Hii ni aina gani ya nyoka?

Hii ni aina gani ya nyoka?

Morogoro mjini wapi mkuu,sema kama upo mikese huko. Hao nyoka ndiyo wengi sehemu hizo.

Sent using iphone pro max
 
Sibaru, Mkuu sibaru,

Nyoka mwenye sumu anakuwa na hizi sifa.

1. Triangled head shape

2. Fangs nyie mnaita meno

3. Single caudal row. Michirizi kama ya duara bila kugawa ktkt ya mgongo wa nyoka.

Achana na habar za rangi sijui nini.

Sent using iphone pro max
 
Huyo nyoka Anaitwa "BROWN HOUSE SNAKE" hana sumu ata kidogo
 
Ukimtoa chatu waliobaki wote wana sumu ila sasa suku zao zimegawanyika makundi mawili yaani "VENOM" pamoja na "POISON" kwa hapo tunapata nyoka wa aina mbili "POISONOUS SNAKES" pamoja na "VENOMOUS SNAKES" tuangalie kwanz kuhusiana na hizo sumu zao .

Poson hii ni aina ya sumu ambayo ikiingizwa mwilini kupitia njia ya damu moja kwa moja huwa haina madhara ya kuondoa uhai bali utajiskia vibaya tu wakati mwili ukiendelea kupambana nayo ,hivyo ni sawa na kusema uking'atwa na poisonous snake hauwezi kufa (nadhani hapa ndo wanajichanganya kusema kwamba hana sumu).
Poison inakuwa na madhara kama ikiingizwa kwa njia ya kinywa moja kwa moja, hapa ndipo unakuta nyoka ukimla bila ya kumuandaa vizuri na kitaalamu lazima upate madhara makubwa .

Venom hii ni aina ya sumu ambayo ikiingizwa mwilini kupitia njia ya damu moja kwa moja huwa ina madhara makubwa kutegemeana na aina ya nyoka aliyeiingiza mfano cobra,black mamba na wengineo na hivyo ni sawa na kusema uking'atwa na venomous snake upo katika hatari ya kupoteza maisha kama hautawahishiwa matibabu.
Venom ikiingizwa kwa njia ya kinywa moja kwa moja huwa haina madhara ya kukuweka hatarini labda uwe na vidonda vya tumbo au michubuko ambayo inavujisha damu kwenye utumbo.
Sasa tuangalie makundi haya ya nyoka.

1).POISONOUS SNAKES.
Hawa ni jamii ya nyoka ambao hawana vichwa vilivyokaa muundo wa pembe tatu(vichwa vyao ni virefu vimenyooka kwa kwenda mbele ) na miili yao haina magamba magumu wala rangi za kuvutia na huwa wakikung'ata moja kwa moja hautapata madhara ya kuondoa uhai.
Kingine ni kuwa wanapikung'ata huwa wanaacha matundu mengi ya meno mahali walipopang'ata.

2).VENOMOUS SNAKES.
Hawa ni jamii ya nyoka ambao vichwa vyao vimekaa muundo wa pembe tatu,na mara nyingi huwa na rangi za kuvutia pamoja na magamba magumu .
Kingine ni kuwa wanapokung'ata huwa wanaacha matundu mawili pekee kwenye eneo waliloling'ata ,na kama usipowahishiwa msaada wa haraka upo hatarini na unaweza poteza maisha .

Tukirudi kwenye swali lako , ni kuwa huyo nyoka ni poisonous na hana madhara kwa mtu wala mnyama yoyote ni jamii ya rat snakes (ptyas fusca) na anajulikana kama white bellied-rat snakes hawa nyoka ni wazuri kwenye kupambana na panya na chakula chao kikuu ni samaki ,mijusi pamoja na wadudu wadogo huwa wanapenda mazingira ya pori pori, na ukimchokoza mara nyingi husimamisha kichwa kama ishara ya kujihami hali ya kuwa hana madhara kwako hata akikung'ata.

Nimeona nitoe elimu kidogo kwa maana sio kila nyoka ni wa kuuwa wengine muwe mnawafukuzia maporini au mpige dawa za kuwazuia wasisogele maeneo mliyopo ila msiwaue wana faida kubwa sana kuliko tunavyodhani.

Picha hizi hapa chini zitaweza kukuonesha utofauti wao kwa urahisi.
snakevenomous.jpeg
Screenshot_2020-04-16-08-59-30.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naona watu mnatoa elimu zisizo rasmi kwanza huyo ni mfupi mno kwa black mamba, kingine black mamba mdomo wake huwa ni mweusi sana.

Sababu nyengine ni kuwa msingemuuwa kirahisi hivyo bila ya kupata angalau vifo visivyopungua 10 .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom