Hii ndio Tanzania ya viwanda

Hii ndio Tanzania ya viwanda

hakuna sheria iliyovunjwa. ishu ni kwamba, Kiongozi wa mbio za Mwenge ana mamlaka ya kumwamuru DC? Kwa hiyo huyu kiongozi wa mbio za mwenge ana renki ya Mkuu wa Mkoa? au waziri? au waziri mkuu? au makamu wa Rais? au ana renki ya Rais ? au juu ya Rais? you see the point? mambo shaghalabaghala!!!
Mkuu kuna kitu kinaitwa "akiliccm au siku hizi -MATUMBILI" hawana muda wa kujiuliza chochote zaidi ya kile ambacho wamekuwa programmed nacho! wakimezeshwa uchafu watautapika huohuo
 
Nisijeitwa mchochezi sijawahi penda hili dibwana kabisa
Unapoishia kutokulipenda, mimi ndo naanzia hapo.

Nilipandisha uzi humu wa kuliponda, naona mods wameuchinjia baharini akati uzi ulipokelewa vizuri mno na wadau
 
mwenge unachochea maendeleo hasa vijijini ni alama yetu lazima tuidumishe
Duh!

Bila mwenge maendeleo hayaji?

Yaani unakuta mwenge unapita shule ya secondary kuzindua kakisima ka maji au choo.

Wakati wenzetu wanazindua hata treni za umeme bila mwenge
 
Maambukizi mapya ya ukimwi, mimba zisizotarajiwa, zinaa holela, unyanyasaji wa kijinsia, kusimamisha shughuli za kiuchumi, uvutaji bhangi, ulevi, kutumia vibaya rasilimali na fedha za Taifa nk.

Kweli ni kichocheo cha maendeleo kwa wagonga meza na kupiga mayowe
Kwa maendeleo ya aina hiyo, na mimi naunga mkono kwamba kweli Mwenge ni kichocheo cha maendeleo. pia ni mahali pa kukuza unafiki. Tuseme tu kwamba kulikuwa na wakati Mwenge ulikuwa na maana kubwa tu, kama icon ya yale tunayoamini. Wakati huo Tanzania ikiwa nchi ya mstari wa mbele katika ukombozi wa Afrika. wakati huo Tanzania ikiwa ni sauti kali inayosikika duniani kote kupinga maonevu, unyonyaji, ukoloni, ukandamizaji. Hapo Mwenge ulilkuwa na maana. Wakati huo Siasa ni kilimo, katika kujenga taifa la wakulima na wafanyakazi. viwanda chekwa chekwa. ndani ya nchi Nyerere akihaha mikoani kusimamia kilimo, nje ya nchi kusimamia maslahi ya wanaoonewa popote duniani. Kuna wengi, wakiwemo waalimu maarufu katika Chuo Kikuu cha DSM na akina Mabala, waliovutiwa na misimamo ya Nyerere na wakaamua kuja Tanzania kupiga kazi.

Leo Tanzania hata haieleweki inasimamia kitu gani. Tumeanzisha mahusiano na mfalme wa Moroko, nchi inayokalia Sahara Magharibi kwa mabavu. Magu kamsujudia cheki bobu yule, akamomba amjengee msikiti na kitu gani sijui - uwanja wa mpira vile? Tumeanzisha mahusiano na Israeli, nchi inayomiliki taifa jingine la wapalestina, kama koloni lao. enzi hiyo hao wote walikuwa hawawezi kuisogelea Tanzania.

Enzi hizo TANU ilisema "BINADAMU WOTE NI NDUGU ZANGU NA AFRIKA NI MOJA" wakati huo usingesikia Nyerere anasema fulani siyo raia! Maana yake nini? wakati tunajenga Afrika moja, wakati mipaka iliwekwa na wakoloni ili watutawale? leo tunasema haya warundi nenda huko, wakati sisi wenyewe tukianza kuangaliana vizuri, ni Mgogo tu ndio mzaliwa wa nchi hii. lakini lengo siyo hilo. lengo ni kujenga Afrika iliyo imara na inayoamini katika usawa wa binadamu.

Ndani ya nchi hatueleweki pia. Kilimo tumekipiga kumbo, tunatangaza nchi ya viwanda wakati Nyerere hata hakusema hayo lakini alijenga viwanda vya kuheshimika. leo tunaongelea vyerehani vinne. Tunaporwa mali zetu kwa sababu ya upofu. Nyerere aliuona mchezo mzima akasema ngoja tujipange kwanza ndio tuchimbe madini yetu. Akaja Lofa Mkapa akatuingiza mkenge. Tuliingia kwa miswada ya dharura na kwa papara, leo tunataka kujinasua kwa miswada ya dharura na kwa papara vile vile. hatujifunzi tu?

Kifupi niseme tu kwamba Mwenge wakati ule kweli ulikuwa ni ishara ya mwanga wa Taifa la Tanzania kuangaza Afrika na dunia nzima. leo sisi ni kiiiza kinene. hatuwezi kuangaza popote. Mwenge umeshapoteza maana yake siku nyingi.
 
Huu mwenge naona ni njia tu watu wanatumia kijitafutia ulaji, hamna kitu hapo.
 
Unajua kinacho onekana ni kwamba hakuna hata mmoja kati ya viongozi wa hii awamu walikuwa na hisia kama wangefika kwenye hizo nafasi hata siku moja. Kwahiyo hakuna mwenye kujua uongozi wa sheria ukoje.
Wanadhani kila litokalo kinywani kwao ni aheria. Hii ni hatari sana kukaa na viongozi ambao mawazo yao ni kutawala kwa vitisho na kutumia dola.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kweli kabisa, kuna ombwe la uongozi ambalo wanaopwaya wanajaribu kuliziba kwa vitisho, matamko na sanaa huku wakivitumia vibaya vyombo vya umma.

Udhaifu wa ungozi ni tatizo sugu la nchi yetu.
 
Back
Top Bottom