Che Kalizozele
JF-Expert Member
- Jul 20, 2008
- 777
- 49
Kutokana na ndoa ya baba kuwa na matatizo mengi,nilijikuta nikisoma vitabu vingi sana vinavyoongelea mahusiano.Vingi ya vitabu hivi vilikuwa vinaonesha kuwa tatizo kubwa katika mahusiano mengi hasa mapenzi ni kukosekana kwa mawasiliano baina ya wawili wapendanao.Baada ya kufanya uchunguzi usiokuwa rasmi nikagundua wanandoa wangi hawaongei hasa hisia zao.Si nikaingia katika ndoa,you can't believe Iam facing the same problem.Si kwamba hatuongei,tunajitahidi lakini sikumbuki tangu tumeoana siku ambayo tulikaa chini na kulijadili tendo la ndoa,ili labda tuliboreshe zaidi ingawa tuna tabia ya kuulizana kama tumefikishana kileleni kila baada ya kumaliza kupeana dozi.HIVI KUNA UGUMU GANI WA WANANDOA KUZIONGEA HISIA ZAO.