Hili la Kenya, UDOM mna la kujifunza

Hili la Kenya, UDOM mna la kujifunza

Tky

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2012
Posts
439
Reaction score
140
Kama inavyo fahamika Afrika mashariki UDOM ndio chuo kikubwa. Lakini nina mashaka na ulizi wa hiki chuo, kuna get kubwa moja tu ambalo unapo ingia hukaguliwi ila unapo toka ndio unakaguliwa, hii ina maana kwamba ulizi uliopo ni kwa ajili ya kuzuia uwizi tu na ndio maana wanakagua unapo toka tu na kuzuia uvamizi wa ugaidi haupo maana wanapo ingia hawakaguliwi afu kuna vichochoro vingi vya kuingia hapo chuoni bila ulizi. Wito wangu kwa Serikali liangalieni hili kwa umakini sana.
 
Kama inavyo fahamika Afrika mashariki UDOM ndio chuo kikubwa. Lakini nina mashaka na ulizi wa hiki chuo, kuna get kubwa moja tu ambalo unapo ingia hukaguliwi ila unapo toka ndio unakaguliwa, hii ina maana kwamba ulizi uliopo ni kwa ajili ya kuzuia uwizi tu na ndio maana wanakagua unapo toka tu na kuzuia uvamizi wa ugaidi haupo maana wanapo ingia hawakaguliwi afu kuna vichochoro vingi vya kuingia hapo chuoni bila ulizi. Wito wangu kwa Serikali liangalieni hili kwa umakini sana.
Lugha yako tu ya ulizi inaonyesha wewe ni kutoka nchi jirani. Pia neno uwizi linashahijisha dhana yangu. Ulifuata nini huko? Mbona vyuo vikubwa ni vingi hapa nchini au unataka kutupoteza maboya? Angalia
 
Mbona hujaiunganisha udsm hapo?
udsm sifaham vizur, nimezungumzia udom maana nimesoma miaka mitatu na njia zote za kutoka na kuingia nazifahamu vizuri.
 
udsm sifaham vizur, nimezungumzia udom maana nimesoma miaka mitatu na njia zote za kutoka na kuingia nazifahamu vizuri.
Umesoma UDOM kweli mkuu? Mbona kama siamini amini? Usome UDOM miaka mitatu hata kama ulitoka Congo ushindwe kutofautisha wizi na uwizi ama ulizi na ulinzi. Haya huwa yanatamkwa na jamaa wa nchi jirani
 
Nawe ni mtanzania au ulikuja soma maana lugha yako ni ya kujifunzia ukubwani
 
Umesoma UDOM kweli mkuu? Mbona kama siamini amini? Usome UDOM miaka mitatu hata kama ulitoka Congo ushindwe kutofautisha wizi na uwizi ama ulizi na ulinzi. Haya huwa yanatamkwa na jamaa wa nchi jirani

Hata kama mleta mada ni wa nchi unayoifahamu wewe ila alisemalo naona lina mashiko...tena si kwa udom pekee
 
Udom pale vichaka kibao labda wawatight mkiwa darasani.. Kwanza kuna eneo kubwa sana .
 
Hawa wasomali tusiwaamini sana,hakuna msomali tanzania asiye na ndugu somalia na kenya.Hata hawa waakina kinana na rage wameoa huko shemeji zao nawakwe zao ni wahuko.kuingia huku rahisi sana.
 
Umesoma UDOM kweli mkuu? Mbona kama siamini amini? Usome UDOM miaka mitatu hata kama ulitoka Congo ushindwe kutofautisha wizi na uwizi ama ulizi na ulinzi. Haya huwa yanatamkwa na jamaa wa nchi jirani

Mnang'ang'ana na vitu visivyo katika mada, umeshaelewa changia, sasa wewe unabadilisha mada. Ata ndani ya tz mmakonde hatamki kama mchaga au msukuma, shida iko wapi hapo!
 
Tunavyojadili ugaidi tusiufananishe na kuomba chumvi kwa jirani na mnaowaza hivyo hamjaelewa kiwango cha tisho la hawa jamaa.
Wanaodai kuwa suala la Amboni lilikuwa ni hawa jamaa unadhani wangelitokea sehemu ya jamii tungelikuwa tunasimulia nini leo!? Laki hata kwa jirani na ndugu zetu Wakenya linganisha tukio la Westgate na hili la Garissa ni scenarion mbili tofauti na ndizo zinatoa picha na malengo halisi ya magaidi (ambao wenyewe wanataka waitwe 'freedom fighters')!

No country or community is immune from terrorism, we endelea kuongelea viudom vyenu hivi.
 
Umesoma UDOM kweli mkuu? Mbona kama siamini amini? Usome UDOM miaka mitatu hata kama ulitoka Congo ushindwe kutofautisha wizi na uwizi ama ulizi na ulinzi. Haya huwa yanatamkwa na jamaa wa nchi jirani

Jamani kwanza uelewe kuwa huyu mkuu kaandika akiwa emotional na hali iliyopo.
Mambo mengine ni typing errors.
Tuache kuzodoana km ukielewa alichoandika changia km hukuelewa muulize kwa ufafanuzi
Nakusubiri unizodoe
 
Mnang'ang'ana na vitu visivyo katika mada, umeshaelewa changia, sasa wewe unabadilisha mada. Ata ndani ya tz mmakonde hatamki kama mchaga au msukuma, shida iko wapi hapo!
Nichangie kwamba tuweke mageti UDOM? Kujilinda dhidi ya ugaidi ni zaidi ya kuweka mageti ama kuta kama ukuta wa Berlin.
 
Jamani kwanza uelewe kuwa huyu mkuu kaandika akiwa emotional na hali iliyopo.
Mambo mengine ni typing errors.
Tuache kuzodoana km ukielewa alichoandika changia km hukuelewa muulize kwa ufafanuzi
Nakusubiri unizodoe
Huo ndio uchangiaji wangu kwa hili. Magaidi ni wajanja sana, huko Kenya walisemekana watavamia Nairobi University ama Kenyatta. Kwa bahati mbaya sana wanausalama wa Kenya wakawa wamejikita kwenye maeneo hayo wakasahau sehemu kama Garissa, matokeo yake wameenda Garissa na kusababisha mauaji ya kutisha. Ni vyema kama nchi tukawa macho kila eneo, tukawa makini sana. Huwa mimi nasikitishwa kusikia wahamiaji haramu 100 wamekamatiwa Dodoma ama hata Mbeya. Hii inaonyesha hatuko makini mipakani pia. Haiwezekani watu watembee maelfu ya kilomita bila vyombo vyetu kuwaona.
Tuna sikukuu hizi za pasaka, ni vyema vyombo vyetu vikawa makini pia. Kwa hiyo si UDOM peke yake. Suala la ulinzi ni mtambuka.
 
Umesoma UDOM kweli mkuu? Mbona kama siamini amini? Usome UDOM miaka mitatu hata kama ulitoka Congo ushindwe kutofautisha wizi na uwizi ama ulizi na ulinzi. Haya huwa yanatamkwa na jamaa wa nchi jirani

So unamaanisha jamaa ni muhamiaji haram au??!!!!
 
Umesoma UDOM kweli mkuu? Mbona kama siamini amini? Usome UDOM miaka mitatu hata kama ulitoka Congo ushindwe kutofautisha wizi na uwizi ama ulizi na ulinzi. Haya huwa yanatamkwa na jamaa wa nchi jirani

Anakueleza kitu muhimu, 147 dead in garissa University a day ago
 
Na hivi maisha yenyewe afadhali ya jana, wao waje tuu,
 
Back
Top Bottom