Hii trick ya CCM inafanikiwa

Hebu fikiria! Tutakulipa mishahara yako yoteeh!Tutakulipa na kiinua mgongo na posho zote za vikao mpaka 20! Je kama ni wewe ungekataa!? Na they told you ukikataa tunakupoteza! Utakataaaah? Nina wasiwasi na mungu wa mukulu je ni huyu wa isaka na yakobo!?
 
Hivi huyu mtolea kweli mtaani akipita kwann masela wasimpige mitama dawa ya wasaliti ni kipigo tu...nawaaminia CUF.Ila na yy kafanya maamuz mazito kakaa kawaza 2020 hatoboi so bora ale chake mapemaaa afanye mambo mengine kwli siasa inahitaji ukomavu sana
 
Weka hapa ushahidi kuwa Mh. Mtolea kanunuliwa!
Nawe thibitisha hapa kuwa hajanunuliwa! Jifunze kudifferentiate unaowaandikia humu ukidhani wote wapo level moja na uwezo wao unalingana! Kuna kakikundi kamo humu kutoka lumumba st wanaofadhiliwa kwa kazi kama unayofanya wewe ya kuwaaminisha wasomaji uongo. Bisha! Na kuna kitengo cha siri chini ya wateule wa wilayani na mkoani waliopewa kazi maalumu ya kuwatisha na kuwarubuni wanachama na viongozi wa vyama vingine kujiunga ccm kwa ahadi ya cheo! Hata spika aliwahi kuwaelekeza mawaziri kutokupeleka huduma au maendeleo kwenye maeneo yanayoongozwa na upinzani kama rungu la kuwavunja moyo wananchi!
Ni sawa kwa sababu mna dola na pesa zisizoratibiwa na chombo chochote, zitumieni kuwahonga badala ya kujenga viwanda mlivyoahidi!
 
Najaribu kuwaza, inawezekana kweli wakaua VYAMA VYA UPINZANI, ila wanaweza kuua DHAMIRA ya kipinzani kwenye mioyo ya wenye nchi yao?

Nchi ikishakua ya chama kimoja na kwa bahati mbaya sana haitokua ikiongozwa na mawazo ya wanachama, ni watu wawili tu ndiyo watakaokua wanapanga mambo yaendaje je, wanatosha kuvaa viatu vya watanzania wote zaidi ya 50mil?

Pia hili fukuto litakalo baki na hawa watanzania wenye nchi yao wataweza kulihilimili miaka yote? Wakishindwa nini kitatokea?

Tuombe uzima, Na tuombe hawa wawili wasizime mitandao hasa JF tuje kuona mwisho wake yote haya ni nini.

Mpango wao si wa kuua vyama vya upinzani. Tena nakuhakikishia wanahitaji sana jina la CHADEMA lidumu daima. Ila chama hicho na vingine vyote vya upinzani viongozwe na watu wanaohamasisha wanachama na wafuasi kuunga mkono juhudi za rais kupambana na ufisadi, kulinda rasilimali za taifa, kupigania wanyonge na kujenga Tanzania ya viwanda. Period. Kwao, huo ndio upinzani uliokomaa au upinzani makini; sio huu wa “kupinga kila kitu”.

Leo akina Mbowe wakiamua kuachana na siasa na kuivunja CHADEMA, utasikia kundi la vijana wazalendo “wenye uchungu na nchi” wakijitokeza sawia na kudai wamechukua uongozi wa CHADEMA ili kunusuru chama na kuongoza upinzani makini kuisimamia na kuisaidia serikali ilete maendeleo nchini. Historia inatufahamisha kuwa Mobutu aliunda vyama kibao vya upinzani kupambana na washindani wake wakuu.
 
Waliweza kumnunua Lipumba sembuse Mbunge?
Usisahau na dr slaa. Na hadi sasa bei yake imedhihirika kwani kila mwisho wa mwezi atazilamba ili ile ahadi waliyokubaliana itimie. Nilikuwa na mashaka sana juu ya ile safari ya waziri wa mambo ya nje kama kweli alikwenda kwa ajili ya bombadia iliyowekwa lockup na kumbe badala ya kuitoa kamtoa slaa!
 
Weka hapa ushahidi kuwa Mh. Mtolea kanunuliwa!

Hana kazi, kipato chake ni ubunge aliokuwa nao, leo kaachia Ubunge, Kapoteza mapato yake yote ya kila mwezi?, kapoteza mafao yake ya miaka mitano, karudi kuwa jobless kwa sababu ya kumsupport Magufuli, kweli kajitoa na hajanunuliwa huyu
 
Hana kazi, kipato chake ni ubunge aliokuwa nao, leo kaachia Ubunge, Kapoteza mapato yake yote ya kila mwezi?, kapoteza mafao yake ya miaka mitano, karudi kuwa jobless kwa sababu ya kumsupport Magufuli, kweli kajitoa na hajanunuliwa huyu
Kabla ya kupata Ubunge 2015 alikuwa analishwa na Mumeo?
 
Back
Top Bottom