Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,162
- 48,433
Siku ya tarehe 6/ 8/1945 saa mbili za Asubuhi mji wa Hiroshima ulipigwa bomu la Atomiki na siku tatu baadaye yaani tarehe 9/08/1945 majira ya saa tano za Asubuhi mji wa Nagasaki nao ulipigwa Kwa bomu la Atomiki pia. Miji yote miwili ipo nchini Japan.
Miji hiyo miwili ilipigwa mabomu hayo ya Atomiki ili kuilazimisha Japan kusalimu amri na kutokuendelea na vita Kuu ya Pili ya Dunia.
Madhara ya kupigwa mabomu hayo yangaliko hata Sasa huko Hiroshima na Nagasaki!
Lakini baada ya kupigwa na mabomu hayo bado baada ya miaka kadhaa baadae, Japan iliibuka na kuwa miongoni mwa nchi tajiri duniani.
Kwa Sasa Japan inashikilia Hati fungani na dhamana za Serikali ya Marekani zenye thamani ya Dolla za kimarekani trioni 1.13 sawa na asilimia 13 (13%) ya deni lote la nje wanaodaiwa wamarekani.
Maelezo hayo nimeyatoa baada ya kuona CCM inatumia silaha zake zote kuhakikisha CHADEMA haiendelei kuwa chama imara cha siasa.
Haitokei kwa bahati mbaya kwenye nchi yenye vyama vya siasa zaidi ya 18 iwe tu ni watu wa CHADEMA wanatekwa, wanaouawa au wanapotezwa.
Lakini Sasa kinachoendelea kwa kesi dhidi ya CHADEMA na wanachadema zinazofunguliwa Kila siku, ni dalili kuwa CCM inataka CHADEMA isalimu amri.
Lakini niwaambie tu wana -CCM kuwa, baada ya kipindi cha kutumia silaha zao za maangamiz kupita, CHADEMA itasimama tena na kuwa imara zaidi.
Kama ilivyo kwa wakazi wa Hiroshima na Nagasaki ambao walijifunza kuishi na taathira zilizotokana na kushambuliwa na bomu la Atomiki, ndiyo CHADEMA itakavyoweza kuishi na matokeo ya kinachotokea Sasa.
Kilichowategemeza watu wa Hiroshima na Nagasaki, ilikuwa ujasiri, uvumilivu, tumaini na Imani kuwa mbele Kuna maisha bora zaidi kuliko kabla ya kushambuliwa.
Ninavowaona wanachadema wengi, bado wanaamini kuwa kesho ya chama chao ni bora zaidi kuliko Leo.
HAKUNA KIVULI KISICHO NA MWENYEWE!
Miji hiyo miwili ilipigwa mabomu hayo ya Atomiki ili kuilazimisha Japan kusalimu amri na kutokuendelea na vita Kuu ya Pili ya Dunia.
Madhara ya kupigwa mabomu hayo yangaliko hata Sasa huko Hiroshima na Nagasaki!
Lakini baada ya kupigwa na mabomu hayo bado baada ya miaka kadhaa baadae, Japan iliibuka na kuwa miongoni mwa nchi tajiri duniani.
Kwa Sasa Japan inashikilia Hati fungani na dhamana za Serikali ya Marekani zenye thamani ya Dolla za kimarekani trioni 1.13 sawa na asilimia 13 (13%) ya deni lote la nje wanaodaiwa wamarekani.
Maelezo hayo nimeyatoa baada ya kuona CCM inatumia silaha zake zote kuhakikisha CHADEMA haiendelei kuwa chama imara cha siasa.
Haitokei kwa bahati mbaya kwenye nchi yenye vyama vya siasa zaidi ya 18 iwe tu ni watu wa CHADEMA wanatekwa, wanaouawa au wanapotezwa.
Lakini Sasa kinachoendelea kwa kesi dhidi ya CHADEMA na wanachadema zinazofunguliwa Kila siku, ni dalili kuwa CCM inataka CHADEMA isalimu amri.
Lakini niwaambie tu wana -CCM kuwa, baada ya kipindi cha kutumia silaha zao za maangamiz kupita, CHADEMA itasimama tena na kuwa imara zaidi.
Kama ilivyo kwa wakazi wa Hiroshima na Nagasaki ambao walijifunza kuishi na taathira zilizotokana na kushambuliwa na bomu la Atomiki, ndiyo CHADEMA itakavyoweza kuishi na matokeo ya kinachotokea Sasa.
Kilichowategemeza watu wa Hiroshima na Nagasaki, ilikuwa ujasiri, uvumilivu, tumaini na Imani kuwa mbele Kuna maisha bora zaidi kuliko kabla ya kushambuliwa.
Ninavowaona wanachadema wengi, bado wanaamini kuwa kesho ya chama chao ni bora zaidi kuliko Leo.
HAKUNA KIVULI KISICHO NA MWENYEWE!