JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 2,091
- 4,716
Hivi mtu uko kwenye safari zako sijui umetokea wapi mi nakuona kama jirani/rafiki au ndugu napaki gari pembeni mimi ndo naelekea upande wa mjini wewe ndo unarudi unavuka barabara unakuja upande wa abiria unafungua mlango wa gari langu unaingia unavuta mkanda wa abiria unajifunga yani sikuelewi hujui mimi nna mishe gani naelekea wapi unaingia kwenye gari tu unakaa.
Mimi lengo langu ni kusimamisha gari tu na kukusalimia tu kinidhamu ili tujuliane hali na kupeana habari za ya yaliyojiri tu kwa ufupi sijakuambia ufungue gari langu na uingie ukae wakati mimi naelekea upande tofauti na wewe.
Unajuaje kama mimi nilikuwa nawahi kamchepuko kangu hapo mbele au niliagiza mdudu ndo nimepigiwa simu umeiva sasa unaunga tu tela mi sina bajeti na wewe kwa nini tusisalimiane tu nje ya gari ukarudi zako kwako mi niende zangu kwenye mishe zangu kwani nimekuomba kampani yako kwamba nna hela nyingi za kukupa bata na wewe au?
Yani kuna jamaa moja alikuwa kila akiniona natoka na gari lazima anisimamishe alafu anaingia tu kisa anajua ni jumamosi naenda kula bata ajabu nikifika maeneo yangu ya bata yeye yuko kama zombi tu linasubiri pombe tu sasa nani alikuita wewe huku? Nikalitosaga.
Ila sikuhizi naona kuna tabia kama hizi bado zipo kwa watu wanaonifahamu upya kama wageni nashindwa tu kuwachana ila hii tabia sielewi.
Mimi lengo langu ni kusimamisha gari tu na kukusalimia tu kinidhamu ili tujuliane hali na kupeana habari za ya yaliyojiri tu kwa ufupi sijakuambia ufungue gari langu na uingie ukae wakati mimi naelekea upande tofauti na wewe.
Unajuaje kama mimi nilikuwa nawahi kamchepuko kangu hapo mbele au niliagiza mdudu ndo nimepigiwa simu umeiva sasa unaunga tu tela mi sina bajeti na wewe kwa nini tusisalimiane tu nje ya gari ukarudi zako kwako mi niende zangu kwenye mishe zangu kwani nimekuomba kampani yako kwamba nna hela nyingi za kukupa bata na wewe au?
Yani kuna jamaa moja alikuwa kila akiniona natoka na gari lazima anisimamishe alafu anaingia tu kisa anajua ni jumamosi naenda kula bata ajabu nikifika maeneo yangu ya bata yeye yuko kama zombi tu linasubiri pombe tu sasa nani alikuita wewe huku? Nikalitosaga.
Ila sikuhizi naona kuna tabia kama hizi bado zipo kwa watu wanaonifahamu upya kama wageni nashindwa tu kuwachana ila hii tabia sielewi.