MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,171
- 23,976
- Thread starter
-
- #101
Mkuu;Kama umedurusu vizuri historia ya upinzani Tanzania huwezi kuwa dismissive kiasi hiki unless uwe kwenye denial. Tuliokuwepo kuanzia uchaguzi mkuu Wa kwanza Wa vyama vingi mwaka 1995 tunajua. Ni pattern kwa kila chama cha upinzani chenye nguvu kupotea kila awamu mpya inaposhika hatamu. Dr. Lamwai mwaka 1997 alirudi CCM kutoka NCCR Mageuzi, kina Kasanga Tumbo, Fundikira na wengine wote walirudi CCM.
Soma historia na usiwe mbishi kwa vile tu akili yako INA matamanio makubwa kwa upinzani
hizi ndoto zilikuwepo tangu enzi za mwalimu. lakini mwishowake ndio hayo...wakat mwingine tujifunze kukubali ukweli hata ukiwa mchunguHizo ni ndoto za mchana kweupe. Kwa mwenye akili kama yako,ataamini hivyo,Ila ukweli ni kwamba CCM wanatengeneza CHADEMA imara kuliko wakati mwingine wowote
If you don't believe me, take my words
Fikiria mara mbili kama kweli mbinu hii inaisaidia CHADEMA au inaiangamiza kabisa.CHADEMA haiwezi kufa kwa mbinu za kijinga kama hizi. Nawaona waliobuni mbinu hii kama vile wana akili ndogo. Wanafikiria kinyumenyume. CCM wanaifanyia CHADEMA 'pruning' bila wao kujua, hivyo itachipua upya na kwa nguvu.
[/QUOTE]NCCR-Mageuzi iliingia kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1995 ikiwa ni chama kikuu cha upinzani nchini..
NCCR-Mageuzi imekuwepo tokea kwenye utawala wa awamu ya Rais Mwinyi.
CUF iliendelea kuwa chama kikuu cha upinzani hata baada ya uchaguzi wa mwaka 2005.
CHADEMA haikuwa kuwa chama kikuu cha upinzani mwaka 2005. Nimekuambia baada ya Uchaguzi mkuu mwaka 2005, CUF iliendelea kuwa chama kikuu cha upinzani.
Wewe ndiye unafikiria masuala ambayo sikuweka kwenye mada yangu.
Kazeni buti kuongeza madau makubwa makubwa mnaweza kufanikiwa...
Sometime uwa ckuelewi unaandika nn. Unauliza chama gani kinategemewa kuchukua nafasi ya chadema. Je umejiuliza kwanini chadema inakufa?? Na Kama chadema inakufa umejiuliza Tena inakufa kwasababu zipi. Unategemea chadema ikifa Kuna chama itakuja kwass mbadala. Muda mwingine Kama huna cha kuandika Bora ukae kimyaThere’s a saying that goes like: Once is chance, twice is coincidence, third time is pattern.
Nimeanza na angalizo hapo juu ili kuwasaidia wale ambao watadhani andiko langu ni kama ramli bila kuangalia ukweli wa historia.
Kwa wale wanaojua vizuri historia ya siasa za Tanzania lazima watatambua kuwa kila utawala mpya unaongia madarakani kwa tiketi ya TANU/CCM huhakikisha unafuta nguvu ya chama kikuu kilichokuwa cha upinzani na huibuka chama kingine kuchukua nafasi hiyo.
Mkakati huu hufanikiwa sana kwa sababu TANU/CCM ni Chama Dola na pia migogoro ya kiungozi ndani ya chama kikuu cha upinzani. Ninaposema CCM ni Chama Dola nina maana kuwa huwezi kuitenganisha CCM na ‘’Kitengo’’. Kitengo kwa lugha ya kiingereza kinaitwa Deep State. Swali labda utauliza, kwa nini huwezi kuitenganisha CCM na Kitengo (Deep State)? Jibu fupi ni kwa sababu Taifa letu limeundwa katika muundo huo.
Ifahamike kuwa chama kinakuwa ni kikuu cha upinzani kama kina wabunge na madiwani wengi. Ikumbukwe pesa za ruzuku zinategemea wingi wa Wabunge, Madiwani na kura za Urais. Huwezi kuendesha kwa mafanikio chama cha siasa nchini bila pesa za ruzuku toka serikalini.
Katika utawala wa Mwl. Nyerere mwaka 1961 kulikuwa na chama kikuu cha upinzani kulichoitwa ANC chini ya Zuberi Mtemvu lakini kufikia mwaka 1965 Rais Nyerere akawa amekifuta katika uso wa dunia.
Tuliona katika utawala wa Rais Mwinyi kulikuwa na NCCR-Mageuzi ambayo ilikuwa ni chama kikuu cha upinzani.
NCCR-Mageuzi iliingia kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1995 ikiwa ni chama kikuu cha upinzani nchini.
Baada ya Rais Mkapa kuingia madarakani mwaka 1995 alihakikisha nguvu ya NCCR-Mageuzi kama chama kikuu cha upinzani inapotea nchini.
Kwa kudhihirisha hilo tuliona katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2000 NCCR-Mageuzi ikizikwa kama chama kikuu cha upinzani ambapo chama cha CUF chini ya Prof. Lipumba kiliibuka kuwa chama kikuu cha Upinzani nchini.
CUF iliingia kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka 2005 ikiwa ni chama kikuu cha upinzani nchini ambapo Rais Kikwete alichaguliwa kuwa Rais huku CUF ikiendelea kuwa chama kikuu cha upinzani.
Baada ya kuingia madarakani, Rais Kikwete alihakikisha nguvu ya CUF inapotea kama chama kikuu cha upinzani nchini.
Kwa kudhihirisha azma hiyo tuliona katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 CUF ikizikwa kama chama kikuu cha upinzani nchini ambapo CHADEMA kiliibuka kuwa chama kikuu cha upinzani nchini.
Kama ilivyokuwa kwa NCCR-Mageuzi na CUF, tumeona CHADEMA ikiingia kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka 2015 ikiwa ni chama kikuu cha upinzani na kutoka bado ikiwa chama kikuu cha upinzani nchini.
Kama historia inavyobainisha basi kifo cha CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani ni baada ya Uchaguzi Mkuu 2020.
Kwa wale wanatumia upeo mkubwa katika kuchambua na kuchanganua masuala ya kisiasa nchini watagundua kuwa dalili za CHADEMA kupotea kama chama kikuu cha upinzani nchini zimeanza kujionesha.
CHADEMA demise is a real thing, and it's happening now!
Hoja iliyoko mbele yetu kwa sasa ni chama gani kitachukua nafasi ya CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani nchini baada ya Uchaguzi Mkuu 2020?
Ni chama gani kinaandaliwa kwa sasa ili kuchukua nafasi ya CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani kama ambavyo CUF iliandaliwa kuchukua nafasi ya NCCR-Mageuzi na CHADEMA kuchukua nafasi ya CUF?
Nadhani wanaotumia 3D thinking and reasoning wamejua ni chama kipi kinaandaliwa kuchukua nafasi ya CHADEMA!
Mkuu;Ungekuwa unajua maana ya upinzani usingeandika hili gazeti lako. Upinzani siyo kikundi cha watu, upinzani siyo CHADEMA,CUF au ACT- Wazalendo, upinzani ni mawazo ,upinzani ni fikra,upinzani ni utashi. Nataka nikuambie leo unaweza kuua mtu lakini huwezi kuua mawazo na fikra. Hii maana yake nini CHADEMA na CUF vinaweza kufa lakini fikra na mawazo hayawezi kufa. Upinzani ni maisha ya mwanadamu.Kila sehemu kuna upinzani ,kwenye familia kuna upinzani ,ndani ya CHADEMA kuna upinzani ,CCM pia kuna upinzani.
Mkuu;
Hakuna anayesema CHADEMA itakufa. Ninachosema CHADEMA itadhoofika.
Tatizo ambalo ninadhani linakusumbua ni kudhani kuwa CHADEMA ni kama Baba na Mama kuwa huwezi kuachana naye au kumkataa.
Historia inaonyesha hata NCCR-Mageuzi ilikuwa na wafuasi kama ilivyo CHADEMA lakini hao hao wafuasi waliondoka na kuwa wafuasi wa CUF.
Hao hao wafuasi wa CUF waliondoka na kuwa wafuasi wa CHADEMA. Hoja yangu ni kuwa usidhani hawa wafuasi wa CHADEMA wataendelea kuwepo kama kesho tutaamka na kujikuta CHADEMA sio chama kikuu cha upinzani nchini.
Muda utaongea chief.Fikiria mara mbili kama kweli mbinu hii inaisaidia CHADEMA au inaiangamiza kabisa.
Kwa jinsi wasiodhaniwa wanavyojiunga na CCM inasababisha kutoaminiana kati ya viongozi na wanachama wa upunzani hii tunaita Divide and Rule (divide et impera in Latin).
Haujasikia mheshimiwa flani alitaka kupigana na mwezie kisa kutuhumiana usaliti kwamba mbunge flani anataka kuunga mkono juhudi za mwenyekiti wa chama cha kijani?
Haujasikia kanda ya ziwa kuna watu wamevuliwa vyeo na kufukuzwa chamani kisa wanahisiwa kusaliti chama kwa kutaka kujiunga chama kingine?
Kifupi CHADEMA wameshaingia mkenge wanaanza kushambuliana wenyewe kwa wenyewe huku adui akifurahia. Leo kwenye vikao vyao vya ndani vya madiwani, wabunge na viongozi wa CHADEMA na hata vyama vingine vya upinzani hawaaminiani tena sababu hawajui nani anahama kesho na atapeleka mikakati ya siri kwa mpinzani wao.
historia ya KANU siyo historia ya CCM, hitoria ya UPC siyo historia ya CCM, eti kwa kuwa KANU na UPC ambavyo ni vyama viasisi katika nchi zao vimekufa/ kudhofika basi na CCM ambayo ni chama mwasisi wa nchi yetu kupitia TANU na TAA (siyo taa ya chemli)nayo itadhofika/itakufa.Mkuu;
Mimi nimejenga hoja ya kihistoria lakini wewe ulichofanya ni kujenga hoja kwa hisia zako.
Kwa hizi hisia zako hata NCCR-Mageuzi na CUF walisema kile ulichokiandika lakini leo sio vyama vikuu vya upinzani nchini!
Una maana gani unaposema hakuna idadi ya wapiga kura?
Nimesema Chama chochote makini cha siasa ni kushika dola. Ndio maana huwezi kukuta eti sheria inasema ili uchaguzi ufanyike ni lazima pawepo na idadi fulani ya wapiga kura.
Kuna vitu vingi hujui, usijifanye mjuaji sana.
Ni kweli wanatumia mbinu "tofauti" kudhoofisha au kutaka kuua vyama vya upinzani lakini wote kinacho wapa kiburi ni UCHAMADOLA na likatiba libovu. Na ukichunguza sana ni uchu wa madaraka-lazima tushinde sisi, na hapo ndo CHAMADOLA kinapotumika. Mfano mnyime ruzuku Maalim, mpa Ruzuku Lipumba. Mpe Lipumba ulinzi, mnyime Maalim ulinzi. Hakuna mikutano ya hadhara, lakini wewe kila leo una mikutano inayo rushwa na TBC etc, na ndani yake unapiga siasa.Hata Mbinu aliyotumia Mwl. Nyerere kukifuta chama cha ANC ni tofauti na mbinu aliyotumia Mkapa kuidhoofisha NCCR-Mageuzi, Hata Kikwete alitumia mbinu tofauti kuidhoofisha CUF.
Vivyo hivyo hata Magufuli atatumia mbinu nyingine ili kuidhoofisha CHADEMA
Hili genge lifutike tu, hakuna namna nyingine ya hili genge kusavaivuThere’s a saying that goes like: Once is chance, twice is coincidence, third time is pattern.
Nimeanza na angalizo hapo juu ili kuwasaidia wale ambao watadhani andiko langu ni kama ramli bila kuangalia ukweli wa historia.
Kwa wale wanaojua vizuri historia ya siasa za Tanzania lazima watatambua kuwa kila utawala mpya unaongia madarakani kwa tiketi ya TANU/CCM huhakikisha unafuta nguvu ya chama kikuu kilichokuwa cha upinzani na huibuka chama kingine kuchukua nafasi hiyo.
Mkakati huu hufanikiwa sana kwa sababu TANU/CCM ni Chama Dola na pia migogoro ya kiungozi ndani ya chama kikuu cha upinzani. Ninaposema CCM ni Chama Dola nina maana kuwa huwezi kuitenganisha CCM na ‘’Kitengo’’. Kitengo kwa lugha ya kiingereza kinaitwa Deep State. Swali labda utauliza, kwa nini huwezi kuitenganisha CCM na Kitengo (Deep State)? Jibu fupi ni kwa sababu Taifa letu limeundwa katika muundo huo.
Ifahamike kuwa chama kinakuwa ni kikuu cha upinzani kama kina wabunge na madiwani wengi. Ikumbukwe pesa za ruzuku zinategemea wingi wa Wabunge, Madiwani na kura za Urais. Huwezi kuendesha kwa mafanikio chama cha siasa nchini bila pesa za ruzuku toka serikalini.
Katika utawala wa Mwl. Nyerere mwaka 1961 kulikuwa na chama kikuu cha upinzani kulichoitwa ANC chini ya Zuberi Mtemvu lakini kufikia mwaka 1965 Rais Nyerere akawa amekifuta katika uso wa dunia.
Tuliona katika utawala wa Rais Mwinyi kulikuwa na NCCR-Mageuzi ambayo ilikuwa ni chama kikuu cha upinzani.
NCCR-Mageuzi iliingia kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1995 ikiwa ni chama kikuu cha upinzani nchini.
Baada ya Rais Mkapa kuingia madarakani mwaka 1995 alihakikisha nguvu ya NCCR-Mageuzi kama chama kikuu cha upinzani inapotea nchini.
Kwa kudhihirisha hilo tuliona katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2000 NCCR-Mageuzi ikizikwa kama chama kikuu cha upinzani ambapo chama cha CUF chini ya Prof. Lipumba kiliibuka kuwa chama kikuu cha Upinzani nchini.
CUF iliingia kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka 2005 ikiwa ni chama kikuu cha upinzani nchini ambapo Rais Kikwete alichaguliwa kuwa Rais huku CUF ikiendelea kuwa chama kikuu cha upinzani.
Baada ya kuingia madarakani, Rais Kikwete alihakikisha nguvu ya CUF inapotea kama chama kikuu cha upinzani nchini.
Kwa kudhihirisha azma hiyo tuliona katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 CUF ikizikwa kama chama kikuu cha upinzani nchini ambapo CHADEMA kiliibuka kuwa chama kikuu cha upinzani nchini.
Kama ilivyokuwa kwa NCCR-Mageuzi na CUF, tumeona CHADEMA ikiingia kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka 2015 ikiwa ni chama kikuu cha upinzani na kutoka bado ikiwa chama kikuu cha upinzani nchini.
Kama historia inavyobainisha basi kifo cha CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani ni baada ya Uchaguzi Mkuu 2020.
Kwa wale wanatumia upeo mkubwa katika kuchambua na kuchanganua masuala ya kisiasa nchini watagundua kuwa dalili za CHADEMA kupotea kama chama kikuu cha upinzani nchini zimeanza kujionesha.
CHADEMA demise is a real thing, and it's happening now!
Hoja iliyoko mbele yetu kwa sasa ni chama gani kitachukua nafasi ya CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani nchini baada ya Uchaguzi Mkuu 2020?
Ni chama gani kinaandaliwa kwa sasa ili kuchukua nafasi ya CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani kama ambavyo CUF iliandaliwa kuchukua nafasi ya NCCR-Mageuzi na CHADEMA kuchukua nafasi ya CUF?
Nadhani wanaotumia 3D thinking and reasoning wamejua ni chama kipi kinaandaliwa kuchukua nafasi ya CHADEMA!
Halijalishi ni akili za Lumumba au Ufipa, kinachoangaliwa ni hoja kutoka kwenye hiyo akili.Akili za Lumumba hizi... Hayo yote ya kuua upinzani ni kwa faida ya nani hasa?