Hili Tunda nimeli Miss sana jamni

Hili Tunda nimeli Miss sana jamni

Zambarau! dah.....nadhani kisutu sokoni zitkauwepo! nilikuwa nanunua hapo kipindi fulani...............

babe hizi zambarau zinanikumbusha mengi na huzuni.. zamani sana tulikuwa tunaenda kurasini na kuvuka kwenda upande wa kibada.. Siku yangu ya mwisho kwenda kuangua zambarau ni pale rafiki yangu wa utoto (wenyewe tulikuwa tunamuita Juma bondia) alipoanguka toka juu ya mzambarau.. urefu wa kama mita 20 hivi.. Sintoisahau hiyo siku.. nakumbuka alipofika chini akili zetu za kitoto zilitutuma kukimbia na kila mtoto alirudi kwao kimya.. Nakumbuka ilipokuja kugundulika nilikula kibano cha haja toka dingi.. Mshkaji wangu alifia hospital baada ya kufikishwa na wavuvi waliokuwa maeneo ya karibu..

RIP Juma Bondia..
 
babu toka lini ukawa mtaaluma..? niko busy ninachukua mafunzo.. ntaifanya menyewe.. sawa babu Asprin..?
sosoliso babu ODM huyu aliweka kambi maternity ward, naona sasa amehamia wa wavuta misuba!!!
nina wasiwasi na utaalamu wake akitoka huko kwa waathirika wa misuba si hata yeye atakuwa ameathirika!



babe hizi zambarau zinanikumbusha mengi na huzuni.. zamani sana tulikuwa tunaenda kurasini na kuvuka kwenda upande wa kibada.. Siku yangu ya mwisho kwenda kuangua zambarau ni pale rafiki yangu wa utoto (wenyewe tulikuwa tunamuita Juma bondia) alipoanguka toka juu ya mzambarau.. urefu wa kama mita 20 hivi.. Sintoisahau hiyo siku.. nakumbuka alipofika chini akili zetu za kitoto zilitutuma kukimbia na kila mtoto alirudi kwao kimya.. Nakumbuka ilipokuja kugundulika nilikula kibano cha haja toka dingi.. Mshkaji wangu alifia hospital baada ya kufikishwa na wavuvi waliokuwa maeneo ya karibu..

RIP Juma Bondia..

oooh sad story! pole sana mwayego sosoliso wangu!!
 
Last edited by a moderator:
Kwa kudhungu sijui kwani ndio hivyo tena maimuna mie
Dalili zake ni vidonda vingi kwenye miguu kwa watoto wadogo vinaambatana na homa za vipindi sijui kama umenielewa au bado unataka ufafanuzi zaidi
Wandugu Masanja hebu tufafanulie huu ndo ugonjwa gani, dalili zake je? Labda ukilitaja kwa kidhungu ndo tutalielewa!
 
Huu uzi umenikumbusha mbali sana,nilipoanza kupitia comments za wadau nimejikuta nacheka mpaka basi...Unajua Zambarau ukiziona mtini ni kama zinakuita sasa ukijipendekeza lazima utengue kiuno matawi yake rahisi sana kukatika...msimu wa zambarau kesi za watoto kuvunjika viungo ni nyingi sana.
 
Utoto raha na hatari sana, tulikuwa tunazifuata zambarau makaburini bila uoga. Leo hii uniambie nikaokote kitu makaburini nile. Thubutu!!
 
kwa kizungu zinaitwaje hizi zambarau. halafu MziziMkavu nini importance take mwilini
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom