa na Warundi na Wanyarwanda sio sababu ya kuwa na fikira mbovu kama hizo. Afrika iligawanywa na Wakoloni kwa hiyo hapakuwa na sayansi iliyotumika kufanya mji Fulani uwe katika nchi Fulani au mto Fulani uwe katika nchi yako au ya jirani yako. Kumbuka Tanganyika,Rwanda na Burundi zilikuwa himaya ya Mjerumani kabla ya vita ya kwanza ya dunia kwa hiyo Wajerumani wasingeshindwa katika vita hatujui mipaka ya nchi 3 hizi ingekuwaje. Yamkini mkoa unapotoka wewe ungekuwa ndani ya nchi nyingine kama wakoloni wangeimega Tanganyika/TZ Bara tena. Muwe mnafikiria kwa kina kabla hamjaongea utumbo.