Mdharuba
JF-Expert Member
- Oct 26, 2011
- 824
- 521
STORY: Historia Batili(Fake History)
MTUNZI: Jumaa Khatib Mdharuba
+255 718 274 130
Season 01-Episode 02
★★★★★★★★★★★★★★
Kawaida bwana Khatib alikua akimuachia mkewe kila siku hela ya matumizi madogo madogo ya nyumbani sh elf 50, licha ya kuwa kulikua na kila kitu mle ndani, ila hela hizi Khatib alikusudia zinunuliwe vtu vidogo vidogo vya dharura. Na kila siku alikuwa akiziweka pesa katika droo ya meza ndogo ya pale chumbani..Ila leo asubuhi alimshuhudia akiziweka pesa nyingi kuliko alivyozoea.. ingawa haikumstua sana, ila kwa sasa ndo anapata picha nini kilifanyika!! Kwa hesabu za haraka haraka pesa ile ilikua ni ya matumizi ya siku 22!!
"Ina maana Khatib hatokuepo nyumbani kwa siku 22?" Ni swali lililozunguka kichwni mwa Sauda muda huo..
"Na kwa mara ya kwnza leo namshuhudia amefikisha saa 4 bdo yupo nyumbani, na alinambia hatoki!! baadae akaniaga tena kuwa anaenda kazini, imekuajee??" alizidi kupatwa na mawazo mazito bi Sauda.. alishapiga simu ofisini kwa mumewe tangu saa 2 ucku muda ambao ndo ofisi ilikua inafungwa na cm yake ilipokelewa na bwana Nira Saire na kumjibu kuwa boss hakufika kazini siku hiyo..na kua alishampgia simu na kumpa maelekezo muhimu na kumwambia pia kuwa kesho atampa maendleo yalikuaje.
Alibaki akijiuliza maswali mengi saaana..wazo kuu la wakati huu ni kuwa Khatib ameenda kulala na mwanamke mwingine leo!! Mwanamke yeyote lazima angewaza hivi kabla ya yote-wivu ndo mapenzi!! Lakini wazo hli lilijipinga lenyewe kichwani mwake, kwani Khatib hakuwahi kuonesha dalili yoyote ya kuchepuka kabla ya hapo..hata simu yake ilikua free sana kwa mkewe, muda wowote aliojisikia alishika na kufanya atakacho katika simu ile...
Akiwa katika dimbwi hili la mawazo ikiwa ni takriban saa 7 unusu za usiku, alipokea simu kutoka kwa Mama Mdharuba, "Vipi huyo mumeo bado hajarudi?"
"Ndio, hajarudi mama"
"Sasa, naomba nisikilize kwa makini sana mwanangu" Alianza kuongea Mama Mdharuba na kuweka kituo kumruhusu Sauda aitike kidogo..
"Ndio mama nakuckiliza, endelea tu" alijibu Sauda kwa sauti ya upole saaana..
"Khatib, ndo mwanangu wa kwanza baada ya yeye kuna mdogo wake hyu wa kike Hawa, wanangu ni hao wawili tu, na mimi Khatib namtegemea sana.. naomba nikutoe wasiwasi, kama kungekua kuna tatizo lolote linalomuhusu ningekua nimeshapata taarifa mwanangu, hata kama asingenipa yeye mwenyewe lakini mimi taarifa ningepata tu, kwhy ondoa wasiwasi mwanangu, mumeo atakua yu salama tu" Aliweka nukta kubwa Mama Mdharuba na kumfanya Sauda kushusha pumzi ndefu na kuitia kuwa amemuelewa..walitumia takribani dakika 10 kuongea, Mama Mdharuba akijitahidi kumliwaza Sauda alichukulie kuwa lile ni jambo la kawaida.
Na kwa kutumia utu uzima wake, Mama Mdharuba alifanikiwa kumshawishi Sauda alale kwa amani tu bila ya mumewe pembeni..licha ya kuwa ndio ilikua mara yake ya kwnza..
★★★★★★★★★★★★★
Mama Mdharuba, aliijua historia halisi ya mwanawe mpaka kufika hapo alipo, na hakuwa tayari kumwmbia mtu yeyote kuwa mwanae anatembelea HISTORIA BATILI katika ulimwengu huu.. Historia halisi ya maisha ya Khatib aliijua yeye na mwenyewe Khatib tu basi..
Kutokupatikana kwa Khatib hakumpi mawazo kabisaa mama hyu na sababu hiyo tabia alikua nayo kabla hajaoa wala hakusumbuka sana.. Khatib alishapitia kwake mchana na kumwachia hela ya matumizi inayoweza kutumika mwezi mzima, kwhyo alilijua hilo mapema kuwa Khatib hatokuwepo hapo kwa mda kidogo.. Kitu pekee na cha muhimu alichokua akikifanya Mama Mdharuba ni kumliwaza Sauda na kumfanya asijihisi mpweke sana, mpaka Sauda akaanza kupatwa na wasiwasi huenda hyu mama anajua nini mwanawe anafanya na ni kwamba tu anafichwa yeye Sauda..
"Mama, naomba kama unajua mume wangu alipo uniambie plzzz mama, ni wiki ya pili sasa mume wangu hajatokea na sina taarifa yake yoyote..na ww nakuona kama huna wasiwas mama".
Alihoji Sauda machozi yakimtoka akiwa nyumbani kwa mama mkwe wake maeneo ya Mbezi jijini Dar, Morogoro palikua hapakaliki, hakuwa na kampani ya aina yoyote, maana Khatib hakutaka kuwa na housegirl nyumbani kwake..sababu alizijua mwenyewe..ilikua ni siku ya 13 tangu Khatib aondoke pale nyumbani!! Sauda alikua ameanza kukonda tayari, tabasamu lililokua usoni mwake lote lilishapotea, hakuonekana kuyafurahia tena maisha yale ya ndoa, mume wake pekee aliyempenda na ndo mwanaume wake wa kwanza katika maisha yake ndo hyu asiyeeleweka..Alipata kila anachohitaji, lakini bdo amani haikuwepo moyoni mwake.. ukimuona lazima umlilie gere kwa maisha ya kifahari aliyokua anaishi..Lakini kumbe ni kama sumu tu iliyofichwa kwenye vikombe vya dhahabu!! Alikosa amani..
Ndoa yake ilikua na matatizo mengi sana ambayo hayakutaka pesa kuyamaliza..Tukio hili lilimfanya awaze mambo mengi saaanaa..
Kwanza, Khatib hakutaka wapate mtoto kipindi chote cha miaka miwili alichoishi naye, akidai bdo sana, walitakiwa wafurahie ndoa kwanza..
Pili, Khatib alikuwa na ratiba maalum ya kufanya mapenzi na mkewe kwa sababu alizozijua mwenyewe.. na kutokana na sababu ya kwanza, alikua akimkwepa sana mkewe katika siku zote za kipindi cha hatari..hivyo hata kama angetaka bi Sauda ratiba ilikua haibadiliki.
★★★★★★★★★★★★★★
"Haloo dada..mambo??" Aliongea Sarah mdogo wake Sauda ambaye wakati huo alikua akisoma Bachelor degree nchini Canada alikotafutiwa nafasi na shemeji yake Mr.Khatib!!
"Poa, mzima Sarah?" Aliongea bi Sauda lakini kwa sauti ya kinyonge sana..
"Nimemuona shem huku katika Supermarket moja hapa Vancouver" Aliongea Sarah kwa kujiamini akiwa hajui kinachoendlea..
"Wee usinambiee..umemuona huko Canada?"
"Ndio dada, yani mi niko kwenye basi naelekea chuo na yeye nimemuona anaingia Supermarket" Alizidi kusisitiza Sarah na kumfanya Sauda apagawe..
"Sasaa..sijui nisemeje jaman..Sarah..naomba ushuke katika hilo basi uende ukahakikishe kuwa ni yeye kweli!! Na uhakikishe kuwa anajua kuwa umemuona.." Aliongea Sauda akianza kupata matumaini akiwa na wasiwasi mkubwa..kitendo kilichofanya Mama Mdharuba aliyekuwa chumbani wakati huo atoke na kuja mlangoni kwake, na kuweza kuyafuatilia maongezi yale ya Sauda katika simu akajua Sauda anaongea na nani na anataka Sarah afanye nini..!!
"Kwani kuna tatizo lolote dada? Maana nawahi chuo nina presentation leo" Alihoji Sarah akianza kupata wasiwasi..
"Fanya kama nilivyokuagiza..maswali mengine utauliza baadae.."
"Sawa dada" Aliitikia Sarah na kushuka kituo cha mbele na kuanza kurudi kumfuatilia shemeji yake.
★★★★★★★★★★★★★★
Don't Miss Episode 03
MTUNZI: Jumaa Khatib Mdharuba
+255 718 274 130
Season 01-Episode 02
★★★★★★★★★★★★★★
Kawaida bwana Khatib alikua akimuachia mkewe kila siku hela ya matumizi madogo madogo ya nyumbani sh elf 50, licha ya kuwa kulikua na kila kitu mle ndani, ila hela hizi Khatib alikusudia zinunuliwe vtu vidogo vidogo vya dharura. Na kila siku alikuwa akiziweka pesa katika droo ya meza ndogo ya pale chumbani..Ila leo asubuhi alimshuhudia akiziweka pesa nyingi kuliko alivyozoea.. ingawa haikumstua sana, ila kwa sasa ndo anapata picha nini kilifanyika!! Kwa hesabu za haraka haraka pesa ile ilikua ni ya matumizi ya siku 22!!
"Ina maana Khatib hatokuepo nyumbani kwa siku 22?" Ni swali lililozunguka kichwni mwa Sauda muda huo..
"Na kwa mara ya kwnza leo namshuhudia amefikisha saa 4 bdo yupo nyumbani, na alinambia hatoki!! baadae akaniaga tena kuwa anaenda kazini, imekuajee??" alizidi kupatwa na mawazo mazito bi Sauda.. alishapiga simu ofisini kwa mumewe tangu saa 2 ucku muda ambao ndo ofisi ilikua inafungwa na cm yake ilipokelewa na bwana Nira Saire na kumjibu kuwa boss hakufika kazini siku hiyo..na kua alishampgia simu na kumpa maelekezo muhimu na kumwambia pia kuwa kesho atampa maendleo yalikuaje.
Alibaki akijiuliza maswali mengi saaana..wazo kuu la wakati huu ni kuwa Khatib ameenda kulala na mwanamke mwingine leo!! Mwanamke yeyote lazima angewaza hivi kabla ya yote-wivu ndo mapenzi!! Lakini wazo hli lilijipinga lenyewe kichwani mwake, kwani Khatib hakuwahi kuonesha dalili yoyote ya kuchepuka kabla ya hapo..hata simu yake ilikua free sana kwa mkewe, muda wowote aliojisikia alishika na kufanya atakacho katika simu ile...
Akiwa katika dimbwi hili la mawazo ikiwa ni takriban saa 7 unusu za usiku, alipokea simu kutoka kwa Mama Mdharuba, "Vipi huyo mumeo bado hajarudi?"
"Ndio, hajarudi mama"
"Sasa, naomba nisikilize kwa makini sana mwanangu" Alianza kuongea Mama Mdharuba na kuweka kituo kumruhusu Sauda aitike kidogo..
"Ndio mama nakuckiliza, endelea tu" alijibu Sauda kwa sauti ya upole saaana..
"Khatib, ndo mwanangu wa kwanza baada ya yeye kuna mdogo wake hyu wa kike Hawa, wanangu ni hao wawili tu, na mimi Khatib namtegemea sana.. naomba nikutoe wasiwasi, kama kungekua kuna tatizo lolote linalomuhusu ningekua nimeshapata taarifa mwanangu, hata kama asingenipa yeye mwenyewe lakini mimi taarifa ningepata tu, kwhy ondoa wasiwasi mwanangu, mumeo atakua yu salama tu" Aliweka nukta kubwa Mama Mdharuba na kumfanya Sauda kushusha pumzi ndefu na kuitia kuwa amemuelewa..walitumia takribani dakika 10 kuongea, Mama Mdharuba akijitahidi kumliwaza Sauda alichukulie kuwa lile ni jambo la kawaida.
Na kwa kutumia utu uzima wake, Mama Mdharuba alifanikiwa kumshawishi Sauda alale kwa amani tu bila ya mumewe pembeni..licha ya kuwa ndio ilikua mara yake ya kwnza..
★★★★★★★★★★★★★
Mama Mdharuba, aliijua historia halisi ya mwanawe mpaka kufika hapo alipo, na hakuwa tayari kumwmbia mtu yeyote kuwa mwanae anatembelea HISTORIA BATILI katika ulimwengu huu.. Historia halisi ya maisha ya Khatib aliijua yeye na mwenyewe Khatib tu basi..
Kutokupatikana kwa Khatib hakumpi mawazo kabisaa mama hyu na sababu hiyo tabia alikua nayo kabla hajaoa wala hakusumbuka sana.. Khatib alishapitia kwake mchana na kumwachia hela ya matumizi inayoweza kutumika mwezi mzima, kwhyo alilijua hilo mapema kuwa Khatib hatokuwepo hapo kwa mda kidogo.. Kitu pekee na cha muhimu alichokua akikifanya Mama Mdharuba ni kumliwaza Sauda na kumfanya asijihisi mpweke sana, mpaka Sauda akaanza kupatwa na wasiwasi huenda hyu mama anajua nini mwanawe anafanya na ni kwamba tu anafichwa yeye Sauda..
"Mama, naomba kama unajua mume wangu alipo uniambie plzzz mama, ni wiki ya pili sasa mume wangu hajatokea na sina taarifa yake yoyote..na ww nakuona kama huna wasiwas mama".
Alihoji Sauda machozi yakimtoka akiwa nyumbani kwa mama mkwe wake maeneo ya Mbezi jijini Dar, Morogoro palikua hapakaliki, hakuwa na kampani ya aina yoyote, maana Khatib hakutaka kuwa na housegirl nyumbani kwake..sababu alizijua mwenyewe..ilikua ni siku ya 13 tangu Khatib aondoke pale nyumbani!! Sauda alikua ameanza kukonda tayari, tabasamu lililokua usoni mwake lote lilishapotea, hakuonekana kuyafurahia tena maisha yale ya ndoa, mume wake pekee aliyempenda na ndo mwanaume wake wa kwanza katika maisha yake ndo hyu asiyeeleweka..Alipata kila anachohitaji, lakini bdo amani haikuwepo moyoni mwake.. ukimuona lazima umlilie gere kwa maisha ya kifahari aliyokua anaishi..Lakini kumbe ni kama sumu tu iliyofichwa kwenye vikombe vya dhahabu!! Alikosa amani..
Ndoa yake ilikua na matatizo mengi sana ambayo hayakutaka pesa kuyamaliza..Tukio hili lilimfanya awaze mambo mengi saaanaa..
Kwanza, Khatib hakutaka wapate mtoto kipindi chote cha miaka miwili alichoishi naye, akidai bdo sana, walitakiwa wafurahie ndoa kwanza..
Pili, Khatib alikuwa na ratiba maalum ya kufanya mapenzi na mkewe kwa sababu alizozijua mwenyewe.. na kutokana na sababu ya kwanza, alikua akimkwepa sana mkewe katika siku zote za kipindi cha hatari..hivyo hata kama angetaka bi Sauda ratiba ilikua haibadiliki.
★★★★★★★★★★★★★★
"Haloo dada..mambo??" Aliongea Sarah mdogo wake Sauda ambaye wakati huo alikua akisoma Bachelor degree nchini Canada alikotafutiwa nafasi na shemeji yake Mr.Khatib!!
"Poa, mzima Sarah?" Aliongea bi Sauda lakini kwa sauti ya kinyonge sana..
"Nimemuona shem huku katika Supermarket moja hapa Vancouver" Aliongea Sarah kwa kujiamini akiwa hajui kinachoendlea..
"Wee usinambiee..umemuona huko Canada?"
"Ndio dada, yani mi niko kwenye basi naelekea chuo na yeye nimemuona anaingia Supermarket" Alizidi kusisitiza Sarah na kumfanya Sauda apagawe..
"Sasaa..sijui nisemeje jaman..Sarah..naomba ushuke katika hilo basi uende ukahakikishe kuwa ni yeye kweli!! Na uhakikishe kuwa anajua kuwa umemuona.." Aliongea Sauda akianza kupata matumaini akiwa na wasiwasi mkubwa..kitendo kilichofanya Mama Mdharuba aliyekuwa chumbani wakati huo atoke na kuja mlangoni kwake, na kuweza kuyafuatilia maongezi yale ya Sauda katika simu akajua Sauda anaongea na nani na anataka Sarah afanye nini..!!
"Kwani kuna tatizo lolote dada? Maana nawahi chuo nina presentation leo" Alihoji Sarah akianza kupata wasiwasi..
"Fanya kama nilivyokuagiza..maswali mengine utauliza baadae.."
"Sawa dada" Aliitikia Sarah na kushuka kituo cha mbele na kuanza kurudi kumfuatilia shemeji yake.
★★★★★★★★★★★★★★
Don't Miss Episode 03