Kazi iliyokuja kuheshimika sana Tanzania na Zanzibar katika miaka ya 60 mwishoni na mwanzoni mwa miaka ya 70 ilikuwa Ubaharia. Baharia enzi hizo alikuwa mtu mwenye pesa za kigeni za kutosha, alivaa mavazi ya bei ghali na mavazi adimu yaliyokuwa yanalingana na wakati kwa kujilinganisha na Uingereza. Vijana wengi walitamani sana kuipata nafasi ya kuajiriwa kwenye meli yoyote inayotia nanga Dar es salaam na wakati mwingine pale Ferry-Posta ya zamani ilikuwa mahali maarumu ambapo vijana walikuwa wanavizia meli za kuzamia. Kila aliyekataa kwenda shule.... alijiita Baharia bwana!.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.