MTAZAMO
JF-Expert Member
- Feb 8, 2011
- 19,643
- 33,432
Wasalam mama na dada zangu,
Leo naomba niseme na nyie mawaridi ya ulimwengu huu. Huu ulimwengu ni bure bila nyie, Mungu baada ya kumuumba Adam baadae aliona Adam hakukamilika na alihitaji MSAIDIZI! Hivyo kwa ufupi sana wewe mwanamke ni MSAIDIZI! Najua unajua hilo.
Sasa sikia, tena tega sikio uzuri kabisa! Kuwa msaidizi maana yake ni nini! Maana siku hizi wengi mmeenda shule kama wanaume, mna kazi nzuri kama wanaume, mnafanya hadi kazi za kichungaji kama wanaume! Hivyo kupitia usawa huu kuna mipaka mnavuka bila kujua na ulimwengu unavurugika!
Msaidizi ni yule anayefanya kazi ambayo mwenzake hawezi kufanya! Ni mtu anayekamilisha jambo, anayeleta utimilifu. Inawezekana huyo anayesaidiwa hawezi kufanya au kukamilisha jambo fulani sababu ya asili yake ( mapungufu ya kibinadamu), maumbile, au kutokana na majukumu aliyonayo n.k
Hivyo tunapohubiriwa tutafute wenza wa kufafana nao maana yake si mtu mnayeendana kwa namna ya kibinadamu tu! Mwenza mnaofanana ni yule ambaye Mungu atakupa ili ukawe MSAIDIZI (kwa mwanamke). Kufanana ni wewe kwenda kumtimiliza mwenza wako ktk mapungufu yake.
Hivyo kama mtajua nafasi yenu hapo ulipo kwenye ndoa yako, tutaokoa ndoa nyingi na hazitovunjika kwa petty issues kama ilivyosasa na mtatimiza nafasi yenu ya malezi ya familia. Siku hizi mna walimu wengi na mbaya zaidi wengi ndoa zilishawashinda na hutumia matukio machache mabaya ya ndoa kueneza sumu kuhubiri ubaya wa ndoa na hasa mkiambiwa msiwe wavumilivu ule mliokiri madhabahuni.
Usikiuke kile kiapo na kuvunja ndoa bila baraka za Kanisa ulipokula kiapo.Sisemi mvumilie hadi mambo yanayo hatarisha uhai wenu lakini pia msidanganywe muache asili na nguvu yenu ya uvumilivu. Kama ni mtu wa ibada na unaishi kama MSAIDIZI, Familia yako itapona na mwisho mtajenga jamii na taifa bora.
Mama na dada zangu, nyie ndio chanzo cha dhambi kuingia duniani kwa kumtii shetani kupitia Eva lakini Mungu akawatumia nyie pia kurekebisha hiyo laana kupitia Eva mpya (Bikira Maria) kwa kutii ujumbe wa malaika Gabriel na pale pale kupitia Roho Mtakatifu dunia ikapata mkombozi Yesu Kristo, Maria angeweza kukataa maana ni nafsi huru lakini alitii kwa unyenyekevu! Hivyo hata sasa ukengemfu mwingi unaweza kurekebishwa na nyie kupitia utii na kuitambua nafasi yako.
Itambue nafasi yako kama mwanamke na usimame bila kuyumba ingawa mawimbi ni mengi maana nyie ndio mnaojenga jamii. Fanyeni kazi ya USAIDIZI na si kujaribu kuwa sawa na wanaume! Ndio wanaume wana mapungufu na matatizo mengi lakini hao wanaume wametoka kwenye mikono yenu! Ndio mfahamu madhara ya kutotambua nafasi yenu mnaandaa wanaume wabovu ambao ndio akina baba wa kesho.
Chukueni nafasi yenu mponye ulimwengu!
N.B
Leo ni akina mama tu wapumzisheni akina baba. Pia nimetumia mifano kupitia imani ya Kikristo ninayoifahamu lakini dini zingine wanaweza kuelewa maana mantiki ya ujumbe wa Msaidizi ni kwa binadamu wote.
Leo naomba niseme na nyie mawaridi ya ulimwengu huu. Huu ulimwengu ni bure bila nyie, Mungu baada ya kumuumba Adam baadae aliona Adam hakukamilika na alihitaji MSAIDIZI! Hivyo kwa ufupi sana wewe mwanamke ni MSAIDIZI! Najua unajua hilo.
Sasa sikia, tena tega sikio uzuri kabisa! Kuwa msaidizi maana yake ni nini! Maana siku hizi wengi mmeenda shule kama wanaume, mna kazi nzuri kama wanaume, mnafanya hadi kazi za kichungaji kama wanaume! Hivyo kupitia usawa huu kuna mipaka mnavuka bila kujua na ulimwengu unavurugika!
Msaidizi ni yule anayefanya kazi ambayo mwenzake hawezi kufanya! Ni mtu anayekamilisha jambo, anayeleta utimilifu. Inawezekana huyo anayesaidiwa hawezi kufanya au kukamilisha jambo fulani sababu ya asili yake ( mapungufu ya kibinadamu), maumbile, au kutokana na majukumu aliyonayo n.k
Hivyo tunapohubiriwa tutafute wenza wa kufafana nao maana yake si mtu mnayeendana kwa namna ya kibinadamu tu! Mwenza mnaofanana ni yule ambaye Mungu atakupa ili ukawe MSAIDIZI (kwa mwanamke). Kufanana ni wewe kwenda kumtimiliza mwenza wako ktk mapungufu yake.
Hivyo kama mtajua nafasi yenu hapo ulipo kwenye ndoa yako, tutaokoa ndoa nyingi na hazitovunjika kwa petty issues kama ilivyosasa na mtatimiza nafasi yenu ya malezi ya familia. Siku hizi mna walimu wengi na mbaya zaidi wengi ndoa zilishawashinda na hutumia matukio machache mabaya ya ndoa kueneza sumu kuhubiri ubaya wa ndoa na hasa mkiambiwa msiwe wavumilivu ule mliokiri madhabahuni.
Usikiuke kile kiapo na kuvunja ndoa bila baraka za Kanisa ulipokula kiapo.Sisemi mvumilie hadi mambo yanayo hatarisha uhai wenu lakini pia msidanganywe muache asili na nguvu yenu ya uvumilivu. Kama ni mtu wa ibada na unaishi kama MSAIDIZI, Familia yako itapona na mwisho mtajenga jamii na taifa bora.
Mama na dada zangu, nyie ndio chanzo cha dhambi kuingia duniani kwa kumtii shetani kupitia Eva lakini Mungu akawatumia nyie pia kurekebisha hiyo laana kupitia Eva mpya (Bikira Maria) kwa kutii ujumbe wa malaika Gabriel na pale pale kupitia Roho Mtakatifu dunia ikapata mkombozi Yesu Kristo, Maria angeweza kukataa maana ni nafsi huru lakini alitii kwa unyenyekevu! Hivyo hata sasa ukengemfu mwingi unaweza kurekebishwa na nyie kupitia utii na kuitambua nafasi yako.
Itambue nafasi yako kama mwanamke na usimame bila kuyumba ingawa mawimbi ni mengi maana nyie ndio mnaojenga jamii. Fanyeni kazi ya USAIDIZI na si kujaribu kuwa sawa na wanaume! Ndio wanaume wana mapungufu na matatizo mengi lakini hao wanaume wametoka kwenye mikono yenu! Ndio mfahamu madhara ya kutotambua nafasi yenu mnaandaa wanaume wabovu ambao ndio akina baba wa kesho.
Chukueni nafasi yenu mponye ulimwengu!
N.B
Leo ni akina mama tu wapumzisheni akina baba. Pia nimetumia mifano kupitia imani ya Kikristo ninayoifahamu lakini dini zingine wanaweza kuelewa maana mantiki ya ujumbe wa Msaidizi ni kwa binadamu wote.