Hii style nimeiona kwa wengi mjini

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,595
215,272
Kupata kiwanja cha kujenga nyumba hasa katika prime area ni changamoto kubwa kwa sisi tunao safiri kuelekea uchumi wa kati. Unakuta pango la mwezi unapokaa ni 350, 000, ukipiga hesabu kwa miaka miwili unaona ni kheri ujenge ya kwako.

Umepata kiwanja kwa milioni 20. Bahati nzuri ulikua na akiba ya milioni 5, benki wakakupa milioni 20 mkopo. Rafiki zangu wengi walichofanya ni kujenga nyumba ya kujistiri nyuma ya kiwanja. Ina basic needs tu na kuhamia.

Mbele ya kiwanja anaweka banda la kuku hawa wa kienyeji na matuta manne ya mchicha. Hapo amepiga mahesabu ya kurudisha mkopo. Watoto wakilalamika wamechoka kula mchicha wanapozwa na kuku. Maharage ndiyo kubadilisha menu.
 
Anajenga banda la kuku sehemu ambayo nyumba kubwa itasimama mambo yakiwa sawa.
Hiz habar za kujenga nyumba ndog kwanza halaf et tutajenga kubwa baadae mimi nilishayakataa, unajenga kijumba cha kisela af matokea yke unajikuta unazeekea humo. Kwanini usijipe muda tu ukiinuka unainuka mzima mzima?

Ndio yale unakuta mstaafu anajengea nyumba pesa ya pensheni. Si sawa sana sema tu ndio maisha. Binafsi naona ni bora nijenge bangaloo pagare complete nipige bati na kuingia nitai finish taratibu mdogo mdog kuliko kujenga kijumba kidogo na kukipiga finishing huku nina mpango wa kujenga nyumba kubwa baadae hapana.
 
Ukishapata kiwanja umeshapata password. Ukiwa unaishi hapo hapo Ina accelerate speed. Unaweza kuacha kunywa bia kwa uchungu.
Hahahhaaa...

Hapo kwenye bia umenigusa.

Imebidi nipunguze sana unywaji ili kuondoa kero ndogo ndogo za hapo kwenye mji wangu.

Unaweza kuacha kunywa bia mbili siku hiyo ukapata nyama robo(mlo mmoja) au sangara nusu watoto wakajilamba.

Unaweza potezea bia kwa wiki moja ukapata pesa ya kujiunga bando.

Yaani ni wewe kucheza na hesabu zako tu alimradi pa kulala papo na hubudhiwi na mtu.
 
Hivi kiwanja milioni 20,mkopo million 20, banda la kuku na kuku wake 2 million. Jumla napata kama milioni 42 hivi.

Hivi haiwezekan katika milioni 25~30 kupata nyumba ambayo ipo standard ukiwa umepunguza million 10 za mkopo? Na kuwaepusha watoto kula ugali tembele daily? Au ndio ile lazima tukae madale, mbezi beach, kawe nk!
 
Mtu mwenye uwezo wa kulipa kodi ya nyumba laki 3 na nusu kwa mwezi uchumi wake ni mzuri asee ningekuwa mimi nahamishia maisha pembezoni mwa mji ambako maisha ni nafuu ndani ya miaka 5 ntakuwa nshajenga.
Japo kupanga ni kuchagua.
True... ila hiyo 350 ni normal tu kwa wengi... kijiwen nina bwana mdogo mmoja 26 years tunapiga kazi yy analipa 900k.Mawazo yako haya hutakaa mshawishi...atakupiga makofi 😂
 
Ki ukweli hata mimi nikipata hela uwezi kunishawishi nikakae pembezoni mwa mji yaani nikateseke chumba cha elfu 40, sijui nikaangaike kujenga kanyumba akaeleweki polini uko.

Big No izi hela namtafutia nan sasa mimi nitapanga apartment nzuri mjini uko nitajenga taratibu nikiwa mzee pembezoni mwa mji.

Duniani hatujaletwa kuteseka jamaani.
 
True... ila hiyo 350 ni normal tu kwa wengi... kijiwen nina bwana mdogo mmoja 26 years tunapiga kazi yy analipa 900k.Mawazo yako haya hutakaa mshawishi...atakupiga makofi 😂
Waliojenga maporini ndo wapo mjini sasa. Kuna ndugu yangu mwaka 2007 alienda kujenga chanika porini tena alipata kiwanja 45*90 kwa 900,000tulimcheka sana. Sasa yupo mjini ana nyumba na frem za maduka.

Sisi bado tunakomaa na tunataka viwanja vya mil 15 tena kwa mkopo/

Fainali uzeeni.
 
Mtu mwenye uwezo wa kulipa kodi ya nyumba laki 3 na nusu kwa mwezi uchumi wake ni mzuri asee ningekuwa mimi nahamishia maisha pembezoni mwa mji ambako maisha ni nafuu ndani ya miaka 5 ntakuwa nshajenga.
Japo kupanga ni kuchagua.
Waliojenga porini wapo mjini sasa. Fikiria by 2009 yaoiyokua mapori sasa ni mjini kabisa eg Kinyerezi na Kifuru.
 
Waliojenga maporini ndo wapo mjini sasa. Kuna ndugu yangu mwaka 2007 alienda kujenga chanika porini tena alipata kiwanja 45*90 kwa 900,000tulimcheka sana. Sasa yupo mjini ana nyumba na frem za maduka.
Sisi bado tunakomaa na tunataka viwanja vya mil 15 tena kwa mkopo
Fainali uzeeni.
Sasa rafik tunafanyaje?
 
Back
Top Bottom