Hii TAKUKURU ya mwaka huu imeota meno

jaman iv kweli
 

Attachments

  • 1438450409164.jpg
    1438450409164.jpg
    12.4 KB · Views: 191
Inavyoelekea Dr. Edward Hosea ameamua kuwa mtiifu kwa Mh. Lowasa kwa hivisasa.

HOSEA AMEKASIRISHWA SANA na kukatwa kwa EL. sasa anafanya kaz ipasavyo kuwaonyesha WATANZANIA namna maccm yalivyotaabani.. MTOA MADA USIWE NA WASWAS kwan HOSEA NI mtiifu kwa EDWARD..
 
Huko tabora mwenyekiti wa ccm wilaya bw. Moshi konkota akamatwa na pccb akitoa rushwa ili mwakasaka ashinde.
 
Huko tabora mwenyekiti wa ccm wilaya bw. Moshi konkota akamatwa na pccb akitoa rushwa ili mwakasaka ashinde.
 
Inavyoelekea Dr. Edward Hosea ameamua kuwa mtiifu kwa Mh. Lowasa kwa hivisasa.
Sio hivi sasa, huyu ni kambi yake, hata cheo alikipata kwa influence yake!Hii ni sabotage, ccm and the President have to act!Haiwezekani tuhuma bila hata ushahidi unaita vyombo vya habari, huku ni kuchafua image ya CCM!
 
kwakweli hata mm haya meno ya mwaka huu yamenishngaza na sijui yameota lini?

kiuhalisia itakua ni mpango flani unataka kutekelezwa,,jamaa wanakuaga na mbinu za kitoto sana
 
Hawa ccm wameshaona Watanzania Mazuzu, yaani wanatumia Taasisi hii kujipanga ili kuharibu mpango Mzima, hivi Nape kuna mtu mwenye jeuri ya kumkamata na kumuhoji eti mambo ya Rushwa.
Wamechelewa sana, huyu wangemkwatua akiwa kule, huku hakuna mchezo wa Rushwa. Ni Watanzania tu walishaamua kuamua ya kwao.
Ndo ajipange sasa manake dalili za mvua ni mawingu; wakati akiwa kule na jamaa zake wanahimiza wagombea kibao wajitokeze hakustukia drafti lilokuwa linapangwa kuila kingi yake ajue kabisa hilo ni drafti jingine na safari hii kingi ikiliwa ndio baibaiiiii
 
rushwa ni mtuhumiwa na namba mbili katika kesi ya kuwasababishia watanzania walio wengi umasikini mtuhumiwa namba moja akiwa ni ujinga.

siku zote wananchi tumekuwa hatuelewi tunachokitaka na matokeo yake ni kujikuta tukipinga mambo ya kutusaidia na kusapoti yanayotuumiza, ilimradi tunaangalia nani kafanya nini.

rushwa ni adui mkubwa anayewatia wanancchi wengi kwenye lindi la umasikini.

1. tunapata viongozi wengi wabovu kutokana na rushwa.
2. rasilimali zetu hatupati manufaa kutokana na watendaji kupokea rushwa.
3. miradi mingi ya maendeleo inatumia gharama kubwa na kutekelezwa kwa viwango duni kutokana na rushwa.
4. huduma za jamii zinaathiriwa na rushwa.
5. mipango ya kuwawezesha na kuwakomboa masikini inaporwa na matajiri kwa kutumia rushwa.
6. rushwa inasababisha gepu katika ya masikini na matajiri kuendelea kuwa kubwa maana matajiri wanatumia rushwa kuchukua kila kitu huku masikini wasio na cha kutoa kunyanganywa kila kitu.
7. na mengine mengi.

tumeona nia ya dhati katika mchakato huu wa uchaguzi kwa serikali kudhibiti vitendo vya rushwa, kwa maana kunaonyesha political will ya kupambana na rushwa na hapa ndipo pa kuanzia ili kupata watu sahihi.

lakini utashi wa kisiasa pekee hautoshi kama wananchi hawawezi kuuunga mkono jitihada hizi.

ombi langu kwa mashirika na vyama vya kiraia kuielekeza jamii katika kuunga mkono mapambano haya ili jamii yetu ibadilike.

pia naiomba serikali iendeleze jambo hili mpaka mwisho wa uchaguzi ili tupate viongozi bora. lakini ieleweke kuwa kutokutoa rushwa haimaniishi wewe ni bora unastahili kuchaguliwa maana unaweza kutokutoa rushwa kwa sababu hauna na kama ungekuwa nayo ungetoa.

vyama vya kiraia vitoe elimu ya nguvu kwa wakati huu na kuipongeza serikali na kuwaelimisha wananchi kuwa mapambano haya inabidi tunayunge mkono sote ili wale wanaofanya hivyo wasije kuona jamii haiko tayari kupambana na rushwa na mapambano yatafsiriwe kama kujinyonga na hilo linaweza kuondoa nia hii katika mda mfupi tu na tukarudi kulekule.
 
siasa tusipozielewa ni kama michezo ya kuigiza lakini wananchi wanataka nini ndio kitu kinachochagua ni wimbo gani wanasiasa wacheze.

hii ni nafasi yetu sisi kushikilia hapohapo ili kuziweka siasa zetu safi.

wanasiasa wao wanatafuta madaraka hivyo kama mkipenda rushwa na hizo ndizo mnazitumia kutoa madaraka basi kila mwanasiasa atakuja na rushwa lakini mkizichukia na kujua kuwa ndizo zinawanyima maendeleo basi hakuna mwanasiasa atakuletea rushwa.

ujinga wetu unawafanya wananchi wasitambue uadui wa rushwa na kudhani rushwa inawajengea ukaribu na viongozi wao. elimu inahitajika tena sasa ili wananchi wjitambue

Nani kakwambia joka la kibisa lina madhara?
 
Kwa hiyo we ndo umeona serikali imefanya kazi..? Orodhesha watatu tu ambao wapo mahakamani, kama hujakuta wako uraiani na wanaendelea na porojo zao uchaguzi waliopita asilimia kubwa ni kwa rushwa... Acha kutufumba macho.. Hata kwa maskio tunaskia.. Nitajaie hapo angalau watatu nijue, kwa maana tunaskia hata akina nape, mwigulu na wengeni wengi wamepita kwa goli la mkono...! Acha kutumika hasa nyakati hizi za uchaguzi.. Bila mifao hai we ni mlumumba
 
kuwa mahakamani ni hoja ya mtu mbumbumbu kwa maana viongozi wa kisiasa wanatumia mbinu ambazo wananchi wanazitambua lakini ni vigumu kuwaweka hatiani kisheria kutokana na sababu zifuatazo.

kwanza hawa watu wanajua ni ushahidi upi unahitajika mahakamani hivyo hujihadhari katika vitendo vyao ili kusipatikane ushahidi wataalamu wanaita kutokuacha "loose ends"
pili ni jamii ya watu wanyonge ambao wanadhulumiwa na rushwa kutokutoa ushirikiano katika mapambano haya kwani wengi wanapewa rushwa na wanapokea wakidhani ni wakati wao kuchuma kumbe ndio wakati wa kupotea. kama jamii nzima ingejua ikatoa ushirikiano basi wangekamatwa wengi kwa vielelezo.

kwa rushwa za watendaji ni vigumu pia maana kwanza tumeweka mifumo ya kunyenyekea watu na sio taifa. leo hii una ushahidi ukijuifanya kuutoa basi yule uliyemuanika anaenda anahonga anarudi kukushughulikia, au kwa kuwa mifumo yetu sote ni ya ulaji basi waliobaki wanakushughulikia na hakuna chombo cha kukutetea maana kila mtanzania njia za kupata ndio hizo.

kwa yeyote anayejua mazingira tuliyonayo sasa akajifanya kudai ushahidi wa mahakamani basi unajua huyu ni mnafiki asiyemkweli.

jamii nzima inahitaji kubadilika na kuwa na mtizamo wa kupinga vitendo hivyo ndio njia pekee ya kutoka.

Kwa hiyo we ndo umeona serikali imefanya kazi..? Orodhesha watatu tu ambao wapo mahakamani, kama hujakuta wako uraiani na wanaendelea na porojo zao uchaguzi waliopita asilimia kubwa ni kwa rushwa... Acha kutufumba macho.. Hata kwa maskio tunaskia.. Nitajaie hapo angalau watatu nijue, kwa maana tunaskia hata akina nape, mwigulu na wengeni wengi wamepita kwa goli la mkono...! Acha kutumika hasa nyakati hizi za uchaguzi.. Bila mifao hai we ni mlumumba
 
CCM ni chama kinachoamini kwenye misingi ya Rushwa na misingi hiyo ya Rushwa imeonekana kwenye mchakato wake wa kuwachagua wabunge Mpaka kutokea kumizana kwa ubabe wa wagombea ubunge.

Je Ndio chama kinacho jinasibu kushinda october?
 
Ninashuhudia mkipoteza mda mwingi na CHADEMA,Lowasa na Dr.Slaa.Nimeona mkijikakamua kuilamu ITV kwa kuripoti matendo machafu ya rushwa kwenye chaguzi zenu.Leo Chanel 10 imewachoresha kupita kiasi.Mnapataje nafasi za kuchochea mambo ya Chadema mkakosa nafasi ya kukemea rushwa kwenye chaguzi.Ni lipi lina madhara kwenye chama chenu na taifa kati ya Sintofahamu ya Chadema na Rushwa?
 
Hao wote waliokamatwa hakuna ata aliyeshtakiwa waliyamaliza juu kwa juu shikamoo pesa
 
Back
Top Bottom