Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,632
- 697,796
Poleni UVCCM, Poleni sana!
Poleni LMB7, Poleni sana!
Poleni MATAGA, Poleni sana!
Poleni CHAWA wote, Poleni sana!
Hii ni CCM toleo la nne na kimsingi ndio toleo la mwisho, hakuna CCM nyingine baada ya hii!
Toleo la kwamza lilikuwa CCM asili ya Mwalimu Nyerere muasisi na rais wa kwanza wa Tanzania. Hapa hata CCM ya Mzee mwinyi rais wa pili wa Tanzania iko bado kwenye kundi hili la CCM toleo la kwanza
Toleo la pili lilikuwa CCM maslahi. Waasisi wa hili kundi ni marais Benjamin mkapa marehemu na Jakaya Kikwete mstaafu..hapa kigezo kikubwa ni mali, kipato na madaraka.
Hapa ndio vijana wa UVCCM maarufu kama LMB7 sana walipata umaarufu na nguvu kubwa..kwakuwa CCM maslahi waliwatumia vilivyo.
Toleo la tatu ni CCM makinikia. Muasisi wake akiwa ni marehemu John Pombe Magufuli..hawa walichujwa toka CCM asili na CCM maslahi, kisha akachanganya na wahamiaji wa kutosha sana!
Toleo la NNE ni CCM toleo la mwisho; ni CCM inayomezwa na wahamiaji wa kutosha na wasio na background na chama!
Simlaumu Mama Samia kwa hatua hii. CCM aliyorithi toka kwa mwanakwenda ilijaa chawa, wanafiki, watengeneza hujuma na kundi maarufu la MATAGA chini ya mwamvuli wa UVCCM/LMB7.
Hawa hawakuridhishwa na siasa za maridhiano za mama. Hawa hawakufurahishwa kabisa na hatua alizochukua mama kuwapeleka kizimbani makada maarufu wavunja sheria, haki za binadamu, waporaji na wala rushwa.
Hawa daily kwenye makundi yao, mitandaoni na kwenye vikao vyao hawakukoma kumkosoa bimkubwa na kumsema vibaya
Walichokisahau ni kimoja tuu kwamba wao wameshika makali na bimkubwa kashika mpini.
Teuzi mpya muhimu sana za wakuu wa wilaya zimesafisha karibia mabaki yote ya UVCCM, MATAGA NA LMB7. Ni kilio huko kwao. Ni msiba usio na matanga, wamenuna na kukunja sura. Hawaamini mama alichowafanyia!
Na hii ndio CCM toleo la mwisho. Baada ya hii hakuna CCM tena!
Ukipenda waeza hifadhi hii post kwa matumizi ya baadae!
Sent using Jamii Forums mobile app
Poleni LMB7, Poleni sana!
Poleni MATAGA, Poleni sana!
Poleni CHAWA wote, Poleni sana!
Hii ni CCM toleo la nne na kimsingi ndio toleo la mwisho, hakuna CCM nyingine baada ya hii!
Toleo la kwamza lilikuwa CCM asili ya Mwalimu Nyerere muasisi na rais wa kwanza wa Tanzania. Hapa hata CCM ya Mzee mwinyi rais wa pili wa Tanzania iko bado kwenye kundi hili la CCM toleo la kwanza
Toleo la pili lilikuwa CCM maslahi. Waasisi wa hili kundi ni marais Benjamin mkapa marehemu na Jakaya Kikwete mstaafu..hapa kigezo kikubwa ni mali, kipato na madaraka.
Hapa ndio vijana wa UVCCM maarufu kama LMB7 sana walipata umaarufu na nguvu kubwa..kwakuwa CCM maslahi waliwatumia vilivyo.
Toleo la tatu ni CCM makinikia. Muasisi wake akiwa ni marehemu John Pombe Magufuli..hawa walichujwa toka CCM asili na CCM maslahi, kisha akachanganya na wahamiaji wa kutosha sana!
Toleo la NNE ni CCM toleo la mwisho; ni CCM inayomezwa na wahamiaji wa kutosha na wasio na background na chama!
Simlaumu Mama Samia kwa hatua hii. CCM aliyorithi toka kwa mwanakwenda ilijaa chawa, wanafiki, watengeneza hujuma na kundi maarufu la MATAGA chini ya mwamvuli wa UVCCM/LMB7.
Hawa hawakuridhishwa na siasa za maridhiano za mama. Hawa hawakufurahishwa kabisa na hatua alizochukua mama kuwapeleka kizimbani makada maarufu wavunja sheria, haki za binadamu, waporaji na wala rushwa.
Hawa daily kwenye makundi yao, mitandaoni na kwenye vikao vyao hawakukoma kumkosoa bimkubwa na kumsema vibaya
Walichokisahau ni kimoja tuu kwamba wao wameshika makali na bimkubwa kashika mpini.
Teuzi mpya muhimu sana za wakuu wa wilaya zimesafisha karibia mabaki yote ya UVCCM, MATAGA NA LMB7. Ni kilio huko kwao. Ni msiba usio na matanga, wamenuna na kukunja sura. Hawaamini mama alichowafanyia!
Na hii ndio CCM toleo la mwisho. Baada ya hii hakuna CCM tena!
Ukipenda waeza hifadhi hii post kwa matumizi ya baadae!
Sent using Jamii Forums mobile app