Forgotten
JF-Expert Member
- Jul 20, 2018
- 3,630
- 11,096
Kwakweli kwenye sekta ya Teknolojia hasa huduma za kifedha hizi kampuni zinatia hasira sana.
Jana nimefanya muamala kwa T-Pesa (TTCL) kwenda HaloPesa (Halotel) haukukamilika, nikawapigia simu huduma kwa wateja, masaa 24 yamepita muamala haujakamilika na pesa haijarudi kwenye akaunti.
Leo nimefanya muamala kwenda Selcom Pesa: pesa ikafika vizuri tu ndani ya sekunde kadhaa. Hiyo pesa nilikuwa nataka kufanyia malipo mtandaoni kupitia Virtual card. Cha kushangaza wakati nafanya malipo yakawa hayakamiliki, kurudi kwenye app ya Selcom Pesa nakuta Virtual card niliyotumia mara ya mwisho mwezi uliopita tu imefutwa na natakiwa ku-request card mpya. Nime-request card mpya bila mafanikio, nikaamua kufunga app, cha kushangaza zaidi sasa hivi siwezi kuingia kwenye akaunti yangu.
Sasa ningependa kujua, nchi hii ni huduma gani inayotolewa kwa uhakika?
Jana nimefanya muamala kwa T-Pesa (TTCL) kwenda HaloPesa (Halotel) haukukamilika, nikawapigia simu huduma kwa wateja, masaa 24 yamepita muamala haujakamilika na pesa haijarudi kwenye akaunti.
Leo nimefanya muamala kwenda Selcom Pesa: pesa ikafika vizuri tu ndani ya sekunde kadhaa. Hiyo pesa nilikuwa nataka kufanyia malipo mtandaoni kupitia Virtual card. Cha kushangaza wakati nafanya malipo yakawa hayakamiliki, kurudi kwenye app ya Selcom Pesa nakuta Virtual card niliyotumia mara ya mwisho mwezi uliopita tu imefutwa na natakiwa ku-request card mpya. Nime-request card mpya bila mafanikio, nikaamua kufunga app, cha kushangaza zaidi sasa hivi siwezi kuingia kwenye akaunti yangu.
Sasa ningependa kujua, nchi hii ni huduma gani inayotolewa kwa uhakika?