Elections 2010 Hii Ndo Tanga Zaidi Ya Uijuavyo!

Kilichofanyika ni kukarabati ile ya zamani jamani tusidanganyane

1049.jpg
Abdallah, Mohamed Rished[CCM]

Pangani Constituency
Session NoQuestion NumberTo the Ministry of SectorDate Asked 1145INFRASTRUCTURE DEVELOPMENTCommunication/Infrastructure11 April 2008 Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa majibu ya matumaini aliyoyatoa jana, ambayo Wananchi wa Pangani wameyapata, lakini leo Mheshimiwa Waziri ametoa majibu ambayo matumaini yameanza kufifia.

Mheshimiwa Spika, kama alivyosema Mheshimiwa Waziri, suala la Kivuko cha Pangani, dharura ya sasa kwa muda wa mwaka mzima ni lazima tupate injini mpya kwa sababu tunahatarisha maisha ya wananchi mwaka mzima. Serikali wanasema hawataki kununua mashine mbili mpya; thamani ya roho za wananchi wale na injini mbili mpya ipi kubwa; mpaka tufe ndiyo tutaleta injini mbili mpya? Je, ni lini mtatununulia injini mbili mpya zifungwe katika Kivuko cha Pangani?
ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION # 45 SESSION # 11
1133.jpg
Answer From Hon.Mahanga, Dr. Milton Makongoro
INFRASTRUCTURE DEVELOPMENTNAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA MIUNDOMBINU:

Mheshimiwa Spika, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Rished Abdallah, kama ifuatavyo:-

Kwanza, nimpongeze kwa kweli kwa namna anavyofuatilia; ni kati ya Wabunge ambao ufuatiliaji wao katika matatizo ya wananchi wa majimbo yao ni mzuri sana.

Mheshimiwa Spika, lakini nimeeleza kwamba, kwa mujibu wa TANROADS mwezi huu wa nne kabla ya mwisho, tutakuwa tumetiliana saini kuleta kivuko kipya na kwa maana hiyo, itachukua mwaka mmoja kivuko kipya kuja.

Mheshimiwa Spika, lakini kama unavyojua, kwa uzoefu tulionao, injini ya vivuko kama hivi, pamoja na propeller yake ambayo inatakiwa vilevile, unapoagiza mchakato ule wote si chini ya miezi sita; huendi tu kuchukua na kesho ukawa umeleta injini kwa maana kwamba, tukileta na kwa matatizo ya fedha tuliyonayo ni kwamba, hata hiyo injini itafika karibu na kivuko chenyewe kipya kufika. Kwa hiyo, imeonekana ni busara kwamba, tuendelee kutengeneza hapa, yaani kukarabati injini na boti ile na sasa hivi tumepata maombi ya shilingi milioni 35, kwa ajili ya kukiweka katika hali nzuri, hela ambazo wizara yetu itadhamini kwa sababu TEMESA wana matatizo kidogo ili feri ile iendelee kufanya kazi kwa mwaka huu mmoja ambapo tunangojea feri mpya, kwa sababu kuleta injini nyingine itakuja wakati ambapo hiyo feri mpya nayo itakuwa inakaribia kufika.

Kazi kinafanya????
 
wapendwa yanini kulumbana, kikubwa ni kwamba tunahitaji mabadiliko kwa ajili ya maisha yetu. yafaa nini chama kimoja kiendelee kuiongoza nchi hii yenye vyama vingi vya siasa? all in all, waliyoyafanya, mazuri kwa mabaya, tunayakubali, lakini utamu wa jembe kupokezana ndugu zangu, mwenge zikuzote hukimkibizwa na wengi, hata kama ni mlo jamani huwa hubadillishwa, tule chakula cha aina moja tangia uzaliwe mpaka ufe! siutapata malnutrition! kwa kifupi kila kiongozi huja na tija yake au kila chama huja na bidii yake ya kuleta maendeleo, Angalia mfano wa marekani na nchi zingine zilizoendelea, watu hawana time na kung'ang'ania chama kimoja, watu wanaangalia nani mwenye mtazamo wa maendeleo, sio kudanganywa na mihadi hewa, tulidanganywa maisha bora badala yake maisha ndo yamekuwa magumu kupita kiasi, hata kama angetekeleza yote si sababu tosha kwa chama kiomja cha siasa kunga'nga'nia madarakani kwa miaka na minaka. ni sawa na wewe usome kidato kimoja miaka na miaka, je utajiita na wewe ni msomi? ndgu zangu siasa si ugomvi cha msingi hasa this new generation, let us make changes. for our future. mwenye kuelewa na alielewe neno hili, angalia mfano wa zimbabwe yule ndingi kang'ang'ana cheki uchumi wao, walipo unda serikali ya mseto at list now jamani ccm msiogope kushindwa asiye shindwa si mshindani, punzikeni tulizeni akili, na hao mafisadi walio zoea kunyonya serikali ya ccm wajifunze kujitegemea, walau kwa miaka kumi tu then hata mkirudi mtakuwa wajanja kidogo, maana mtakuwa mmejifunza mengi na mtakuja na mbinu mpya ya uongozi badala ya uongozi wa sasa wakifamilia na kirafiki, na ushindi wa wizi wa kura kila uchaguzi unaofanyika. Jamani ni busara sana kuwasikiliza wanachi kuliko kujing'ang'aniza madarakani, hata hizi chi zinazopigana wenyewe kwa wenyewe chanzo ni mambo kama haya wanayo fanya ccm. ila ukimkimbiza mjusi sana anaweza akakung'ata.twendeni tu

Tafuta threaad imeandikwa Mabere Marando.Soma ucheke.
 
Pata ujumbe wa rais kupitia video hii

 
Last edited by a moderator:
duh,kuna mtu kaniuliza kama nafahamu jiolojia ya hapo pangani.mkuu hii ni karne ya 21,watu wamefika mpaka mars,wewe bado umenangania jioljia?yaani sisi watanzania tunatafuta njia za mkato sana kusolve problems zetu.tunapenda ku postpone matatizo badala ya kusolve them promptly.ukitaka bana,kila kitu kina wezekana.yaani unaniambia hapa daraja ni imposible?sasa we tembea china,utaona madaraja,na jiolojia ndiyo usiseme.let me tell you.IF THERE IS A WILL,THERE IS A WAY,but we tanzanians we like simple things,easy to get,we dont want to work hard.
 
JF kuna kazi, ndugu ya kunani unataka kuniambia watanzani ni wavivu? mimi naamini kabisa watanzania ni wachapa kazi isipokuwa kinachotuangusha ni mfumo mbaya wa utendaji wa serikali yetu ya CCM, hapa kilichojadiliwa ni ahadi za CCM kivuko cha Pangani kimetumika kama mfano tu wa ahadi hizo, sasa inashingaza hawa makada wa CCM mnyalukola Anyisile na Kunani kutaka kututoa nje mada tunayoijadili, kama mnataka tujadili maeneo tunayoishi ama tunayotoka anzisheni topic tuanze kujadili kwani utakayoyaona yatakushangaza, hiyo Pangani utaiona bora mara elfu maana angalau wao wana usafiri, umeme, barabara, hospitali na huduma nyingine za kijamii, zipo sehemu nyingi sana Tanzania huduma hizo ni ndoto kutokana na ahadi za CCM, Kunani acha kutumia picha za magazeti kama ungefika china usingeitumia kama mfano, China wana resources zote muhimu za maendeleo jeje sisi tunazo? Naona umezungumzia kuwa watu wamefika mars, ni hivi mpaka sasa hivi hakuna binadamu ambaye ambaye amefika mars NASA wamefanikiwa kutuma chombo isipokuwa wanataka ifikapo 2020 wawe wameshapeleka binadamu kama walivyoepeleka mwezini, lets use this forum as tool to educate one another instead of bring down our morales
 
Hivi hiyo sound track ni original au imepikwa? Naona kama jamaa anaongea maneno yasiyotoka akilini mwak kabisa.

Inategemea akili yako ikoje.Kama kubeba box kumekuwa kugumu utaona imepikwa:becky:
 
shukrani CCM, tupe zingine ambazo zimetekelezwa na mimi naanza wanajamvi mnaweza kuongezea ambazo hazitekelezwa, yaani ahadi zilizotelekezwa:
1. daraja la kigamboni
2. maisha bora kwa kila mtanzania
3.
4.
5.
6.

2. maisha bora kwa kila mtanzania
 
Back
Top Bottom