VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Nimeamua kuwadokeza watanzania jambo hili. Kujua chimbuko ni mwanzo wa kujua suluhisho la tatizo, kama lipo. Kwa ubobevu wangu kiutumishi serikalini na chamani, nimefuatilia na kujua chimbuko la mkataba huu 'tata' wa bandari kati ya Serikali yetu na ile ya UAE ikiwakilishwa na kampuni ya DP World.
Sakata la ukodishwaji wa Bandari lilianza mwaka 2016. Ni pale ambapo Serikali ya Hayati Magufuli ilipoona kuwa kuna haja ya kufanya mapitio ya mkataba wa uendeshaji wa Bandari yetu kati ya Serikali na Kampuni ya TICTS. Kampuni ya TICTS ilikuwa na mkataba mrefu wa kuendesha Bandari (hasa upande wa makontena).
Kamati Maalum ya kufanya mapitio hayo ya mkataba wa TICTS iliundwa. Kiongozi wake alikuwa Wakili Hamza Johari, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TCAA). Kazi ilianza mwaka 2016 na kukamilika mwaka 2017. Kati ya matokeo ya mapitio hayo, mkataba wa TICTS ulifanywa kuwa wa miaka mitano (2017-2022). Pia, TICTS waliwekewa malengo ya kuyafikia ili kuweza kupewa mkataba mwingine.
Mwaka 2022 ulipofika, TICTS ilionekana kutotimiza/kutoyafikia malengo ya kimkataba na hivyo ikaondolewa Bandarini. Mamlaka ya Bandari (TPA) ikachukua majukumu yote ya TICTS na kuiendesha Bandari rasmi kuanzia Januari mwaka huu. Lakini, katika kipindi chote cha TICTS na hata cha TPA, Serikali haikuwa ikiridhishwa na utendaji, manufaa na ustawi wa Bandari yetu.
Serikali ikajipanga kupata ufumbuzi. Ukatokea mwaliko wa kuhudhuria Maonesho ya Bidhaa na Huduma mbalimbali huko Dubai, Falme za Kiarabu mwaka 2022. Timu kubwa ya Serikali ikiongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan ilihudhuria. Walikuwapo pia Mawaziri, Wakurugenzi wa Taasisi mbalimbali za kiserikali (zikiwamo TPA na TCAA). Huduma na Bidhaa zikaonwa.
Kutokana na Maonesho hayo ya Dubai, DP World akaonekana. Alionesha, zaidi, masuala ya huduma za kibandari kwenye nchi mbalimbali duniani. Serikali ikatamani kufanya kazi naye. Ikatamani (na si jambo baya) kuwa na huduma kama zilizooneshwa kwenye Maonesho hayo. Ikakata shauri kukaa mezani na DP World, kwa msaada wa Serikali yao, kuona nini cha kufanywa.
Timu ya Majadiliano ya Serikali iliundwa. Ikaongozwa tena na Wakili Msomi Hamza Johari. Timu hii iliundwa na Wajumbe ambao, kwa aslimia zaidi ya 90, walikuwa ni Wanasheria wabobevu katika nyanja ya majadiliano; biashara; uwekezaji na masuala ya Bandari. Majadiliano yakafanyika na Makubaliano pamoja na Mkataba baina ya Serikali zetu ni watoto wa majadiliano hayo.
Kiukweli, hakukuwahi kuwepo na kushindanisha makampuni ili kumpata DP World. Hakukuwahi kuwepo mchakato wa 'kimanunuzi' uliozoeleka wa kushindanisha. Ilitumika 'single source procurement'. Hadi hapo, iko wazi kuwa Maonesho ya Dubai ndiyo chimbuko la Makubaliano na Mkataba uliozua mjadala kila mahala. Na vyote vina baraka ya kiserikali.
Pamoja na nia njema ya kuboresha utendaji na ufanisi wa Bandari yetu, Makubaliano na Mkataba wa Bandari vimeleta sintofahamu kubwa. Vimekataliwa na wanachi kwa kusema na hata kwa kuguna. Bado wananchi wanatoa maoni yao. Waachwe wakosoe. Waachwe wakohoe. Waachwe waboreshe. Waachwe walie na kucheka hadi mabo yawe yanaeleweka.
Hadi hapa, wapo wa kutueleza juu ya hili. Nimewataja. Watuambie, wanayaonaje Makubaliano yaliyozalishwa na Majadiliano? Watuambie wanauonaje Mkataba uliotokana na majadiliano yao? Watuambie, itakuwaje mikataba ya utekelezaji itakayofuata baada ya msingi huu uliojengwa uliozua gumzo na mzozo?
Kosa lolote kwenye Bandari ni hatari!
Mzee Tupatupa wa Lumumba ( kwasasa Chato, Geita)
Sakata la ukodishwaji wa Bandari lilianza mwaka 2016. Ni pale ambapo Serikali ya Hayati Magufuli ilipoona kuwa kuna haja ya kufanya mapitio ya mkataba wa uendeshaji wa Bandari yetu kati ya Serikali na Kampuni ya TICTS. Kampuni ya TICTS ilikuwa na mkataba mrefu wa kuendesha Bandari (hasa upande wa makontena).
Kamati Maalum ya kufanya mapitio hayo ya mkataba wa TICTS iliundwa. Kiongozi wake alikuwa Wakili Hamza Johari, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TCAA). Kazi ilianza mwaka 2016 na kukamilika mwaka 2017. Kati ya matokeo ya mapitio hayo, mkataba wa TICTS ulifanywa kuwa wa miaka mitano (2017-2022). Pia, TICTS waliwekewa malengo ya kuyafikia ili kuweza kupewa mkataba mwingine.
Mwaka 2022 ulipofika, TICTS ilionekana kutotimiza/kutoyafikia malengo ya kimkataba na hivyo ikaondolewa Bandarini. Mamlaka ya Bandari (TPA) ikachukua majukumu yote ya TICTS na kuiendesha Bandari rasmi kuanzia Januari mwaka huu. Lakini, katika kipindi chote cha TICTS na hata cha TPA, Serikali haikuwa ikiridhishwa na utendaji, manufaa na ustawi wa Bandari yetu.
Serikali ikajipanga kupata ufumbuzi. Ukatokea mwaliko wa kuhudhuria Maonesho ya Bidhaa na Huduma mbalimbali huko Dubai, Falme za Kiarabu mwaka 2022. Timu kubwa ya Serikali ikiongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan ilihudhuria. Walikuwapo pia Mawaziri, Wakurugenzi wa Taasisi mbalimbali za kiserikali (zikiwamo TPA na TCAA). Huduma na Bidhaa zikaonwa.
Kutokana na Maonesho hayo ya Dubai, DP World akaonekana. Alionesha, zaidi, masuala ya huduma za kibandari kwenye nchi mbalimbali duniani. Serikali ikatamani kufanya kazi naye. Ikatamani (na si jambo baya) kuwa na huduma kama zilizooneshwa kwenye Maonesho hayo. Ikakata shauri kukaa mezani na DP World, kwa msaada wa Serikali yao, kuona nini cha kufanywa.
Timu ya Majadiliano ya Serikali iliundwa. Ikaongozwa tena na Wakili Msomi Hamza Johari. Timu hii iliundwa na Wajumbe ambao, kwa aslimia zaidi ya 90, walikuwa ni Wanasheria wabobevu katika nyanja ya majadiliano; biashara; uwekezaji na masuala ya Bandari. Majadiliano yakafanyika na Makubaliano pamoja na Mkataba baina ya Serikali zetu ni watoto wa majadiliano hayo.
Kiukweli, hakukuwahi kuwepo na kushindanisha makampuni ili kumpata DP World. Hakukuwahi kuwepo mchakato wa 'kimanunuzi' uliozoeleka wa kushindanisha. Ilitumika 'single source procurement'. Hadi hapo, iko wazi kuwa Maonesho ya Dubai ndiyo chimbuko la Makubaliano na Mkataba uliozua mjadala kila mahala. Na vyote vina baraka ya kiserikali.
Pamoja na nia njema ya kuboresha utendaji na ufanisi wa Bandari yetu, Makubaliano na Mkataba wa Bandari vimeleta sintofahamu kubwa. Vimekataliwa na wanachi kwa kusema na hata kwa kuguna. Bado wananchi wanatoa maoni yao. Waachwe wakosoe. Waachwe wakohoe. Waachwe waboreshe. Waachwe walie na kucheka hadi mabo yawe yanaeleweka.
Hadi hapa, wapo wa kutueleza juu ya hili. Nimewataja. Watuambie, wanayaonaje Makubaliano yaliyozalishwa na Majadiliano? Watuambie wanauonaje Mkataba uliotokana na majadiliano yao? Watuambie, itakuwaje mikataba ya utekelezaji itakayofuata baada ya msingi huu uliojengwa uliozua gumzo na mzozo?
Kosa lolote kwenye Bandari ni hatari!
Mzee Tupatupa wa Lumumba ( kwasasa Chato, Geita)