Hii nchi ya ajabu sana!!

Nyalotsi

JF-Expert Member
Jul 20, 2011
6,978
5,025
Leo kwenye uchambuzi wa magazeti radio one nimesikia kuna shule kibaha inawawekea alama nyekundu wanafunzi wenye vvu kwenye sale zao. Hivi,bado kuna unyanyapaa mpaka leo? Tukiamua kufanya namna hii, ni walimu,manesi,madaktari,wahasibu na watumishi wengine wangapi watawekewa alama? Hii kuambukizana kwa makusudi ni kwa sababu ya unyanyapaa,wangapi watarudi kwenye kuambukiza watu makusudi? Ni wangapi mpaka leo hatujapima na tunaendelea kutembea mtaani,na tutaogopa kwenda kupima?
 
it boared!!!,
Nafikiri kuna human rights violation hapo shuleni...jaman mashirika ya kutetea haki za wanadaumu mpoo?
 
itakuwa shule mnazoziita za international hizo,
siamini kama ni za jk nyerere.
 
Hata mimi nimeisikia hiyo habari kwenye briefing za magazeti,nadhani ni gazeti la Zanzibar leo,na hiyo issue ni Zanzibar sio bara,imeniboa sana nikajiuliza na waalimu wenye VVU nao wanawawekea Lebo,na kwanini wawekee wenye VVU tu,je wenye malaria,TB,Sickle cells.fungus etc kwanini wagonjwa wote wasiwekewe lebo,hii ni gross violation of human rights ,naomba wana harakati msiachie ili suala,kama ni kweli wahusika wapelekwe mahakamani,marufuku peke yake haitoshi
 
it boared!!!,
Nafikiri kuna human rights violation hapo shuleni...jaman mashirika ya kutetea haki za wanadaumu mpoo?

Wakijitokeza kutetea na serikali yetu babe si kesho utasikia wamepandishwa kisutu
 
Hata mimi nimeisikia hiyo habari kwenye briefing za magazeti,nadhani ni gazeti la Zanzibar leo,na hiyo issue ni Zanzibar sio bara,imeniboa sana nikajiuliza na waalimu wenye VVU nao wanawawekea Lebo,na kwanini wawekee wenye VVU tu,je wenye malaria,TB,Sickle cells.fungus etc kwanini wagonjwa wote wasiwekewe lebo,hii ni gross violation of human rights ,naomba wana harakati msiachie ili suala,kama ni kweli wahusika wapelekwe mahakamani,marufuku peke yake haitoshi

Hivi kwani suala la VVU nila muungano?
 
Kuna shule hapa dar zinafanya hivo ila wao wanawakea wanafunzi wenye magonjwa sugu kama kisukari. Nafikiri huu ni utaratibu wa wizara. Unajua TZ bwana mambo kama haya yakipingwa na watu wengi viongozi wa wizara wanakaa kimya kuogopa kashfa.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom