Maisha pesa
JF-Expert Member
- Nov 6, 2015
- 681
- 632
Huyu kijana ambae ni kaka mshikaji kiaina kwa sasa baba yake alikua mfanya biashara. Biashara ilianza kunenepa wakati wa awamu wa pili, awamu ya tatu biashara ilikua nzuri kiasi ambacho msure aliamua kijana akasome nje baada ya six.
Alisoma first degree huko nchi za wenzetu. Akiwa mwaka wa pili katika masomo yake, hali ya afya ya mzee ilianza kuzorota. Akiwa kama mtoto mkubwa ilibidi arudi nyumbani. Amerudi Masters ilibidi aingie UDSM. Wakati yuko pale alikutana na mdada mmoja, baba yake akiwa waziri wa awamu ya nne. Mdada alibabaika na swaga za mamtoni za jamaa.
Mtaani kuna binti amemaliza six nae anamzimikia kaka vibaya sana mshikaji akawa anajipoza akija home lakini roho yake yote ilikuwa kwa mtoto wa waziri ambae alishampeleka mpaka kwao.
Wakati anafanya research yake alikuwa nyumbani muda mwingi, baba yake alimshauri kheri aoe kwakua ndiye kijana mkubwa na baba alisema kama sitaona wajukuu zangu angalau nishuhudie harusi yako, kama unavyoona afya yangu inaleta matata.
Lile wazo lilimuingia kijana. Amerudi Dar akaanza kumtafuta mpenzi, alipropose moja kwa moja. Binti kwa dharau sana alimwambia, khe wewe vipi, zaidi ya hivyo vi nguo, sijui simu, na laptop una nini cha maana, unaweza kunitunza mimi wewe? Kwa fedheha kaka wa watu aliondoka. Alirudi kwao weekend ile na kupropose kwa yule dada wa form six mtaani kwao. Kumbe mdada alikua anafunga na kusali lile jambo litokee.
Harusi ilikua nzuri kwani baba aliigharamia kwa uwezo wake wote, kijana alimaliza shule na kupata ajira nzuri. Alianza kumsomesha mke wake, mke yuko chuo bado anasoma, mtoto wa waziri analia anadai jamani ulikua ni utoto, mimi nina kazi yangu basi niko tayari kuzaa tu na wewe.
hahahahaha Malii Wassup hommie..
Huu mfano wako chiboko.Ukiona hivyo huyo mtoto wa waziri kasalitiwa na aliyekuwa anahisi atamuoa, kwa hasira anataka kuharibu ndoa ya mwanamke mwenzake. Wanasema siku zote mwanamke ni adui mkubwa wa haki ukiondoa Chama Cha CCM na utawala uliopita.
Kumbe na wewe yalikukutaeeeh? Pole mwaya!Hizi dharau zilipotezea dhahabu wengi.
Mwisho wa siku tunajipoozaga haukuwa mpango wa Mungu.
ulinifanya kitu mbaya sana we binti ila any way bado sijaoa nakusubiri tuMie ilishanitokea pia wakati niko kigori haswaaa. ... sikumkataa jamaa kwasababu hakuwa na mbele wala nyuma laah bali nilimkataa kwa sababu ya inheritance disease kwenye uko wao. Thank God alikuwa mawazo sana maana aliniambia kila kitu yeye mwenyewe.... jamaa alinizimikia sana pamoja na mengine mengi nyingine ya sababu ya kumwaga ni kuwa na mahusiano ya urafiki wa wadada wengi wazi wazi akijitetea just friends hamna kitu na mie ndo namba one wake........ Wivu ulinishinda nikaona siwezi mitaala mapema hii. Pia alikuwa mtu wa kabila ambao kwao wanavalue sana kuoana wao kwa wao. Mie akaniambia wewe hakuna atayekugusa wewe ni mimi na mimi ni wewe. Ila akaniwarn kuwa mama yake mzazi anaweza asipende pamoja na dada yake..... nikaona cha kuanza stress kabla ya mahusiano nini..... nikamwambia I just want to be among your friends tuu nothing else.
Maskini jamaa hakuamini. .... hadi mwaka juzi alikuwa hajaoa sijui kwa miaka 2 hii sijasikia habari zake.
A friend in deed and a friend in need with no string attached!!
Kasie.
ulinifanya kitu mbaya sana we binti ila any way bado sijaoa nakusubiri tu
Binti kwa dharau sana alimwambia, khe wewe vipi, zaidi ya hivyo vi nguo, sijui simu, na laptop una nini cha maana, unaweza kunitunza mimi wewe? Kwa fedheha kaka wa watu aliondoka.
Mh unataka mengi wewe, ukishajua?