Hii tabia ya kudharau simu za Tecno itakwisha lini?

Hii tabia ya kudharau simu za Tecno itakwisha lini?

toplemon

JF-Expert Member
Joined
Mar 26, 2017
Posts
4,607
Reaction score
4,766
Tabia ya kudharau simu za Tecno itawaponza milele baadhi yenu milele

Nashangaa hii tabia ikoje kwa sababu ni jambo la kushangaza Watanzania wa humu jf mnadharau simu za Tecno bila sababu zozote zile za msingi

Na watu wamekua wakibeza simu za tecno bila mantiki bila hoja ilhali taifa letu hata kile kichuma au kichwa cha kuchaji simu hatujaweza kuunda

Ni mambo ya ajabu sana katika makampuni yanayojitahidi kutengeneza na kuboresha bidhaa zao ni tecno miaka ya nyuma walikua na changamoto mbalimbali ila kwa sasa wapo vizuri

Angalia uimara wa simu,battery hata camera tunaweza kusema tecno sasa waweza mshindanisha hata na samsung

Kinachosikitisha ni kwamba zaidi ya asilimia 90% ya wana jamiiforum wanatumia tecno

Kama mnakumbuka kipindi ule ujumbe uliokua unatokea kwenye thread au comment za wana humu ule wa "SENT BY USING...

Jf kila mtu ana iphone na samsung ukipost tecno unapopolewa haya mnambie hivi kipind kile cha sent by using....mbona zaidi 90%users zilionekana tecno?hizo iphone au samsung zilipoteleaga wap?

ilionekana zaidi ya 90% ni tecno tu zilikua zinaonekana humu halafu hao hao watu watajifanya wana iphone na samsung tuacheni kufake maisha.

Tuache kubeza kampuni za watu na kuharibu brand za watu jamani mtakujaga kushtakiwa shauri yenu.
 
Smart phone 3 bora Dunia
1)iPhone
2) sumsung
3)Sony experia
NA hapo Sony na sumsung wanashinda
wangombania namba mbili

Smart phone za hovyo 3 Dunia
1)Tecno
2)Huawei
3)iflnix
Mimi sijawai kutumia simu ya smart ya kichina toka simu za kawaida kipindi hiko nilikuwa natumia Nokia sumsung blackberry hizo ndio simu zangu na Sasa natumia Sony kwa matumizi ya kawaida kwa sababu inabebeka na iPad tablet ni ya nyumbani
 
Viva Tecno...

Nilianzia tecno nilionunuliwa na baba, baba hiyo siku aliniuliza nikuletee simu aina gani nikamwambia naomba dk 2 nakujibu.

Nikamuuliza rafiki angu brand ya kuchukua kati ya Tecno na Huawei, akasema chukua Tecno.
Samsung sikuiweka sababu nilikuwa naona ya mama jinsi ilivyo na camera mbaya mbaya tu

Mpaka sahivi natumia tecno ninazo nunua mwenyewe, sijawahi kuwaza kuhama sijui Tecno wameniroga 😩😩
 
Tuna dharau vya wenzetu wakati hata radio call au yale masimu ya mezani hatuwezi kitengeneza?

Tumepumbazwa mno mtu mwenye iphone ya laki 6_7 kumcheka mwenye samsung ya laki tano na mwenye samsung ya laki tank kumcheka mwenye tecno ya laki tatu

Bila kujua pesa mlizonunulia zimejenga uchumi wa mabeberu huku wao wakiwapigisha vita ya maneno kwa kuwaongezea specifications za simu kwenye camera?utadhani mmekuwa wapiga picha)

Kupanua ukubwa wa 'prosesa' na RAM halafu hujawah ku notice any difference kwa maana bado utachomeka laini hizihizi za tigo na airtel ambazo speed yake unapimiwa kwenye kibaba

Wakeup Africa
 
Smart phone 3 bora Dunia
1)iPhone
2) sumsung
3)Sony experia..
Pole sana mkuu huna exposure ya nje ya nchi na wala hujui teknolojia.

Huawei ana simu kali na nzuri kuliko hayo mauchafu yako ya iphone na samsung

Vivo ana simu kali sana kama za nex , Teknolojia ambayo samsung na iphone bado, Hujatembea wewe na unategemea simu za kibongo bongo.

One plus series ni simu kali kuliko hizo samsung na iphone

Hebu jaribu kutembea kidogo.

Mimi binafsi siwezi beba simu ambayo kila mtu ana hiyo brand mfano samsung au iphone

Simu kama one plus 8 pro, Vivo nex dual screen, Huawei P 40 huwezi linganisha na takataka za samsung au iphone.

Wewe unanunua simu Tanzania, kuna simu hapa Tanzania haziletwi kutokana na umaskini wa watu ila mtandaoni unanunua.

Simu ya Vivo nex 1805 ya mwaka 2017 imeizidi hata samsung galaxy s10+ ya mwaka jana 2019
 
Jichange pesa achana na takataka kama samsung na iphone kila mtu anayo

Nunua simu unique hata ukitoa watu wanatikisika na hawawezi kuipata kirahisi

Simu kama. Vivo nex dual screen

- Huawei P40 pro
- Nokia 8 siroco
- Huawei nova 5T
- One plus 8 pro

Vivo nex 1805,Hii ni ya mwaka 2017 ila ni kali kuliko hata samsung za mwaka 2020 kwa matumizi na teknolojia,ni super technology

Achana na mauchafu samsung au iphone kila mtu anayo kama sare za shule
 
Tuna dharau vya wenzetu wakati hata radio call au yale masimu ya mezani hatuwezi kitengeneza?

Tumepumbazwa mno mtu mwenye iphone ya laki 6_7 kumcheka mwenye samsung ya laki tano na mwenye samsung ya laki tank kumcheka mwenye tecno ya laki tatu...
Kiongozi iphone na samsung hakuna kitu

Tatizo Tanzania hakuna soko ndio maana simu haziletwi sana

Brand nzuri ni nyingi sana

Makampuni kama xiomi ya simu kali kuliko hizo

One plus series au vivo ni next level
 
Back
Top Bottom