WAZIWAZI
JF-Expert Member
- Mar 10, 2014
- 1,807
- 1,561
- Thread starter
- #61
Maneno kuntu kwa ndugu zetu hawa labda waweke pamba masikioni.Nikupe "big up" GENTAMYCINE kwa mawazo na fikra pevu kwa CHADEMA ili wajenge chama imara cha upinzani.
Hilo litafanikiwa siyo tu kubali ulichokiita mwendelezo wa Visasi au Uhasama au kuendekeza uwongo, majungu na chuki ila kubadili kabisa safu ya uongozi wa chama.
Kama unavyodhani kuna tatizo mahala ndani ya Utawala / Uongozi wao wa juu kabisa, na mimi nahisi hivyo. Ushahidi ni maneno, lugha na matendo ya hao viongozi, yasiyo na chembe ya ustaarabu kabisa. Wanayatoa na kutenda pasipo tofauti na vichaa.
Kama kuwa kiongozi wa CHADEMA sifa ni uongo, unafiki, kuongea kwa sauti, na kutukana, basi kuna nchi CHADEMA itatawala na siyo Tanzania. Hata wendawazimu watawakimbia.
WATAFAKARI NA KUCHUKUA HATUA