JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Asubuhi ya leo nimeamka na taarifa niliyoikuta mitandaoni kuwa Bodi ya Ligi inayosimamia Ligi Kuu kwamba haijamlipa mshambuliaji wa Simba, Chriss Mugalu fedha zake za Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwezi wa Ligi Kuu.
Nimejaribu kupekenyua sijajua hasa ni ipi inayozungumzia lakini niliyoiona labda ni ile tuzo ya Julai mwaka jana.
Sasa wadau ninachojiuliza, taarifa hiyo ambayo nilianza kuona imefichuliwa na Ricardo Momo wa Wasafi FM, hivi ina ukweli na kama kweli kwa nini mpunga huo haujatolewa hadi leo?
Inamaana wadhamini wa tuzo hiyo hawajatoa mkwanja au ni makusudi tu, hivi lipoje hili wadau?
Nimejaribu kupekenyua sijajua hasa ni ipi inayozungumzia lakini niliyoiona labda ni ile tuzo ya Julai mwaka jana.
Sasa wadau ninachojiuliza, taarifa hiyo ambayo nilianza kuona imefichuliwa na Ricardo Momo wa Wasafi FM, hivi ina ukweli na kama kweli kwa nini mpunga huo haujatolewa hadi leo?
Inamaana wadhamini wa tuzo hiyo hawajatoa mkwanja au ni makusudi tu, hivi lipoje hili wadau?