Hii ni kali toka kwa Magufuli!

Hii ni kali toka kwa Magufuli!

mpk

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2012
Posts
3,115
Reaction score
3,864
Akiwa Kigoma kwenye mkutano wa hadhara amesema Tanzania ina ng'ombe milioni 22, mbuzi milioni 16 na MBWA MILIONI 6. Hivyo kuna umuhimu wa kujenga kiwanda cha nyama Kigoma!
 
Hizi ahadi hadi raha, kiwanda cha nyama ya mbwa akijenga kigoma hatapa soko zuri...
 
Kweli maccm yamechanganyikiwa-ahadi zinaonekana ni wizi tu-kiwanda cha nyama unajenga kigoma au arusha kwenye wafugaji
 
Hawa wagombea wa ccm hasa wanatuchukuliaje wananchi? Ni kwanini wanaropokaropoka hovyo hivi? Ifike mahali kuwepo na sheria ya kuwashtaki endapo hawatatimiza ahadi zao kwani kututia matumaini ni zaidi ya kutupandisha hasira na kutupoteza kwenye malengo ya kusaka mlo wa siku.
Hii ni dharau kubwa sana kwa wananchi kuahidi yasiyowezekana kwa miaka mingine 100. Tuwanyime kura kuwaonyesha kuwa sisi siyo watoto wa kudanganyishiwa pipi.
 
Atakijenga hicho kiwanda akiwa hukohuko upinzani. Ikulu ya lowassa
 
Duuuh baada ya mkutano kuna kazi ya kuwarudisha watu waliosombwa kutoka vijijini
 
Kiwanda cha nyama za mbwa kigoma, ana utani na wanyalukolo huyu.
 
Kweli maccm yamechanganyikiwa-ahadi zinaonekana ni wizi tu-kiwanda cha nyama unajenga kigoma au arusha kwenye wafugaji

Mmeanza ubinafsi kabla hata ya ushndı.Ng'ombe wengi Arusha???Ngombe wengi wapo Shinyanga,Simiyu,Katavi n.k.Sema kiwanda kiwa Shnyanga au Mwanza.
 
Hv nyie mnataka nini?Mnadai uchumi umedorola lakn mkiambıwa namna ya kuufufua mnakosa imani.
 
Mmeanza ubinafsi kabla hata ya ushndı.Ng'ombe wengi Arusha???Ngombe wengi wapo Shinyanga,Simiyu,Katavi n.k.Sema kiwanda kiwa Shnyanga au Mwanza.

Mbwa wengi wanapatikana wapi?
 
ha!!!!mpaka kiwanda cha nyama ya mbwa au sikusoma vizuri
 
Back
Top Bottom