HILI DARAJA NI HATARI

HILI DARAJA NI HATARI

Kuna mlevi kabla ya kwenda kwake anavuka daraja kama hilo basi akilewa anayumba vibaya sana ila akifika hapo darajani anasimama kwanza dakika kama mbili hivi halafu anavuka vizuri ila akimaliza tu daraja anaanza kuyumba tena!
Oyaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa, mbavu zetu.
 
Njoo ujenge daraja huku kijijini kwetu Mwanangeta.
Ndg. Nilijitolea kujenga kibarabara na kuziba madimbwi kadha//:mmh kilichonipata nikaambia nani kakupa ruhusa kufanya hivyo?" nikaanza kuhaha hapo mie nilishaingia gharma za kununua vifaa,cement,lami na kokotonk nk!!
 
Hapo ni kigoma, kule ilagala kwenye chikichi, halafu huu mto malagalas na kuna mamba wenye njaa hatar
 
wangeweka miti miwili........ mimi hapo kuvuka navuka na makalio aisee yani nitajivuta mapaka nifike upande wa pili
 
Hapo ni kigoma, kule ilagala kwenye chikichi, halafu huu mto malagalas na kuna mamba wenye njaa hatar
Yaani wanaume wote waliyopo kijijini.. hawakuweza kufikiri na kubuni maarifa ya kujenga kadaraja kamiti khaaah !!!! Yaani kweli kwenye miti hakuna wajenzi...kuna wa"" "" ""m !!! Poleni sana!!
 
wangeweka miti miwili........ mimi hapo kuvuka navuka na makalio aisee yani nitajivuta mapaka nifike upande wa pili
Mkuu kuvuka na makalio hapo kuna hatari mbili.

Mosi, unakuwa umemkarbia mamba zaid na kuongeza uwezekano wa kugeuka msosi,

Pili, kuna hatari ya kupoteza bikira yako if at all you are virgin still (ingawa kwa wewe hii haikuhusu maana kitambo kwenye gemu)
 
Yaani wanaume wote waliyopo kijijini.. hawakuweza kufikiri na kubuni maarifa ya kujenga kadaraja kamiti khaaah !!!! Yaani kweli kwenye miti hakuna wajenzi...kuna wa"" "" ""m !!! Poleni sana!!
Nadhan huelewi, hiyo ndo sehem wanafugwa mamba wa kutumwa, imeachwa hivyo makusudi kurahisisha upatikanaji wa sadaka.

Kwa ujumla hata serikaki au msamaria mwema atataka kujenga daraja hapo, kijiji chote kitasimama kwa hasira na kumtimimua
 
Nitapita hapo endapo tu inanilazimu au nna kitu cha muhimu sana cha kufanya ng'ambo yake , otherwise hapana aiseee ntajikuta najikolea kabsaaa ama kudumbukia
 
Nadhan huelewi, hiyo ndo sehem wanafugwa mamba wa kutumwa, imeachwa hivyo makusudi kurahisisha upatikanaji wa sadaka.

Kwa ujumla hata serikaki au msamaria mwema atataka kujenga daraja hapo, kijiji chote kitasimama kwa hasira na kumtimimua
Never !! hata chembe ndogo siamini .. hadithi za MAMBA wa kutumwa !!!!! (siyo kejeli ni imani yangu thabiti)
 
Mkuu kuvuka na makalio hapo kuna hatari mbili.

Mosi, unakuwa umemkarbia mamba zaid na kuongeza uwezekano wa kugeuka msosi,

Pili, kuna hatari ya kupoteza bikira yako if at all you are virgin still (ingawa kwa wewe hii haikuhusu maana kitambo kwenye gemu)
hapo kwenye kukaribia mamba sawa.. ila swala la nikra halipo
 
Nitapita hapo endapo tu inanilazimu au nna kitu cha muhimu sana cha kufanya ng'ambo yake , otherwise hapana aiseee ntajikuta najikolea kabsaaa ama kudumbukia
vp kama ni shule ipo upande wa pili, kama mwenzako hapo?
na shule unatakiwa kwenda na kurudi kila siku
 
Never !! hata chembe ndogo siamini .. hadithi za MAMBA wa kutumwa !!!!! (siyo kejeli ni imani yangu thabiti)
Kuna padri mmoja enzi zile alikuwa anahubiri kigoma akasema kama wewe hivi " hakuna uchawi hapa wala mtoto wa uchawi, shijeni imani yenu nanyi mtakuwa salama" akarudi kukaa kule juu altareni,

alipotaka kunyanyuka tena, kiti kikawa kimenasa makalio, ilibidi asemee pale pale " nimeamini uchawi upo," kiti kikamuachia.

Lakini pia waulize wafuatao habari za uchawi wa kigoma.

Mwl Nyerere ( Ni kigoma pekee wakifanikiwa kumuibia fimbo yake pamoja na kuwa baba wa taifa)

Yusuph Makamba ( huyu alilazimisha wananchi kulima pamba katika kijiji cha ruhita, aliporudi kukagua, wakamuonesha pamba imestawi na kuchanua vizuri, akapiga picha akiwa katika mashamba makubwa ya pamba akarudi mkoani. Picha zilipotoka, akajikuta kumbe alipiga picha zote akiwa katika pori kubwa la kibhambila, mpaka leo kigoma hailimi pamba na makamba alihana ukuu wa mkoa akakimbilia dsm.

Mzindakaya. (Huyu alikuja kwenye vikao vya Tanu kule akwatukana wazee, wakaamua kutundika makoti hewani, kikao kiliishia hapo na mpaka leo usimuulize habar za ujiji.)

List ni ndefu, muulize mshana jr
 
Kuna padri mmoja enzi zile alikuwa anahubiri kigoma akasema kama wewe hivi " hakuna uchawi hapa wala mtoto wa uchawi, shijeni imani yenu nanyi mtakuwa salama" akarudi kukaa kule juu altareni,

alipotaka kunyanyuka tena, kiti kikawa kimenasa makalio, ilibidi asemee pale pale " nimeamini uchawi upo," kiti kikamuachia.

Lakini pia waulize wafuatao habari za uchawi wa kigoma.

Mwl Nyerere ( Ni kigoma pekee wakifanikiwa kumuibia fimbo yake pamoja na kuwa baba wa taifa)

Yusuph Makamba ( huyu alilazimisha wananchi kulima pamba katika kijiji cha ruhita, aliporudi kukagua, wakamuonesha pamba imestawi na kuchanua vizuri, akapiga picha akiwa katika mashamba makubwa ya pamba akarudi mkoani. Picha zilipotoka, akajikuta kumbe alipiga picha zote akiwa katika pori kubwa la kibhambila, mpaka leo kigoma hailimi pamba na makamba alihana ukuu wa mkoa akakimbilia dsm.

Mzindakaya. (Huyu alikuja kwenye vikao vya Tanu kule akwatukana wazee, wakaamua kutundika makoti hewani, kikao kiliishia hapo na mpaka leo usimuulize habar za ujiji.)

List ni ndefu, muulize mshana jr
Mababu zangu ndo waliishi hapo walikuwa hapo ujiji karne iliyopita mbona hawakuliona hilo
 
Mababu zangu ndo waliishi hapo walikuwa hapo ujiji karne iliyopita mbona hawakuliona hilo
Mababu zenu walikuwa na hekima. Si busara hata kidogo kumsimulia mtoto mambo yanayotisha maana utaharibu ubongo wake.

Ujue tu uchawi upo maana hata katika biblia ( Rejea kitabu cha kutoka) wakati musa anawaondoa wana wa israeli kutoka utumwani Misri, kulikuwa na maonesho makubwa ya nguvu za giza wachawi wakishindana na Mungu kugeuza fimbo kuwa nyoka.

Ni busara kujielimisha walau kwa kupitia jf au tembelea maeneo husika.

Mimi siyo mchawi ila nimeishi na wachawi cocords kabisa. Ukifika sehemu, ujikalie kimya tu maana ukiongea kama hayo, utageuzwa Field farm, kila mchawi atataka kujaribu uchawi wake kwako kama utashika. Kama utakutana na wabembe, watajaribu kukugeuza fisi, mbwa ama kunguru ilimradi tu wakuone uwezo wako.

Enzi hizo walimu waliofika pwani ya ziwa Tanganyika, waliomba kubadilishiwa vituo mara moja maana walikuwa wanajikuta wamelala utupu bara barani asubuhi, ikawa mwisho wa viboko mashuleni kwa wageni na Mwanzo wa walimu au wafanya kazi kuukwepa mkoa wa Kigoma.

Kuna miti (mibuyu) mingi ilikiwa ikimeza watu na barabara nyingi zsizokuwa na mwisho zilikuwepo hapo kale ambazo habari zake zastaajabisha. Huwa nikiona mshana Jr akiandika naona kama anaufunua mkoa wa kigoma. Ikumbukwe tu na narudia tena, Mimi si mchawi.
 
ningekuwa mie ndo huyo dent, nahisi ningevuka huku nalia....
 
Back
Top Bottom