GadoTz
JF-Expert Member
- Nov 20, 2014
- 350
- 567
- Thread starter
- #61
Mkimaliza za marekani, tujadili na zetu wenyewe
Au ndio mke wa maskini, kuwadi mumewe
Nani anashika usukani, nani ni baridi
Kati ya Joh makini, na ngosha Fid
Ama mbishi na zaeed, sio tu 50 na did
Inapendeza mnapoeleza hip hop na miiko
Wapi na lini ilikuwa chimbuko,
Mtiririko wa list ya maandiko
Sio twist ni mziki wenye wenye mashiko
Noted...!!
Maybe nianze kwa kukutajia baadhi wasanii na makundi ya mwanzo ya Hiphop Bongo,...... Fresh XE, BBG, Adili Kumbuka, Salehe Jabir, KBC, Samia X, The BIG, Rymson, 2 proud (Sugu), makundi ni kama vile, Kwanza Unit, Deplowmatz, HardBlasterz, Gang Stars With Matatizo (GWM), Wagumu Weusi Asilia, Young Da Mob, Afro Reign, Jungle Crewz Pose, Bantu Pound, Hardcore unit kwa kutaja machache.
Nani alikuwa anafanya hiphop ya kweli na nani anabaki kusimama kama nembo ya kuutambulisha utamaduni wa hiphop bongo ilo kila mtu ana mtazamo wake.