Hii ni too much au ni ushamba wangu?

Hii ni too much au ni ushamba wangu?

Sijasema dustbin bali uchafubin ambalo ni kubwa. Piga ua utanitumia tu, tema mate chini tato
Na uajuza wangu huu siolewi tena ....teh teh. Kazi wanayo wasiooa na wasioolewa na wanaotegemea michango ndio waoe? Kwani lazima sherehe? Kafungeni ndoa mrudi nyumbani kuleni pilau na soda. Hata laki tano haifiki.
mtu nitakayemchangia ni ndugu yangu wa damu tu.
 
Kaza moyo wape elfu 50

Waambie hali ngumu iliyobaki utawapa tu mambo yakisimama

Halafu harusi ikipita ndo bye bye
 
Kama mtu huna mpango wa kuja kuwaomba watu mchango huwezi hata kufikiria mara mbili hii issue cse kutoa should be from your heart ili upate baraka na huo mchango wako. Ila ukijilazimisha ili kuwafurahisha watu ndio ushamba wa hali ya juu. Its better to be blamed but you have peace of mind.
Note: Kubanduana wabanduane wao raha wanyimwe wengine
 
Naweza kuchangia mgonjwa apatiwe matibabu apone, harusi!!, ya kwako ww na mkeo!! tena unanipangia!, kama haitoshi unalazimisha!, hata kama ingekuwa sijaoa bado sijashawishika. unachumbia, unalipia mahari, unajipanga unaoa kwa gharama zako ,over
 
Aisee umenigusa ulivyosema kusaidia ndugu na Wazaz Fanya kile Moyo unapendaaaa usijilazimishe kama helaa huna Usitoe na ukiulizwa waambie unamajukum

Usitishie kujamba wakati unaharisha
 
hapo ni kazini kwako na inategemea mnaishije kama wafanyakazi..

mda mwingine unaepusha shari na waswahili.. maana wewe unaweza kupotezea harusi yao wao wakaweka chuki hadi msiba au jambo lolote utakalohitaji msaada wao wakakuponda sana..

kuna mda tunafanya hata tusiyoyataka mradi tu kuepusha shari... huo ndio ukubwa kaka..

wasingekuwa wafanyakazi wenzako au ndugu zako ningesema uchune..

but hao watu mna common interest huwez kimbia..
 
Mm naona kero kwa kwel...huwaga silipi...ofcn washanijua kadi zao za harus hawanipi...
 
Siku hizi imekua lazima, na hizi mambo ya tigo pesa unajikuta huna pa kukwepea, maana wanakaba balaa. ila mi dilisha acha kutoa michango ya harusi, baada ya kutuma pesa kwa m pesa alafu mlengwa akasema mbona hujaweka pesa ya kutolea aisee!

Looh...na ya kutolea tena?
 
Mimi binafsi nilishaachaga kuchangia Harusi, na misiba. Nachangia Ada, na Matibabu tu....! Karibuni......!
 
Inamaana watumishi wote mmekuwa wanakamati au vipi? Hata kama ni wanakamati kiwango cha chini kingekuwa 50 tu.
 
Me ndio maana nimepanga kuoa kimya kimya tu,najua sherehe ya laki 5 itatutosha kabisa na wageni wasiozidi 20.
 
mkuu saidia ndugu zako.
Haina maana kufurahisha watu kwa starehe
na wakati kuna watu wanakuangalia, kukutegemea na kuhitaji
msaada wako.

Mimi sitoagi hata centi moja kwenye maharusu.
ila kila mwezi natoa fedha world vision.

Naamini kama mmeamua kuoana ni jukumu lenu ku save
fedha zenu za harusi. Acheni kutegemea mifuko ya watu .
Kweli kabisa dada. Hii michango ya harusi imekuja kama kutufilisi vile. Suala ni kuacha tu kuchangia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom