Hii ndio njia rahisi ya kuishi na wanawake

STUNTER

JF-Expert Member
Dec 15, 2015
13,077
17,207
Ilikuwa jioni moja tulivu,mwanamke mmoja alielekea kisimani kuteka maji,, alipokuwa huko kisimani Mara akatokea mwanaume mmoja na kumuuliza yule mwanamke "samahani dadangu hivi unaweza kunitajia visa vya mwanamke?".

Yule mwanamke ghafla akaanza kulia huku anapiga makelele kwa sauti sana, hali iliyofanya wanakijiji wengi watoke mbio wakiwa na mapanga na marungu kuelekea huko kisimani!.

Mara yule mwanamke akachukua ndoo ya maji na kujimwagia mwili nzima, wanakijiji walipofika wakauliza kwa hasira kuna nini hapa?. Yule mwanamke akajibu"nilikua nimetumbukia kisimani na huyu baba ndio ameniokoa".

Wanakijiji wakampa hongera yule mwanaume kwa alichokifanya kisha wakasambaa. Yule mwanamke akamgeukia yule mwanaume na kumwambia "hivyo ndivyo visa vya mwanamke, ukimchukiza anaweza kukuua na ukimpenda anaweza kukulinda''.
 
Na hata ukifanya ajali kwa gari kwa bahati mbaya na kwenye gari uko na mwanamke mfano umemgonga jamaa wa bodaboda...Ukipata upenyo muweke mwanamke kwenye streering chap kama yeye ndo alikuwa anadrive hakika shurba haitakuwa kubwa na yataisha salama...Uje ukutwe kwenye steering ni mwanaume utazungukwa na bodaboda kama buku na gari itachomwa.....Wana-nguvu sana hawa mama zetu..
 
Na hata ukifanya ajali kwa gari kwa bahati mbaya na kwenye gari uko na mwanamke mfano umemgonga jamaa wa bodaboda...Ukipata upenyo muweke mwanamke kwenye streering chap kama yeye ndo alikuwa anadrive hakika shurba haitakuwa kubwa na yataisha salama...Uje ukutwe kwenye steering ni mwanaume utazungukwa na bodaboda kama buku na gari itachomwa.....Wana-nguvu sana hawa mama zetu..
Ha haa umenikumbusha tukio la juzi kuna mkaka lilimtokea
 
Valentina alimuweka binti kwenye usukani ama walichoma gari moto?....Boda boda wanaumoja wa ambayo ni hatari sana kwa wenye magari...
Ye aligongwa kwa nyuma,jamaa alivoshuka kuangalia aliemgonga akakuta ni mdada ikabidi jamaa hasira ziishie hapo....

Alichofanya yule jamaa akageuza kosa ili yule dada asionekane mkosa traffic watakapofika... Na jamaa akampeleka yule dada home
 
Ye aligongwa kwa nyuma,jamaa alivoshuka kuangalia aliemgonga akakuta ni mdada ikabidi jamaa hasira ziishie hapo....

Alichofanya yule jamaa akageuza kosa ili yule dada asionekane mkosa traffic watakapofika... Na jamaa akampeleka yule dada home
Hahahahah mko na nguvu sana kwenye hii dunia na ni wachache waliojua hilo na wanaitumia nguvu hiyo kikamivu na wengine hawajajua kuwa tangu kuzaliwa mko na nguvu sana unakuta wanateseka na kuumia kila kukicha...Shtuka na chukua hatua mda wa kuitumia nguvu hiyo ni sasa dada angu..
 
Hahahahah mko na nguvu sana kwenye hii dunia na ni wachache waliojua hilo na wanaitumia nguvu hiyo kikamivu na wengine hawajajua kuwa tangu kuzaliwa mko na nguvu sana unakuta wanateseka na kuumia kila kukicha...Shtuka na chukua hatua mda wa kuitumia nguvu hiyo ni sasa dada angu..
Kwakweli,mana jamaa anasema ghadhab zilimjaa ila zikayeyuka gafla

Kweli power of women ni noma,tunamshkuru Mungu kwa hilo
 
Ye aligongwa kwa nyuma,jamaa alivoshuka kuangalia aliemgonga akakuta ni mdada ikabidi jamaa hasira ziishie hapo....

Alichofanya yule jamaa akageuza kosa ili yule dada asionekane mkosa traffic watakapofika... Na jamaa akampeleka yule dada home
Sijui huko home kama alidai ujira
 
Na hata ukifanya ajali kwa gari kwa bahati mbaya na kwenye gari uko na mwanamke mfano umemgonga jamaa wa bodaboda...Ukipata upenyo muweke mwanamke kwenye streering chap kama yeye ndo alikuwa anadrive hakika shurba haitakuwa kubwa na yataisha salama...Uje ukutwe kwenye steering ni mwanaume utazungukwa na bodaboda kama buku na gari itachomwa.....Wana-nguvu sana hawa mama zetu..
Ukimiliki gari tafuta bastola kujilinda na bodaboda nyumbani bunduki kujilinda na majambazi
 
ILIKUWA JIONI MOJA TULIVU,,
MWANAMKE Mmoja Alielekea Kisimani
Kuteka Maji,, Alipokuwa Huko Kisimani
Mara Akatokea MWANAUME Mmoja Na
Kumuuliza Yule Mwanamke "samahani Dadangu Hivi Unaweza Kunitajia VISA
Vya MWANAMKE?".
Yule MWANAMKE
ghafla Akaanza Kulia Huku Anapiga
Makelele Kwa Sauti Sana, HaLi
ILiyofanya Wanakijiji Wengi Watoke
Mbio Wakiwa Na Mapanga Na Marungu Kuelekea Huko Kisimani!. Mara Yule
Mwanamke Akachukua Ndoo Ya Maji Na
Kujimwagia Mwili nzima, Wanakijiji
Walipofika Wakauliza Kwa HASIRA Kuna
Nini Hapa??.. Yule Mwanamke
Akajibu"Nilikua Nimetumbukia Kisimani Na Huyu Baba Ndio Ameniokoa".
Wanakijiji Wakampa Hongera Yule
Mwanaume kwa alichokifanya Kisha
Wakasambaa!. Yule Mwanamke
Akamgeukia Yule MWANAUME Na
Kumwambia "Hivyo Ndivyo VISA Vya Mwanamke, Ukimchukiza Anaweza
Kukuua Na Ukimpenda Anaweza Kukulinda''



Naomba namba ya huyo mwanamke, nimeshampenda tayari.
 
Na hata ukifanya ajali kwa gari kwa bahati mbaya na kwenye gari uko na mwanamke mfano umemgonga jamaa wa bodaboda...Ukipata upenyo muweke mwanamke kwenye streering chap kama yeye ndo alikuwa anadrive hakika shurba haitakuwa kubwa na yataisha salama...Uje ukutwe kwenye steering ni mwanaume utazungukwa na bodaboda kama buku na gari itachomwa.....Wana-nguvu sana hawa mama zetu..
Hapa kuna kajiukweli aisee
 
Back
Top Bottom