Hii ndio Tanzania tunayoitaka

OBO5

Member
Jan 31, 2013
54
35
HII NDIYO TANZANIA TUITAKAYO!!

Taifa langu la Tanzania ni taifa la kisomi na lililojaaaliwa watu wenye akili nyingi sana pengine kushinda wale magwiji wa kale kama akina Socrates, Aristotle na Plato katika falsafa na pengine hata majina maarufu katika sayansi kama Isaac Newton, Albert Einstein na Charles Darwin.

Kupata daraja la kwanza katika mitihani inayoandaliwa na baraza la mitihani la Taifa (NECTA) na pengine GPA katika vyuo vyetu vikuu ni kigezo pekee kinachotumika kuchanganua mchele na pumba, zile pumba zikipachikwa ei kei ei ya vilaza. Kipimio hiki cha kisasa na cha kwanza ulimwenguni kutumika nchini kwangu kinabainisha kuwa ukipanga unaanzia daraja la kwanza na kuishia daraja la pili na wale wanaoanzia daraja la tatu ni vilaza.

Kuthibitisha hili teuzi zote za kisiasa zimekuwa zikishehenishwa majina yaliyovikwa vibwagizo kama dakta ama profesa. Kwa tafsiri isiyo rasmi ni lazima uwe msomi mwenye pihechidi au profesa kabisa kuwa na kigezo cha kuitwa kipanga hivyo kuweza kubeba dhamana ya kuwea kuongoza taifa hili la Afrika kusini mwa jangwa la sahara lenye wasomi wengi.

Ukaguzi wa vyeti feki kwa kada ya watumishi wa umma serikalini pia ni namna nyingnine ya kuudhihirishia ulimwengu kuwa taifa hili ni la wasomi. Utambuzi wa wasomi hewa katia taifa la kisomi hauwezi fanyika mara moja ni lazima kuwe na duru nyingi kadiri iwezekanavyo ili kuwabaini wale wasiokuwa wasomi wa maana. Katika mataifa ya kisomi kama hili la kwangu utaratibu wa kutambua wasomi hewa huwa hautumi rasilimali wala muda wa shughuli zingine za kimaendeleo maana tayari watu wetu ni wasomi.

Ukilaza katika taifa hili ni laana, ukilaza wenyewe siyo ule uhayawani wala ukichaa, ni kushindwa kupatwa daraja la kwanza au la pili au kikubwa zaidi kutopata majina yalikutangulia jina lako la kwanza kungoja majina yasiyokwepeka kama marehemu, hayati ama mista na misezi ambayo wanadamu karibia wote huyapata katika vipindi vya uhai au umauti.

Wasomi wetu wengi wanamaono ya mbali kweli, kwani hamjui kuwa dunia inazunguka??? Ndiyo ya jana ni hapana ya kesho. Nafsi ilimsuta msomi wetu kipindi cha kampeni za kuelekea uchaguzi mkuu leo imesuuzika. Usomi wake ni mzuri
maana eti nasikia kule Uropa kubadili mtazamo ni mpaka ufanye sijui risechi!!!! Huku ni hapana………

Kuna msomi wetu wa sheria ambaye ndo mlezi wa vyama vingi nae keshatia neno………Ila kwa kweli juu yake sijui kama ni msomi kwa kigezo cha nchi au ni ule usomi wa wanasheria!!! Wao kila mmoja wao ni msomi!!!

Leo tarehe ishirini na sita septemba nimeliangalia li-mwalimu la pale mlimani, dakta Benson Bana, taarifa ya habari ya Aitivi…….safi sana. Limesema wazi kabisa kuwa kile chama cha msomi kimejikita sana visiwani kuliko huku mrima!!!!! Wasomi mnatumia Tanzania bara. Yaani kale kakitabu kalikoandikwa na mzee Pius Msekwa mwaka 1977 sijui mnakaita ka-katiba na kufanyiwa marekebisho mwaka 1992 kuleta mfumo wa vyama vingi ni kaajabu kweli. Eti ibara ya 20(2) inakataza usajili wa chama cha siasa kinachofanya siasa eneo moja la Jamhuri ya Muungano. Ajabu kweli!!!!!.

Ukipatwa na mkosi wa kuwa kilaza mlilie mja wako maana utasemwa na kutukanwa sana katika hadhira na kadamnasi zinazojadili mustakabali na maslahi mapana ya
taifa letu la kisomi. Utachekwa hata na mtoto mchanga maana unatia najisi taifa hili teule la bwana katika usomi.

Katika taifa langu majitu kama lie li-rais la Afrika kusini li-Jacob Zuma ni bure kabisa…….yaani taifa kama hili liongozwe na li-rais lisilosoma?, hata yule Simba wa vita mzee Rashid Mfaume Kawawa mwombeeni alale mahali pema peponi na ajivunie kuongoza enzi za mwalimu sasa ivi na kale kadarasa kake ka-kumi na mbili uwaziri ukuu wa Jamhuri ya Muungano wa Wasomi wa Tanzania angeusikia TIBSI baadae TIYUTI na TIBISI tena, tunataka wasomi.

Ivi kwani yule kiiongozi wa wimeni wing’i wa iliyouwa TaaNuru, Bi Titi Mohamed alifika Makerere Koleji? Muulizeni atupatie jibu ili kama alifika basi tubadili mtaala vijama wamsome katika historia. Kuna mtu anaitwa Edward Mpringe Sokoine nae nina wasiwasi nae kama kweli anafaa kuwekwa kwenye listi ya mawaziri wakuu waliopata litumikia taifa………..enzi za mwalimu za kuokota okota wachunga ng’ombe kule Monduli hatuzitaki kabisa.

Mzee Aman Abeid Karume tunamcheka kwa kuleta Muungano huku akiwa hajasoma, ule mkataba wa muungano wa Tanganyika na Zanzibar mbona
unainyonya Zanzibar. Tatizo la mzee huyu lilikuwa lile lile. Si kweli kwamba alikuwa mzalendo akipigania maslahi ya mzanzibar na Afrika kiujumla, hapana tunakataa.

Ivi huyu kijana anayejiita Daiyamondi Platinaamz au wale ze orijino komedi wamefika wapi katika vidato vyao maana naona mwaka 2020 siyo mbali na yamkini tutawahitaji tena. Chama chetu cha Mapinduzi mwana wa ile TaaNuru na Eiesip kina uhitaji wa watu vipanga katika kuendesha kampeni za kisomi katika taifa la watu wasomi…………………………..

Ala! Ivi huyu mwandishi nae ni msomi ebooo! Hatuhitaji waandishi vilaza katika taifa hili. Mwandishi mwenyewe kumbe licha ya kusoma kwa kodi za watanzania hata akahitimu kilee chuo kikuu cha vipanga cha Taifa ni kilaza. Ni kilaza kwa sababu hana sifa ya kuwa nayale majina yatanguliwayo na sifa ya umauti pekee! Mwandishi ni kilaza mzuri.

Taifa ni lazima liingie kwenye vitabu vya rekodi katika ulimwengu hasa lile li-ginesi buku ovu wedi rekodizi ndo tunalitaka haswaa kwa nini kila siku Marekani na China katika Uchumi na sayansi, Pakistani, Syria na Somalia katika vita. Daaaah! Nuksi
kweli yaani mpaka wale watoto wa boko haram, ali shaababu na Aiesi wanatufunika kwa umaarufu???? HATA!

MWANDISHI NI MAGAKA
 
Back
Top Bottom