Hiki ndiyo kituko nlichowahi kukutana nacho makaburini usiku. Sitosahau

Hizi ishu zinatokea ila hiyo image unavyoona ni ubongo wako mwenyewe tu unakudanganya kwa vile una hofu ya kufirikia kitu fulani kwa sana...Hii inasababishwa na akili za kitoto
No huwezi kusema ni hofu wakati jamaa anasema kwake kupita hapo ilikua kama torati,ni sehemu alishazoea kupita so hakua na hofu nayo
 
Niaje waungwana,

Hiki kisa, au tukio lilintokea miaka mingi kidogo. Enzi zile za kwenda kuangalia movie katika vibanda vya video. Sasa siku hiyo nilienda kuangalia video katika banda moja nililokuwa napenda kwenda kuangalia.

Banda hilo lilikuwa maeneo ya Manzese Midizini kwa mama fulan jina kapuni, na mimi home ni maeneo ya Magomeni mikumi jijini Dar es Salaam.

Njia yangu kubwa kutoka home hadi Midizini, ilikuwa kagera kimamba, nakatiza daraja la mbao, napandisha pale Mburahati Mianzini, napasua Makaburi ya Mburahati kwa jongo hadi midizini. Na kurudi i was doing the same thing kwa kufuata njia ile ile niliyokuja nayo.

Ratiba yangu kwa siku ilikuwa ni shule kwanza, nlipotoka shule, nlielekea mazoezini (mpirani), baada ya kutoka mpirani ndo nikawa naenda sasa kujipoza vibandani kumuangalia Dharmendra, Amita Bachan, Rambo, Anord, Bruce Lee nk.

Ratiba yangu ya mwisho baada ya kutoka huko katika banda la video, ilikuwa ni kwenda katika maskani yetu fulan ambayo ni ya uncle wangu kujifunza mchezo wa karate. Uncle ndo alikuwa masta wetu. Hivyo nilijiamini sana kwamba hakuna kitu au mjinga yeyote anaeweza kunifanyia ushen.z.i mbele yangu. Karate na ngumi ni michezo ambayo humfanya mchezaji ajiamini sana, kwamba anaweza kupambana na mtu yoyote, mahali popote na kwa muda wowote.

Basi bwana siku hiyo nimemaliza kumuangalia Dharmendra mida ya usiku, nakumbuka ilikuwa movie fulan inaitwa LOHA. Tukatoka kila mtu akawa anaelekea kwao. Mimi nikawa natambaa mdogo mdogo kuelekea home.

Nilivyofika katika makaburi ya mburahati kwa jongo kama kawaida yangu, nikageuka nyuma kuangalia huku na huko, sikuona mtu ananifuata nikaendelea na safari yangu.

Sasa nimesogea sogea hadi katikati ya makaburi, kwa mbele nikaona kitu kama mbuzi mweupe, lakini kilichonishangaza na kunitia hofu ni kwamba yule mbuzi alikuwa kama vile amekaa kwenye kitu anavuta sigara, nikafikicha macho kama vile siamini ninachokiona.

Nikaendelea kusogea taratibu ili nihakikishe kuwa ninachokiona ni chenyewe au.

Kusogea nikasikia mbuzi anakohoa, ikabidi nigeuke ili nitoke nduki maana niliona pale hata karate zangu haziwezi kunisaidia.

Sasa wakati nageuka nikaona nyuma yangu kuna kundi la watu wamebeba jeneza wanakuja upande wangu halafu juu ya jeneza kuna mtu kakaa na yeye anavuta fegi, halafu kila jamaa wakipiga hatua, yeye anajamba.

Nikaona nyuma hakufai bora huku huku nilipotaka kupakimbia. Nikageuka na kuanza kutoka nduki kuelekea kwa mbuzi anaevuta sigara. Ghafla nikaona na mbuzi na yeye anatoka nduki na sigara yake.

Akili ikanijia nikaacha kukimbia ule upande anakimbilia mbuzi, nikaelelea upande wangu.

Breki ya kwanza ikawa Magomeni Mapipa, yani sikumbuki hata mikumi home nilipapita saa ngapi, au kule Mapipa nilifika fikaje fikaje.

Nikarudi nyumbani salama. Toka siku hiyo sikurudi tena kwenda video usiku, na ukawa mwisho wa kuendekeza movie.

Ni nani mwngine ambae ashawahi kukumbana na songombingo la aina hiyo?

Aisee it was scary


“Ratiba yangu kwa siku ilikuwa ni shule kwanza, nlipotoka shule, nlielekea mazoezini (mpirani), baada ya kutoka mpirani ndo nikawa naenda sasa kujipoza vibandani kumuangalia Dharmendra, Amita Bachan, Rambo, Anord, Bruce Lee nk"

Kwa ratiba hii, silipi school fee, nenda tu uanze maisha.
 
Niaje waungwana,

Hiki kisa, au tukio lilintokea miaka mingi kidogo. Enzi zile za kwenda kuangalia movie katika vibanda vya video. Sasa siku hiyo nilienda kuangalia video katika banda moja nililokuwa napenda kwenda kuangalia.

Banda hilo lilikuwa maeneo ya Manzese Midizini kwa mama fulan jina kapuni, na mimi home ni maeneo ya Magomeni mikumi jijini Dar es Salaam.

Njia yangu kubwa kutoka home hadi Midizini, ilikuwa kagera kimamba, nakatiza daraja la mbao, napandisha pale Mburahati Mianzini, napasua Makaburi ya Mburahati kwa jongo hadi midizini. Na kurudi i was doing the same thing kwa kufuata njia ile ile niliyokuja nayo.

Ratiba yangu kwa siku ilikuwa ni shule kwanza, nlipotoka shule, nlielekea mazoezini (mpirani), baada ya kutoka mpirani ndo nikawa naenda sasa kujipoza vibandani kumuangalia Dharmendra, Amita Bachan, Rambo, Anord, Bruce Lee nk.

Ratiba yangu ya mwisho baada ya kutoka huko katika banda la video, ilikuwa ni kwenda katika maskani yetu fulan ambayo ni ya uncle wangu kujifunza mchezo wa karate. Uncle ndo alikuwa masta wetu. Hivyo nilijiamini sana kwamba hakuna kitu au mjinga yeyote anaeweza kunifanyia ushen.z.i mbele yangu. Karate na ngumi ni michezo ambayo humfanya mchezaji ajiamini sana, kwamba anaweza kupambana na mtu yoyote, mahali popote na kwa muda wowote.

Basi bwana siku hiyo nimemaliza kumuangalia Dharmendra mida ya usiku, nakumbuka ilikuwa movie fulan inaitwa LOHA. Tukatoka kila mtu akawa anaelekea kwao. Mimi nikawa natambaa mdogo mdogo kuelekea home.

Nilivyofika katika makaburi ya mburahati kwa jongo kama kawaida yangu, nikageuka nyuma kuangalia huku na huko, sikuona mtu ananifuata nikaendelea na safari yangu.

Sasa nimesogea sogea hadi katikati ya makaburi, kwa mbele nikaona kitu kama mbuzi mweupe, lakini kilichonishangaza na kunitia hofu ni kwamba yule mbuzi alikuwa kama vile amekaa kwenye kitu anavuta sigara, nikafikicha macho kama vile siamini ninachokiona.

Nikaendelea kusogea taratibu ili nihakikishe kuwa ninachokiona ni chenyewe au.

Kusogea nikasikia mbuzi anakohoa, ikabidi nigeuke ili nitoke nduki maana niliona pale hata karate zangu haziwezi kunisaidia.

Sasa wakati nageuka nikaona nyuma yangu kuna kundi la watu wamebeba jeneza wanakuja upande wangu halafu juu ya jeneza kuna mtu kakaa na yeye anavuta fegi, halafu kila jamaa wakipiga hatua, yeye anajamba.

Nikaona nyuma hakufai bora huku huku nilipotaka kupakimbia. Nikageuka na kuanza kutoka nduki kuelekea kwa mbuzi anaevuta sigara. Ghafla nikaona na mbuzi na yeye anatoka nduki na sigara yake.

Akili ikanijia nikaacha kukimbia ule upande anakimbilia mbuzi, nikaelelea upande wangu.

Breki ya kwanza ikawa Magomeni Mapipa, yani sikumbuki hata mikumi home nilipapita saa ngapi, au kule Mapipa nilifika fikaje fikaje.

Nikarudi nyumbani salama. Toka siku hiyo sikurudi tena kwenda video usiku, na ukawa mwisho wa kuendekeza movie.

Ni nani mwngine ambae ashawahi kukumbana na songombingo la aina hiyo?

Aisee it was scary


Hemu tuambie ulisoma mpaka degree ngapi? Maama kwa hiyo ratiba hukupaswa kuwa mwanafunzi.
 
No wangetaka kukufika wala wasingeshindwa pia wangetaka ukutane nao kule ulipokimbilia walikua na uwezo huo,sema tuu waliamua kukuonyesha kuwa wapo viumbe wa aina hio
Nafikiri lengo lilikuwa hilo hilo ulilosema. Maana kama kupita nilikuwa napita sana tu. Na nahisi walikuwa wananiona.

Ila siku hiyo pengine walitaka kunionesha kuwa wapo na huwa wananiona sana nikipita.
 
Nafikiri lengo lilikuwa hilo hilo ulilosema. Maana kama kupita nilikuwa napita sana tu. Na nahisi walikuwa wananiona.

Ila siku hiyo pengine walitaka kunionesha kuwa wapo na huwa wananiona sana nikipita.
Yeah mimi binafsi nashukuru sijawahi kukutana na hayo mauzauza na naomba nisikutane nayo mpaka siku nakufa ila naamini hivi viumbe vipo sana tuu
 
Vitu vya ajabu vipo sana ,nakumbuka kipindi nipo kidato cha tatu mwaka 2005 shule x maeneo ya shiyanga.
Baada ya kutoka kwenye kipindi kile cha usiku mida kama ya saa nne kasoro hivi ,kwenye mabweni kuna uwanja wa mpira wa kikapu na baada ya uwanja unavuka barabara kuna kipori fulani

Sasa kwenye pori hilo tulikuwa tunapenda kwenda kujisaidia kama unavyojua vyoo vya shule kukuta vichafu ni jambo la kawaida kwa kipindi kile,hivyo kuna baadhi hatukupendelea kujisave toilet hasa mida ya usiku.
Tulikuwa na tabia ya kualikana kwenda pori kujisave ,sa siku hiyo nikakosa wadau ,ikabidi niliunge mwenyewe nikazama pori peke angu,

Nilienda nikavuka barabara,nikavuka kiwanja cha mipira wa kikapu ,huyooo pori .
Nilijisaidia ,ile nipo hatua ya kumaliza nikashangaa naona gari linapita mle porini,yani kulingana na hali ya pori kwa gari kupita haiwezekani,pana miti ,mashimo ,mawe,visiki nk.

Ila pamoja na hali yote hiyo ile gari ilipita hadi kwenye miti ,inakuwa kama inaigonga miti lakini inazidi kutokomea.
Niliduwaa sana pale chini nilipokuwa nimechuchumaa kwa mana ilipita mbele yangu upande wa kule nilikotoka.

Nilichomoka mbie kutoka huko pori hadi kwenye dom langu.Niliogopa sana ,sikujua kabisa maana ya ile gari iliyo kuwa imejaa watu ikipita kwenye sehemu yenye vikwazo vya miti na vichaka vyote bila tatizo utazani ipo kwenye lami.
Tangu siku hiyo sikurudia kwenda porini kujisaidia.
 
Shule, mpira, video, karate?
Niliandaa maisha yang katika pande zote muhim kama vile elimu na michezo.

Sema ndo hivyo binadam tunapanga yetu na Mungu nae anapanga yake hivyo nilipishana na malengo yangu. Kama wewe mtu mzima utakuwa umeifungua code niliyoweka hapa 😂😂😂
 
Back
Top Bottom