Hii ndiyo Tanzania mpya chini ya Lowassa!

Hii ndiyo Tanzania mpya chini ya Lowassa!

Ukawa imezeeka ghafla.

12109036_1511170319203725_7893429866689020787_n.jpg
Nadhani unaposema UKAWA unakuwa huitendei haki sheria ya vyama vya siasa nchini!

Hakuna chama cha siasa kinachoitwa UKAWA!

Kama una maana ya CHADEMA pia utakuwa huitendei haki CHADEMA.

CHADEMA kama chama haijazeeka bali fikra na malengo ya viongozi wakuu wa CHADEMA kwa sasa ghafla yanajidhihirisha kuzeeka!
 
Hawa wamejitolea kusimamia ukweli na hawakuja kutaka ubunge na kadhalika. Nafasi za wanaukawa hazijachukuliwa na wageni kwahivyo Ukawa hawana budi kuwakaribisha
 
Hii ni kejeli bila shaka. Afrika kusini mpya ilifana chini ya Mandela aliyekuwa na umri wa miaka zaidi ya 70. hawa unaowabaini kama wazee wanachochea fursa ya mabadiliko kwa vijana. Mawazo yao ndio yana matter. The vision and mission!
 
Haya ndiyo Mabadiliko Lowassa, Lowassa mabadiliko!

Hii ndiyo safu ya Tanzania mpya yenye fikra mpya!

Kuna wengine wamekuwa viongozi katika nafasi za juu kabisa za utendaji kabla hata nchi haijapata uhuru!

Hii ndiyo safu itakayowakimbiza Watanzania kwa speed ya km 120!

Ninashindwa kuelewa kama ninaota au ninaishi kwenye ndoto!

There are no desperate situations, there are only desperate people-Heinz Guderian

Haya ndiyo mabadiliko tunayoyataka!

Tanzania iko mbioni kuingia kwenye Guinness World Records!

12109036_1511170319203725_7893429866689020787_n.jpg

c

Lowassa unasubiri kuapishwa tu
 
Nadhani unaposema UKAWA unakuwa huitendei haki sheria ya vyama vya siasa nchini!

Hakuna chama cha siasa kinachoitwa UKAWA!

Kama una maana ya CHADEMA pia utakuwa huitendei haki CHADEMA.

CHADEMA kama chama haijazeeka bali fikra na malengo ya viongozi wakuu wa CHADEMA kwa sasa ghafla yanajidhihirisha kuzeeka!
Hapo nimetumia lugha-picha tu kwa hiyo usiwe na mchecheto. Ninaelewa wazi UKAWA sio chama cha siasa. Baada ya kuona wamepoteza dira CHADEMA waliamua kujificha nyuma ya muungano wa UKAWA; na kama hiyo haikutosha wameamua kukubali waliokuwa wanachama wa CCM kupeperusha bendera kwenye kampeni zao. Ndio siasa za upinzani Tanzania hizo.
 
Hawana jipya. Walisha pewa nafas kibao za kuwatumikia watanzania hamna lolote walilofanya. Tujaribu magufuli.
 
Hebu ipange hiyo safu katika wizara 8 muhimu.
Kisha uniambie hiyo kasi ya kumzidi mlugo itatoka wali na kwa nani.
Muongeze na Lema na Sugu hapo juu.

Sumaye keshasema hakuna wanaojua utumishi wa umma huko.

Speed 120.
Utashangaa

Watanzania tumelemaa na majina ya wanasiasa wa TV, wanaoweza kuongoza wako wengi sana.
 
Hebu ipange hiyo safu katika wizara 8 muhimu.
Kisha uniambie hiyo kasi ya kumzidi mlugo itatoka wali na kwa nani.
Muongeze na Lema na Sugu hapo juu.

Sumaye keshasema hakuna wanaojua utumishi wa umma huko.

Speed 120.
Utashangaa
Nisaidie na wewe kushangaa au kuota!

Tuko mbioni kama taifa kuingia kwenye vitabu vya maajabu ya dunia!
 
Hawa watu nafikiri wanatuona watanzania wote ni mambululu wanataka kutimuza ndoto uzeeni
 
unamdanganya nani, wewe mpiga debe wa mr push-up????? Kibaki na wazee wenzake huko kenya, walimwacha moi na kanu yake, na kujiunga na upinzani, na matokeo ya spidi 120 yalionekana. Nenda kenya hata leo ukaulize, watakwambia kazi za kibaki aliyekuwa hataki maneno mengi, kama lowassa. Hatudanganyiki!!!!!!!!!! Tumekwisha kuamua, rais wetu ni lowassaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!

mpe za usoni bwana.mwambie aangalie thika super highway. Halafu alinganishe na huu mradi wa kichawi unaoitwa dart. Sasa avute pumzi na kujibu swali kati ya kibaki na kikwete ambaye ni mzee ni nani?
 
Katika hao kuna waliokuwa na nafas za juu sana. Ni mwapachu tu hajawahi kuwa juu sana.
Wengine hao wamewah kuwa na madaraka na nafas nyet sana lakin wapi hamna kitu

Waliishia kupiga rushwa au kuchekea rushwa ikipigwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom