Hii mikasa inanipata mimi pekee?

Hii mikasa inanipata mimi pekee?

Kuna msemo unasema usilalamuke kwakuwa umeinguzwa shimo! Mradi uhai, unamikono, macho, akili, vyeti. Pambana mwanangu, piga moyo konde tafuta vyako, huo unyonge unauonyesha ndiyo ushindi wa huyo ndugu yako. Tafuta kazi pengine huku unafanya jitihada za kudai haki yako.
 
Katika kufanya hayo mtangulize Mungu na usisahau kutoa fungu la kumi kwa unachoingiza ktk biashara zako.Wakati mwingine tunapoteza mali,fedha na kazi kwa kuwa tunamwibia Mungu kwa kutokumtolea zaka na sadaka ya shukrani na mungu huamua kuchukua mibaraka yote na kukuacha ktk majaribu.Mrudie mungu wako hakika hatakuacha ktk shida yoyote ile

Hapo kwenye fungu la kumi ndio siri ya mafanikio yangu ilipo. Huwezi amini nikitoa 10% huwa naona maajabu ya Mungu. Napata baraka na pesa nyingi inaingia.
Ni sawa na Kulipa Kodi ya serikali. Usipolipa unaweza fungiwa biashara
 
Mtu anapata ajira pumbavu moja linatokea (kama lenyewe lilisoma vile) eti subiri uende chuo ili uende jeshini ukiwa na degree kabisa (my foot!). Kana kwamba hiyo ajira kaihifadhi kabatini vile na wewe ukamuamini.
 
Kaka katika kitu nilichojifunza usije mkategemea ndugu akutoe kimaisha. Utaumia sana man, mi mwenyewe nimesha experience ishu kama hiyo, ndugu yuko position nzuri serikalini lakin hakusaidii kwa lolote.
itisha kikao cha wana ukooo...
Au fungua kesi ya madai...

Usiache haki yako ipotee hivi hivi
 
Pole kwa changamoto hizo,lakini hayo ndio maisha na hapo ndipo pa kujifunza, wewe bado kijana, tena wa kiume, komaa tu, yote hayo yanapita na yatakuwa historia. Ushauri wangu;

1) Mkabili tena huyo ndugu yako, kwa heshima na unyenyekevu (kwa mara ya mwisho) mwambie kwamba una hali ngumu na una uhitaji sana wa fedha zakom, hivyo ni muhimu sana kwa sasa akupatie haki yako, akikupatia ni vema, lakini akigoma, basi achana naye, usisimamie tena biashara yake na umwambie ukweli kwamba hutaweza kuendelea kusimamia biashara yake wakati maisha yako yanakuwa magumu kila siku, na kwamba yote unamwachie Mungu. Usimtukane wala usimuambie maneno yoyote makali au mabaya. Usihangaike na kumshitaki popote, wala usifungue kesi ya madai, haitakusaidia na utapoteza muda na hutalipwa chako, wewe mshitakie Mungu, kisha endelea na maisha yako. Kwa maneno mengine ni kwamba, amekupa au hajakupa fedha zako, umeshajifunza vya hivyo, achana naye sasa!

2) Kuhusu kuoa - usikimbilie kuoa au kutaka na kuishi na mwanamke wakati maisha yako hayako sawa, kuwa mkweli kwa nafsi yako, kwamba unahitaji kujipanga upya. Kuna raha gani kuishi na mtu kwenye mazingira ya matatizo? Tena sio mkeo? Muambie ukweli huyo mwanamke wako kwamba, kwa sasa maisha/mambo yako hayako sawa na hutaki yeye aendelee kupata shida akiwa na wewe, wakati anaweza kuishi maisha bora huko nje. Mpe uhuru wa yeye kuondoka, kuendelea na maisha yake ili wewe ujipange na maisha yako. Akiamua kubaki ili mle vumbi wote pamoja, poa, maana hayo ndio mapenzi, lakini huo utakuwa uamuzi wake na utakuweka wewe huru ukiwa na amani. Ila ukila bingo na mambo yako yakinyooka huko mbeleni (Nina hakika yatakunyookea) utambue kwamba uda deni kwa huyo mwanamke - usije kujifanya mjanja, kumsaliti na mambo kama hayo.

3) Tatizo ni wewe, inabidi ubadilike hasa unavyotazama mambo na kuwalaumu wengine kwa makosa yako mwenyewe, kwa maamuzi mabovu uliyoyafanya mwenywe siku za nyuma. Kwanini uliacha kazi yako mwenyewe ya kufundisha na kuja kusimamia shughuli ya ndugu yako? Maana yake ni kwamba uliacha kujitegemea mwenyewe na ukarudi kumtegemea mtu mwingine (Kosa kubwa!), yaani maisha/hatima yako yote ulimuachia mtu mwingine na yeye hana sababu ya kuangalia maisha yako, anayepaswa kuangalia maisha yako ni wewe na sio yeye. Kwa mfano, ungebaki na kazi yako ya kufundisha na ukaendelea na biashara yako, leo ungekuwa wapi? Bila shaka mbali sana! Kwa mtazamo wangu ni kwamba huyo ndugu yako sio tatizo kwako, hiyo biashara yako kudorora nayo sio tatizo, hata kuishi maisha magumu nako sio tatizo kivile. Ni mungu au ulimwengu unakufundisha, kwamba badilisha maisha yako, anza upya, bado kijana, tena umesoma, anza kulitazama tatizo lako kama lako na pambana nalo na kama wewe, acha kulaumu wengine. Angalia ulipojikwalia na sio ulipoangukia. Tatizo liko akilini mwako, kwamba 'matatizo yangu haya, yanasababishwa na fulani', Huyo ndugu yako mtoe kabisa akilini mwako. Chukulia kila kilichotokea ni shule kwako. Ni Mungu na Ulimwengu unakupa fursa nyingine huku ukiwa umepata funzo kubwa la maisha.

Kila la heri
 
We Jamaa kilichokuponza ni kulidhika kushika Pesa za Mtu mwingine na kulala nazo ghetto. Ukahisi kama ni zako.
Huwezi kukataa kuwa ulikuwa humpigi ganji. Itakuaje Mtu akupi mshahara halafu uwe umelidhika kama nawe hauli ganji? Hata kama una miradi yako pembeni haiwezekani.

Boss wako anakufikiriaje akikuona una Pikipiki, Grocery na umeoa wakati akupi mshahara?
hahahahaaa kweli aisee ,unajua binadamu tunapimwa padogo sana inawezekana kutokukupa mshahara ni kipimo chake cha imani kwako
Dah kaka una washaur wabaya ever... katika historia yako pale tu ulipopata nafasi ya kubaki na kupata nafas ya kuingia jw a watu wakakwambia uendelee na uchuo ni uchawi tosha... by the way.. pole bro.. matatizo ni ya kwetu.. hapo amna namna ni kumfungulia Madai tu na ikiwezekana na tort juu
 
Kuna wanawake wengine ni nux hawaolewi nyota zenu hazienfani tafakari
 
Msamehe na uendelee na mipango mingine ya kutafuta pesa
Million 3 ni kidogo sana ukilinganisha na muda/pesa utakayoitumia ili upate haki yako kwenye vyombo vya sheria, pia kuuharibu kabisa uhusiano wenu coz hamna kitakachobadili kuwa huyo ni kaka yako, atakuwa kaka yako milele
MUACHIE MUNGU HE WILL DEAL WITH HIM
 
Haki hai ombwi bali ina daiwa,minakushauri kama vipi kinukishe kwa ndugu na marafiki zake,muwekeeee mabango kila mahali kuwa una mdai na hataki kukulipa,mtanganze kwa watu wanao mfahamu na wasiomfahamu,hakikisha mpaka wafanyakazi wenzake wajue una mdai ila hataki kukulipa ana nia ya kukudhulumu,mtangazeeeeee kila mahali aisee! Mpaka ajutie tabia yake ya udhulumati,halafu jitahidi uache kufanya kazi kwake kafanye shughuli zingine huku ukiendelea kumtangaza kila mahali mpaka akulipe dadeki.
 
Masahibu madogo tu hayo. Pambana kiume yatapita. Mi nilijua bonge la ishu.
 
Mtu na elimu yako kwann unga'ang'nie hapo, kwanza ulifanya kosa una mafunzo ya kijeshi mazuri unazubaa mitaani, ulikua pale pale ulipopata mafunxo uingie jeshini badae ungechukua degree kaxini na kupandishwa cheo na mshahara mzuri, nakushangaa sana mtu na elimu yako na ujuzi wako unamrumikia mtu anakuzoritesha hapo nawe unakubali, swala la ndoa sio baya mana umejikinga na zinaa, ilo huyo jamaa co poa kwako, mrejeshee kampuni yake, nawe pambana na hali yko kivyako
wazi mkuu!!
 
Msamehe na uendelee na mipango mingine ya kutafuta pesa
Million 3 ni kidogo sana ukilinganisha na muda/pesa utakayoitumia ili upate haki yako kwenye vyombo vya sheria, pia kuuharibu kabisa uhusiano wenu coz hamna kitakachobadili kuwa huyo ni kaka yako, atakuwa kaka yako milele
MUACHIE MUNGU HE WILL DEAL WITH HIM
ahsante ndugu
 
Huwa naona huruma sana kwa kijana anaejituma na kutafuta maisha halafu mtu anamuharibia pole sana. Usikate tamaa
 
Huyo jamaa anaroho ya kutu aseeeh.. yeye inaonekana ni wa kutumia watu tu hasa ndugu zake kwa faida yake na hili ungelielewa mapema kabla ya kurudi mara ya pili.


Naamini hakuna njia moja ya kutatua tatizo moja. Ingekuwa mimi ok ok DC lookningemfanyia haya.

1. Kulipeleka kwa wazee wa ukoo wanaoheshimiwa na ndugu zenu mlizungumze kwa undani. Ikishindikana...

2. Kwenda kwenye vyombo vya sheria hasa kwa kuanzia kwa serikali za mitaa ikiwezekana ni kiongozi basi ataona aibu yakishindikana fungua kesi.

3. Kama nipo position ambayo nashika pesa za kampuni ningejilipa tena zaidi ya ninachomdai ili aonje niliyoonja.

Mimi kwenye ishu za kumdai mtu natumia ubabe..kama nakudai nakuja kwako nakujabmisha nakupa siku 2 kwa hili nimefanikiwa kwa aslimia nyingi.
Ushauri mzuri Sana. Mkuu tafuta MTU mkumbwa kama uncle aongee naye.
Ndugu wana jamii forum Nawasalimu kwa jina la Mnyezi Mungu Muumba wetu.
Io
Naleta maada hii kwenu ili kuwaeleza maswahibu yanayoniandama moyoni mwangu ili kama kuna yeyote aliyepitia basi tupeane faraja.

Mimi ni kijana wa kiume ambapo tarehe 30/12 mwaka huu ntatimiza umri wa miaka 26, nikiwa kidato cha sita mwaka 2012 nilipoteza baba na mama walipopata ajali na kufariki, kumbuka Mimi ndio kijana pekee wa kiume na Dada yangu mkubwa tu, nilijikaza kiume ambapo mwaka 2013 februari nlihitimu kidato cha sita, Nilijiunga na mafunzo ya JKT pale Ruvu JKT, bahati nzuri nlikuwa moja ya wanafunzi bora waliofanya vizuri kwenye shabaha na kuahidiwa kuingizwa JWTZ iwapo tungependa.

Nilishauriwa na ndugu na jamaa kuendelea na elimu ya chuo kikuu ili hata kama nataka kujiunga JW niwe na shahada tayari, nliamua kusoma degree ambapo 2016 julai nlihitimu elimu ya chuo kikuu, nlipata shule ya kufundisha ya private,

Miezi michache baadae nlikutana na kaka yangu wa ukoo ambaye ni moja ya viongozi wakubwa katika awamu hii ( sitaji jina) aliniomba niache kufundisha ili nikasimamie mradi wake huku akiahidi kunilipa mshahara kila mwezi. nilikubaliana nae....nlianza kazi vizuri katika huo mradi miezi kadhaa ikapita hata kupewa mshahara wangu kitu kilichopelekea Mimi kuanza kuuza mpunga nlionunua huko morogoro kwa mama mdogo ili nijikimu kimatunizi na mambo mengine.

Baada ya mda Mimi na Dada yangu tuliamua kugawana pesa ambayo iliachwa na wazazi wetu, nlipata kama milioni tatu hivi ( 3,000,000/=). Nlinunua kiwanja na kufungua biashara ya Grocery ambayo ilikuwa ikinilipa vizuri tu, mda huo nliendelea kufanya kazi kwenye kampuni ya huyu kaka angu japo nlizidi kuwa na malimbikizo ya mshahara wangu maana sikuwa nikilipwa kila mwezi.

Sikujali hilo na nikapata Dada mmoja ambaye baadae nikaamua kumuoa japo bado hatujafunga ndoa rasmi lakini nlishajitambulisha kwa wazazi na nduguze mambo yakawa sawa,

Zengwe limekuja hivi karibuni ambapo biashara ya hiyo grocery ilianza kudorola na kujikuta mambo yangu hayapo sawa kabisa,
Pia nimeundiwa zengwe la kuwa Nina loss kwenye biashara ya jamaa ambapo malimbikizo yangu tangu nianze kufanya kazi yanafikia milioni tatu hivi!!! niliamua kuchukua mkopo ili nifufue grocery yangu ambayo ndio inanipa ridhiki ya kila siku,

Ninaumia sana jamani hasa nikikumbuka kuwa nilipata ajira ya kufundish nikaiacha kwa kulaghaiwa na mtu mkubwa wa karibu ninayemuamini sana.

Mpaka inafika mda nawaza bora nisingeoa huyu binti wa watu ili nisimuweke kwenye hali ngumu kama hii maana naelekea kudhulumiwa haki yangu huku hali yangu mbaya kiuchumi,
imefikia hatua nataka niuze pikipiki yangu ili nijaribu bahati zingine. maana sina namna sasa.

Naombeni ushauri nifanyeje ili nipate haki yangu toka kwa huyu (kigogo) kaka yangu.
NB: naomba ushauri jamani na uzoefu wenu.

Mkuu I wish you well, keep going we are all coming in from the cold, from difficulties. That is our lives. Blessings and best wishes.
 
Ushauri mzuri Sana. Mkuu yachts MTU mkumbwa kama uncle


Mkuu I wish you well, keep going we are all coming in from the cold, from difficulties. That is our lives. Blessings and best wishes.
thankiu comrade!! I swear to fight till the grave takes me off!! tuombe uzima.
 
Me nianze kukulaumu kwamba uliona mwezi wa kwanza unapita hulipwi wa pili wa tatu na ww umeng'ang'ana na kukaa kimya wakati makubaliano ni mlipane!!!

Kuna watu wana makubwa zaidi ya hilo na wanapojikwaa huendelea mbele wanasahau ya nyuma sasa najua kuna ulichojishauri tayari pamoja na hilo angalia fursa ulizoambiwa na wachangiaji hapo juu usonge mbele tena bahati yako unacho hata cha kuanzia
 
Back
Top Bottom